Kamanda wa Operesheni maalum Paul Chagonja amemtisha Dr Ulimboka Stephen kwamba kauli zake juu ya kumtambua ACP Msangi kwamba alihusika kumteka zitamgharimu mwenyewe.
Kamanda Chagonja amesema hakuna hata mtu mmoja anayejua ni nani alimteka na kumpiga Dr Ulimboka na ndiyo maana tume maalum inafanya uchunguzi.
Katika kejeli na kiburi cha hali ya juu Kamishna Chagonja alihoji mbele ya waandishi ''NANI ANA UHAKIKA JE KAMA ALIKAMATWA NA MKE WA MTU NDIYO AKAPIGWA?''
Source:Mtanzania Jumamosi.
Katumwa kupoza kidogo wakati ndiyo kwanza anajipaka dhambi mwenyewe!Yeye si angekaa kimya kupisha uchunguzi vitisho vya nini?
Katumwa kupoza kidogo wakati ndiyo kwanza anajipaka dhambi mwenyewe!
No no no no no Kamanda, yuko mtu mmoja anayejua nani alimteka na kumpiga Dr Ulimboka, huyo mtu anaitwa Dr Ulimboka. Get real!
Kwenye blue: Vitisho haviishi?
Huku sasa ni kuingilia mambo na sasa tumsikilize nani, hapo ndipo ninapoamini JK kaiaribu nchi hii kwa kuwaendekeza watu hasa viongozi kutotambua wajibu wao ndio maana utaona waziri vs naibu wake wakipingana sasa Chagonja na Kova tumsikilize nani? Harafu tume imeundwa then anasema Dr. Uli itamgalimu kwani yy ni mjumbe ktk tume mbona anaanza kuhukumu kabla?