T2015CCM
JF-Expert Member
- Sep 13, 2012
- 7,931
- 987
Umevurugwa wewe. Endeleeni kulisha watu sumu, kuwamwagia tindikali, kuwalipua mabomu na kuwatishia kuwauwa kwa bastola.chadema ni janga la kitaifaHii inatokana na ukweli kwamba, mtanzania ni mvivu wa kufikiri na mvivu wa kudai haki yake ya msingi. Ingekuwa nchi nyingine, serikali ya CCM ingeshaondolewa kwa sababu,
Hizi ni sababu tosha za CCM kuendelea kututawala kwa miaka 300 ijayo. hiyo imethibitishwa na Mbakajai Kapuya kwamba hao ndio wenye nchi na hakuna tunaloweza kufanya. CCM hoyee !!!!!
- Viongozi wake wanatuhumiwa kufanya biashara ya madawa kulevya lakini hakuna kinachofanyika zaidi ya kuwalinda. Hadi wanajigamba kwamba wao ndio wenye nchi, watoto wao wanauza unga na hakuna wa kuwakamata
- Viongozi wa CCM wanakula rushwa, ni mafisadi wakubwa lakini hakuna wa kuwachukulia hatua yoyote, zaidi wanatetewa na masikini wa kutisha kwenye mitandao kama Ze macorpolo, Chama ritz etc….
- Sheria za Tanzania ni kwa ajili ya kuwalinda mafisadi na familia zao na kuwakandamiza raia masikini
- Viongozi wa CCM wanatuhumiwa kuficha fedha nyingi sana nje ya nchi lakini hakuna wa kuwachukulia hatua
- Viongozi wa CCM wanabaka watoto, wanawapa UKIMWI na hilo likawa tu ni upepo wa kupita
- Uspika na Bunge la Tanzania vimekuwa ni vilabu vya kupitisha na kulinda agenda za watawala wa CCM.
- Vyeo vya uongozi vinagawiwa kwa undugu, urafiki na ufuasi
- CCM itaendelea kutawala kwa sababu polisi wanawaua raia lakini hakuna wa kuwajibishwa, badala yake wanapandishwa vyeo
- CCM itaendelea kutawala kwa sababu ukibishana nao, either unauwawa, unamwagiwa tindikali, kung'olewa kucha au kupotea katika mazingira ya kutatanisha
- Huu ukoo wa panya umeweza kutupumbaza kwa kuwapa watoto wetu elimu duni ili waendelee kuwa wajinga wa kutaliwa
- Serikali ya CCM imeweza kuiuza nchi kwa wachina ambao wanaiba rasilimali zetu kwa kasi ya ajabu. Imefika hadi viongozi wao, kama balozi kuingilia mambo yetu ya kisiasa bila kuchukuliwa hatua.
- Serikali ya CCM imekaa kimya huku raia wa kichina wakitengeneza madawa ya kulevya kwenye majumba yetu wanayokodi huku wakilindwa na watawala
- Serikali yetu itaendelea kututawala kwa sababu, licha ya kwamba ajira ni tatizo nchini Tanzania, wafungwa wa kichina wanaletwa kufanya vibarua huku vijana wetu wakiwa kandoni mwa barabara wakiangalia
- CCM itaendelewa kuwa madarakani kwa miaka 300 kwa sababu wameweza kubuni namna ya kugawa vyama vya upinzani kuwatumia mamluki, wasaliti na watu ambao wameonyesha tamaa ya fedha na madaraka kwa kuwapa kiburi na yale yote mazuri wanayoyatamani mamluki hao
- Licha ya kwamba baadhi yetu, hatuwezi hata kujinunulia au kukodi sehemu ya maana ya kulala, tumeendekeza njaa zetu za pilau, Buku 7, tisheti tukifuraia kuwa neema kwetu huku mafisadi ya CCM yakichota mabilioni ya kodi na kuzipeleka nje kwenye akaunti zao.
- CCM itaendelewa kuwa madarakani kwa sababu Mahakama imekuwa ikilinda zaidi viongozi wa CCM na mafisadi wanaoua, kubaka, huku raia wanaobambambikiziwa kesi kusote kwa miaka 20 magereza bila kesi zao kusikilizwa