Telewolth bin champion
JF-Expert Member
- Dec 11, 2018
- 2,738
- 7,253
Kakudanganya nani kuwa kudisable app kunaizuia kuchukua taarifa zako?Kwenye samsung yangu ipo na naweza ku disable nikitaka
View attachment 3504448
Iko hivi kuna level 3 za uingiliaji wa privacy unaofanywa na hizi Softwares(apps za simu/Computer) kwa malengo fulani.
๐Level ya kwanza ni ile ambayo apps inachukua taarifa zako baada ya wewe kukubali terms+conditions pale unapoitumia hiyo app, na mara nyingi uingiliaji huu haunaga madhara makubwa kwani unahusu kuchukua taarifa kadhaa za mteja/user ili kumsaidia kujua haki zake kimtandao na matumizi sahihi ya data zake, pia kumlinda dhidi ya attacks kutoka kwa malwares, pia kumpa huduma stahiki.
๐Uingiliaji wa pili ni ule ambao software zinakuomba wewe mtumiaji ruhusa ya chombo chako(computer/smartphone), kuruhusu baadhi ya features kuwa active katika kifaa chako ili kuwarahisishia wao wamiliki wa hiyo software kupata control ya kuzipata data kirahisi huku ukiahidiwa kupata secure service/huduma bora zaidi, au ufanisi mkubwa zaidi, na hapa ndipo mtaona baadhi ya apps kuomba permission ya location, Camera, microphone, storage, calendar, hii yote ni kuwasaidia wao kupata full control ya kifaa chako baada ya wewe mwenyewe kukubali.
๐Uingiliaji wa TATU na wa mwisho huu unahusu software yenyewe kuchukua data/taarifa zako bila ya wewe kuruhusu iwe unapenda ama hupendi, na hii hufanyika pale unapodownload app husika au kuwasha data ktk kifaa chako au kwa baadhi ya softwares/ apps ziilizokuja na Operating system ya kifaa(Android/window/iOS) kama Google, Gmail, google map, google photos, na nyinginezo baada tu ya kuactivate account ktk kifaa chako huanza kuchukua taarifa zote za kifaa chako kwa kupenda kwako ama kutokupenda, kwakujua ama kutokujua.
Na taarifa hizi huwasaidia wamiliki wa software hizo ktk mauzo ya taarifa kibiashara na ushindani wa masoko ya rasilimali watu, pia ujasusi kwa baadhi ya mataifa target na watu target wenye maslahi na watu fulani, na uingiliaji huu wa taarifa huwezi kuuzuia kwa njia yoyote ile bali unaweza tu kuuchelewesha ama kuupunguza speed au kudanganya baadhi ya data lakini haiondoi ukweli kuwa kila ufanyacho kinakuwa recorded na kinatunzwa Kwa matumizi ya baadae kama kinafaa.
Ktk technology hakuna kinachopotea asikudanganye mtu kuwa kufuta kitu ktk simu yako inakuwa imeisha hilo halipo, kila ufanyacho ktk mtandao kinahifadhiwa ktk data centers ambapo umuhimu wake ndio utaamua kitumike au kiwe useless.
Mfano mdogo tu, kuna apps zinaweza kukupa picha yako ambayo hujui kama ulipigwa wakati ukitumia simu, sauti yako yako ambayo hukujua kama ulirecordiwa, fingerprints zako, aina ya tabia yako kulingana na maeneo unayopendelea kuingia ktk mitandao, au maeneo unayoshinda physically au watu unaokutana nao na kuwasiliana nao, hili mtambue kuwa, wenye technology sizungumzii hawa wa huku kwetu wasiojua hata kuinstall windows ktk computer zao.
Nazungumzia watu wa dunia ya kwanza wakiamua kukupata watakupata tu hata ufiche taarifa zako zote, ila siku ukajiroga kutumia simu yoyote yenye screen touch na front camera jua umekwisha, taarifa zako za sura na fingerprints zitawapa maelekezo yote, na kitendo tu cha kutumia kifaa cha Android OS, windows OS, jua umekwisha.
WE ARE NOT SAFE