kwa wana jf wote
cc:
invisible paw na wengineo
kama nitakufa leo, nisiuone mwaka mpwa 2014, kama nitaanguka leo hii macho yangu yakafumba nisiione tena kesho, kama nitakufa leo hii, yaani nisiione tena jf, nisiwaone na kuchati na mmu members, chitchat heroes yaani kama nitakufa leo hii.
Najua nitakwenda mbinguni, kule watu waendako wasirudi tena, nitaendelea kuwakumbuka, kuwaombea na kuwapenda. Nitawaombea
ritz na
chamviga wapunguze visasi dhidi ya chadema ntaowambea
cathode ray arudi jukwaani maana tangu afunge ndoa ndio kaifunga na jf, nitamuombea
zumbemkuu apunguze lugha ya ukali dhidi ya ccm. Nitawaombe mabinti wote wa jf na akina kaka wanaotafuta wachumba, kuwa kwa neema ya mungu wakapate kujibiwa haja ya mioyo yao.
Kama nitakufa leo, nisiione jf nitawaombea wale wote wenye chuki binafsi na moderators, nitaiombea jf iendelee na kudumu milele hadi ile siku ya ukombozi itakapofika. Kama nitakufa leo, yaani nisiwepo tena nitamkumbuka mama mchungaji
mamndenyi kwa kuwa na misimamo thabiti ya kile anachokiamini lakini kama ni lazima leo hii uhai wangu unitoke basi sitaacha kuimba shairi la inside verossa kwa ajili ya mpwa wangu mpendwa
mentor
nitaendelea kuwaombea ikiwa ni lazima nife leo, yaani pumzi na mapigo yangu ya moyo yakisimama leo hivi nitamkumbusha mpwa wangu
mani aendelee kutoa nasaha na kuwakusanya group members hata pale ambapo ilibidi kutumia busara na gharama zake binafsi, nitamuombea kwa mungu amuongezee busara hasa katika kumshauri
mohamedi mtoi na harakati zake za ukombozi.
Kama roho yangu itauacha mwili wangu leo hii yaani sasa hivi, nitamuombea sana mzee mwenzangu
mtambuzi aendelee kuandika makala zake nzuri na tamu na kama sitabahatika kuisoma ile hadithi anayoiandaa inayohusu tanga basi nitamuomba aiweke kwa namna ambayo itawaonya na kuwakumbusha yale mema niliyotenda au kuwahi kutenda.
Lakini kama sitaiona kesho yaani kesho itakapofika isinikute basi namuomba mpwa wangu
baba v aongeze ukali kwenye jukwaa la mmu na sometimes aongeze nguvu kwenye chitchat ambako utoto, uhuni na umalaya vinakithiri, yaani jukwaa liwe ni kwa ajili ya kuelimishana na sio kufundishana na kusifiana ujinga,
yaani kama kesho hiyo damu yangu itasimama itakapokataaa kuendelea kuzunguka mwilini tena, hapo moyo wangu utakaposimama na mapigo ya mwili kutoweka nitaomba sana
aine paloma ladyfurahia tinna cute smile na
heaven on earth wabadilike na kuwa wadada wazuri wenye kuelemisha jukwaa, nitaomba kitu kimoja toka kwenu endapo itabidi nife leo, mtafuteni
little angel maana ameliasi jukwaa, seems whatsup imempoteza. Nawapenda dada zangu
nitaomba kabla ya kuupumzisha mwili wangu kwenye nyumba yangu ya milele, nitaomba hili tu na mara hii msikatae, pale mtakapokuwa mmenizunguka kuniaga huku mkibubujikwa na machozi ya furaha na simanzi huku
kokutona akiwa amebeba shada la maua dhidi ya elli nawaombeni na ninawakumbusha kunifanyia hili kwa ajili yangu na yenu, yasomeni yale maandiko yangu yote, ukiianza na lile la kwanza hadi lile la mwisho, mkajililie nafsi zenu maana wakati huo nitakua siwasikii tena, nitakuwa nimepumzika kwa amni, vita nitakuwa nimeimaliza.
Kawalilieni watoto wenu na watoto wa watoto wenu maana hapo katiba mpya itakapokuwa imefika, mbichi na mbivu zitajulikana na hakika hakutakua na kitu kitakacho achwa gizani kisiwekwe hadharani, hakuna dhambi itakoykuwa imefanyika sirni isionekane pale wapwa zangu
nape nnauye na
mwigulu nchemba watakapotubu watakapoyarudia mavumbi maana sisi sote tu mavumbi na mavumbini tutarejea. Kawakumbusheni hao wazililie nafsi zao maana hakika mbele za mola hakuna kinyonge kitakachoionja ahera wala pepo ya mwenyezi mungu
siku ile mkiwa mnaniaga, nikiwa ndani ya jeneza lile, najua unaniona najua machozi yanakutoka, ninakuona unavyoumia na kukiwaza kifo sijui jeneza langu litakuwa limiwekwa pale sitting room kwangu au pale nje chini ya ule mti huku jua kali likiwaka. Mmh najua unaniona usilie mpwa.
Lakini mimi kama nitakufa nisiione kesho nitafanya hayo, je wewe tutakukumbuka kwa yepi? Mungu wangu awabariki na kuwapigania katika mapito yenu, ktika shida ya moyo wako ukapokee haja ya moyo wako, ukajibiwe shida yako siku ya taabu yako kuu. Pale unapokuwa umeshindwa kabisa basi hapo msaada mkubwa na wa ajabu ukaonekane, unaetafuta kazi basi ukapate kazi, unaetafuta mke/mume basi mungu akujibu haja ya moyo wako huo, unataka kujenga maana umechoka kukaa nyumba za kupanga, basi mungu aliyehai akapate kukujibu, huna kodi ya nyumba au ada za watoto ni wakati wa mungu sasa kujibu maombi yako, akaponye ndoa yako, wazazi wako waponywe na familia yako sasa.
Tulianza mwaka na mungu na ni kwa neema yake tu tumefika hadi leo hii, barikiwa sana, tulipitishwa katika mengi, tulifika mahali ndoa zetu zikawa za moto na kazini nako kwa moto tukakosa pa kwenda, lakini mungu alikua kwetu, tuliumwa sana hata wengine wakakata tamaa juu ya uhai wetu, lakini mungu alikua muaminifu leo tena tuwazima, alitukinga na ajali wakati wenzetu wanakufa sisi tulitoka tukiwa salama, sio kwamba tumetenda mema sana ni kwa upendo wake allah hatustahili chochote sisi.
Je unani wewe badala ya kumshukuru mungu wako leo unakuwa na mwazo ya kwenda kulewa, ngono na mengine mabaya? Uwepo wetu jf uwe fundisho na maadili kwa maisha yetu na wala sio chanzo cha sisi kutenda dhambi. Na mungu wangu ninaemwamini atatuvusha na mwaka ujao ili tukawaone watoto na watoto wa watoto wetu.
kumbuka kutubu na kusamehe
heri ya mwaka mpya 2014
ashukuriwe mungu nimeuona mwaka 2014. Asanteni kwa maombi yenu. Nami sitakufa bali nitaishi ili niyasimulie matendo makuu ya mungu
kyan kyanakyomuhaya mungu ni mwema