Kama umezaliwa 90's usipite hapa maana huna experience

Kama umezaliwa 90's usipite hapa maana huna experience

Hahahahahahahahahaha! Bro you make my day!

Hahahaha!!Hehehehe!!kho kho kho!!hizo style zote nimepitia mkuu,yakusimama kwenye kona ya ukuta zen unabinuka kidogo wowo.....acha tu yaaaaaaaaani!!
 
45...Bakora kama hukwenda zamu wakati wa likizo
46...Bila mfagio na kidumu cha maji huhesabu Namba hata kama umewahi SULUHU ni kwenda fasta shimoni kuokota 'chelewa' azima kidumu cha aliehesabu mpango mzima
46...Ukivaa raba yenye lebo DH utakoma madongo eti 'dingi hana uwezo'
48...Kuwabebea manati vilanja wanoko,atakoma wakati wa kupalia kahawa au kulima mnajikusanya mlipua manati anakaa kati fyuu!
49...Kama darasa lenu dirisha halijabomoka nyie darasa la washamba
50...siku ya kumaliza mitihani LY lazima mle ubwabwa,mkwangue madeski...
51...Usiombe awe anakuja kiongozi wa serikali full mazoezi ya kwaya na utamaduni ili mkamwimbie...NAKUMBUKA "Karibu saana mbunge wetu naibu waziri Mwambulukutu" nadhani ni balozi wa tz s/africa...AU wanautamaduni tunaingiaa mamaaa tumetoka mbali Msalilwa na Msalilwa....
52...Wanuka chupi yaani vikojozi full kuzomewa
53...Yanapigwa makofi Heeshimaa toa shikaaamooo mwaaalimu,mwenzio wa deksi la nyuma ashakutegea peni nyuma,unamfingia ngoja atoke ticha
54...Nakumbuka 'wanoko' waliokuwa wataalamu wa kutafuta stiki/bakora nzuri, basi maticha wapenda fimbo watamtuma kila siku halafu yeye hachapwi
55..._Tuligawiwa Madaftari ya 'HALIUZWI NI KWA NATUMIZI YA SHULE TU'
56...Pooh
 
Haya Mambo Huwezi Kuwa Umepitia kama Umezaliwa Baada ya Mwaka 90...
1. Kupakwa GV kwenye kidonda
2. Kung'olewa jino kwa uzi
3. Ubwabwa kupikwa j2 tu
4. Kidonda kuwekwa unga wa 'rangi mbili' a.k.a tetesakrin
5. Kupamba kadi na pamba sebuleni
6. Ukumbi wa sherehe kupambwa kwa toilet paper
7. Kunyolewa na mkasi
8. Kufunga pesa kwenye leso au pindo la kanga
9. Wavulana Kuvaa Nguo ya ndani aina moja nchi nzima VIP, usiombe ikakatika ukakuta imebana Kifua.
10. Ku rewind kanda kwa peni
11. Nchi nzima Kuangalia Movie ya Commando John, Double Impact, Rambo na Bluce Lee..
12. Watoto Wa Mtaa Mzima Kufahamiana sababu ya kucheza Wote Jioni Kombolela na Kibaba..
13. Kuunguzana na tunda ya Ubuyu baada ya kuisugua chini
14. Kukata ndala, ati ni kifutio
15. Kunyolewa msalaba shuleni kisa nywele ndefu
16. Kuweka Vibox box kwenye Shati la shule Mgongoni..
17. Kuweka Shati la Shule "Blue" eti liwe zuri.
18. Ubitoz Ulikuwa ni Kusimamisha Kora Ya Shati.
19. Ukiandika Barua kwa Umpendae lazima uchore moyo na Mkuki na lazima upulizie Pafyumu ya "YU".
20. Hata kama Mlikuwa mmegombana January lakini Mtu anakuambia "Utaipata Siku Ya Kufunga Shule".

Je wewe unakumbuka nini??

we mkuu kiboko!!!
 

  • [*=1]Choo ya shule haikuwa na maji kwa ajili ya mtawazo, badala yake unatembea na gunzi mfukoni, au majani ukikosa vyote unatazama kulia na kushoto hamna mtu unakaa ardhini unasota harakaharaka au ukizidiwa kwenye kona ya ukuta then unatimua,


  • [*=1]Kutumia u.p.u.p.u kukomesha wanaotumia kuta na sakafu kama toilet paper mbadala, akiingia darasani utatambua tu kuwa huyu kakiuka kanuni za mtu ni afya, kiti kinakuwa hakikaliki

Daaaah... hii kali ... nmecheka mbaya
 
Kutengeneza bembea kwenye matawi ya miti na kuanza kusukumana... ikikatika sasa ndio utaona mziki wake..... utarushwa kulee unaugulia maumivu

Kucheza kibaba na mama ikifika mda wa kulala mnaende kugusishana vikojoleo tena utakuta nda ndugu yako
 
Kupiga salute ndege ikipita (shikamoo ndege)

Kusimama barabarani na kuwahi magari yanayopita , ( eeeehh Hilo langu..... like linalokuja langu )

Kucheza bong'oa ukiinama tu unapigwa take kwa nyuma.

Kudaka maua yanayodondoka na kuweka mfukoni ukiamini itageuka hela.


Kupiga chabo ilikua ni issuekichizi
 
sema kwa huku kijijii kwenu dsm mambo hayakuwepo kabisa

Ndio maana jamaa alisema wa 90's msipite hapa,hapo hakuna ambalo Dsm hatukulifanya mimi nimezaliwa na kukulia Msasani nyuma Drive in Cinema enzi hizo sasa ivi ni US EMbassy na bado yaliyotajwa karibu yote nimepitia.
 
45...Bakora kama hukwenda zamu wakati wa likizo
46...Bila mfagio na kidumu cha maji huhesabu Namba hata kama umewahi SULUHU ni kwenda fasta shimoni kuokota 'chelewa' azima kidumu cha aliehesabu mpango mzima
46...Ukivaa raba yenye lebo DH utakoma madongo eti 'dingi hana uwezo'
48...Kuwabebea manati vilanja wanoko,atakoma wakati wa kupalia kahawa au kulima mnajikusanya mlipua manati anakaa kati fyuu!
49...Kama darasa lenu dirisha halijabomoka nyie darasa la washamba
50...siku ya kumaliza mitihani LY lazima mle ubwabwa,mkwangue madeski...
51...Usiombe awe anakuja kiongozi wa serikali full mazoezi ya kwaya na utamaduni ili mkamwimbie...NAKUMBUKA "Karibu saana mbunge wetu naibu waziri Mwambulukutu" nadhani ni balozi wa tz s/africa...AU wanautamaduni tunaingiaa mamaaa tumetoka mbali Msalilwa na Msalilwa....
52...Wanuka chupi yaani vikojozi full kuzomewa
53...Yanapigwa makofi Heeshimaa toa shikaaamooo mwaaalimu,mwenzio wa deksi la nyuma ashakutegea peni nyuma,unamfingia ngoja atoke ticha
54...Nakumbuka 'wanoko' waliokuwa wataalamu wa kutafuta stiki/bakora nzuri, basi maticha wapenda fimbo watamtuma kila siku halafu yeye hachapwi
55..._Tuligawiwa Madaftari ya 'HALIUZWI NI KWA NATUMIZI YA SHULE TU'
56...Pooh

Haaaaah we kiboko jamani mule mule nimeimba sana kwaya daaah
 
62. Kucheza kimama mama na mchezo mbaya kwenye majumba mabovu
63. Kujipikilisha philipo anaiba mchele kwao, Mwajuma anaiba moto halafu mnakutana kichocholoni kujipikilisha.
64. Ukikutana na polisi lazima umuamkie
65. Magari ya udongo
66. Magari ya mbao
67. Magari ya mabati au madebe
68. Kukata picha za wachezaji kwenye magazeti na kubandika kwenye madaftari
69. Kucheza kamali ya goroli
70. Cku mkila wali lazima mtaani na wenzio ajue kwakuwa unabakiza puche pembeni ya mdomo
71. Kupinga na kupingua urafiki
72. Kwenu kukiwa na tv mademu wote mtaani wanataka wawe wachumba zako
73. Kuamka saa kumi na moja alfajili kuangalia Tyson na Bruno kwa jilani.
74. Siku ukinunuliwa chips mayai jua unaumwa na daktari kasibitisha hilo
75. Mwalimu wa nizamu anaogopeka kuliwa mwalimu mkuu
76. Tulibeba sana vibeg vya sport vilukuwa vidogo unafunga kwa kuvuka kamba huku na huku.

=====>>>
 
..hiyo yaa vibegi vya sport nakumbukaa saanaa
....mwisho mwisho yakaja mabag ya saa wanaobeba wale watoto wa wakishuaaa
...viatu vya kipaimara lazima uendee navyo shule...shule ikifunguliwa ukawaonyeshe
... kusoma gazeti la SANI ndio fashion ya kipindi hiko..Ananunua uncle wake mtu mtaani linazunguka mtaa mzima
... nyumba yenye mpera...kila mtoto halali yake kuupanda kuchuma mapera
...Mchana wa saa saba kila nyumba sauti inatoka ya kuitwa home Samweeeeeliiiiiiii,,,,Jeniiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii
...Kupelekwa majumba ya sinema kwa sisi wenye kipato cha afadhali...Drive in,Avalon,Empire,New Chox
---Kusoma Magazeti Ya Uhuru,Mfanyakazi na Mzalendo tuuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom