Mwanamageuko
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 8,602
- 5,569
Ikiwa tunaamini kuwa kiogozi fulani ni bora na atatuvusha kutoka A kwenda B Tunajidanganya!
Ikiwa tunaamini kwamba Chama fulani ndicho bora na kitatukomboa basini dhahiri kabisa
TUMEPOTOKA!
Ukombozi wa kweli utatokana na wananchi wenyewe watanzania na si vyama vya siasa hivi tulivyonavyo. Hivi vyama tulivyonavyo bado vina uasilia wa CCM kataeni ama kubalini huo ndio ukweli wenyewe.
Kama kuna mtu anaamini katika vyama basi na ajiulize mbona ndani ya vyama vyenyewe wanashindwa kukubaliana kutokubaliana? Kama wao wanajenga demokrasia kwanini wanajengena chuki na kutengana kwa mawazo yasiofanana? Je kwanini baadhi wanataka kuwafunika wengine waonekane wao ndio CHAMA chenyewe? Je vyama hivi vikiwa vina wenyewe kama ilivyo CCM ukombozi utatokea wapi!?
Ndugu zangu,
Tunapaswa kubadilika na kuitazama Tanzania tuitakayo, tunapaswa kutafakari vipi iwe Tanzania ijayo. Na ikiwa ndivyo hivyo basi tutambue ya kwamba kwa uhakika mpaka sasa hatuna chama hata kimoja (hivi tunavyoita vya upinzani) ambacho kipo kwa maslahi ya watanzania.
NI MVINYO ULE ULE KATIKA CHUPA MPYA!
Ikiwa tunaamini kwamba Chama fulani ndicho bora na kitatukomboa basini dhahiri kabisa
TUMEPOTOKA!
Ukombozi wa kweli utatokana na wananchi wenyewe watanzania na si vyama vya siasa hivi tulivyonavyo. Hivi vyama tulivyonavyo bado vina uasilia wa CCM kataeni ama kubalini huo ndio ukweli wenyewe.
Kama kuna mtu anaamini katika vyama basi na ajiulize mbona ndani ya vyama vyenyewe wanashindwa kukubaliana kutokubaliana? Kama wao wanajenga demokrasia kwanini wanajengena chuki na kutengana kwa mawazo yasiofanana? Je kwanini baadhi wanataka kuwafunika wengine waonekane wao ndio CHAMA chenyewe? Je vyama hivi vikiwa vina wenyewe kama ilivyo CCM ukombozi utatokea wapi!?
Ndugu zangu,
Tunapaswa kubadilika na kuitazama Tanzania tuitakayo, tunapaswa kutafakari vipi iwe Tanzania ijayo. Na ikiwa ndivyo hivyo basi tutambue ya kwamba kwa uhakika mpaka sasa hatuna chama hata kimoja (hivi tunavyoita vya upinzani) ambacho kipo kwa maslahi ya watanzania.
NI MVINYO ULE ULE KATIKA CHUPA MPYA!