GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,647
- 109,034
Kuna taarifa (si rasmi bado naendelea Kuzichunguza) zinadai kuwa Tiketi nyingi za 'Simba Day' zilizonunuliwa huku Uongozi wa Simba SC ukifurahia SOLD OUT yake wakiamini kuwa Uwanja wa Benjamin Mkapa utajaa hadi Pomoni Keshokutwa zimenunuliwa na Matajiri wenye UMAFIA wa Yanga SC kwa Makusudi ili Mashabiki wa Simba SC wakose Tiketi na Uwanja usijae kisha Simba SC Waumbuke na Wachekwe kwani kama kweli Uwanja ukijaa (Nyomi likiwa ni la Kufa Mtu) kwa Mkapa hadi Uhuru itakuwa ni Fedheha (Aibu) kubwa kwa wana Yanga na Klabu yao ya Yanga SC inayojinasibu kuwa na Mafanikio makubwa ya ndani na nje ya Uwanja.
Hivyo basi GENTAMYCINE nichukue nafasi hii Kuuomba Uongozi wa Simba SC na hata Watendaji wa Serikali na Vyombo vyake muhimu (hasa Watu wa TISS) kulifuatilia na kulichunguza na kama lina Ukweli basi ni muda sahihi sasa kwa Klabu ya Yanga kuchukuliwa Hatua kwani wanachokifanya sasa (kama hii taarifa ni ya kweli) siyo Uungwana na Uanamichezo bali ni Vita rasmi ya Ugaidi Michezoni (Mpirani) na ikiachwa ipo Siku itatupeleka kubaya na Mpira Wetu utakuwa ni Vita Kamili na siyo Burudani tena kama lilivyo Lengo Mama la wenye Mamlaka nao (nalo) akina FIFA Kidunia na CAF kwa Afrika.
Tutaniane, ila tusileteane Uhuni!!!
Hivyo basi GENTAMYCINE nichukue nafasi hii Kuuomba Uongozi wa Simba SC na hata Watendaji wa Serikali na Vyombo vyake muhimu (hasa Watu wa TISS) kulifuatilia na kulichunguza na kama lina Ukweli basi ni muda sahihi sasa kwa Klabu ya Yanga kuchukuliwa Hatua kwani wanachokifanya sasa (kama hii taarifa ni ya kweli) siyo Uungwana na Uanamichezo bali ni Vita rasmi ya Ugaidi Michezoni (Mpirani) na ikiachwa ipo Siku itatupeleka kubaya na Mpira Wetu utakuwa ni Vita Kamili na siyo Burudani tena kama lilivyo Lengo Mama la wenye Mamlaka nao (nalo) akina FIFA Kidunia na CAF kwa Afrika.
Tutaniane, ila tusileteane Uhuni!!!