Kama siyo Magufuli kuwaokoa 2015 na agenda ya mabadiliko CCM, leo ingekuwa chama cha upinzani

MSHINO

JF-Expert Member
Jul 26, 2013
1,067
709
Katika binadamu aliowaumba hapa duniani watanzania aliwapa sifa na vipawa tofauti kama ifuatavyo

  • Wakati MUNGU amewaumba wanadamu kusahau lakini wamepewa uwezo wa kukumbuka lakini Watanzania MUNGU ametuumba kusahau milele bila kukumbuka.
  • Mungu aliwaumba Watanzania kuwa wapole na wavumilivu
  • Watanzania Mungu aliwaumba kwa kuwapa woga kutohoji au kuuliza hata kama wanaumia mioyoni.
  • Watanzania wameumbwa kuwa wakarimu huku wakiugulia moyoni hata kama ukiwauliza wanaonaje maisha utasikia mambo ni poa hata kama siyo sawa.
Nimeanza na MUNGU kwa sababu miaka 6 iliyopita hakuna mtanzania asijua kilichofanyika katika siasa za Tanzania. Hivi nani asiyejua kuwa Lowasa alikuwa achukue nchi km siyo watu kuamua kwenda na JPM badala ya CCM? Kwa sababu wananchi walishakichoka hiki chama. Kwa hiyo wana CCM wenzangu tuweni na kumbukumbu 2025 siyo mbali.
 
Back
Top Bottom