Teknolojia ni Yetu sote
JF-Expert Member
- Apr 28, 2020
- 1,221
- 2,425
Inawezekana umeshangaa au kushtuka lakini Kuna habari inasambaa mtandaoni kuhusu app ya Siri ambayo imewekwa kwenye Simu za Samsung haiwezekani kufutika ikiwa unataka kuiondoa.
App hiyo inaitwa Appcloud, ni app ambayo Kwa miaka mingi, inajihusisha na masuala ya kibiashara ikikupa uwezo wa kuinstall app nyingine ndani ya Simu Yako. Ni app ambayo imeundwa na Israeli kupitia Kampuni ya IronSource ambayo Kwa sasa inamilikiwa na Kampuni ya Unity Toka Marekani.
App hiyo haiwezekani kufutika kwani inafuatilia taarifa mbalimbali za Siri za watumiaji wa Simu za Samsung bila wao kujua. Kuna ripoti inaonyesha baadhi ya nchi zimeanza kupiga marufuku Matumizi ya Simu za Samsung kutokana na tabia zake.
Japo Samsung walikana Kwa kusema " Wao Wanatengeneza vifaa ambavyo ni salama Kwa watumiaji wake Kwa kufuata kanuni na sheria za Eneo Husika".