Kama ni kweli, ni picha gani unapata hapa??

unaachosema ni kweli, wanawake wanayalea haya. Usikute toka wanaanza mahusiano mwanamke ndo analipa, labda kwa ujinga wa kudhania ndo anabembelezea ndoa wakifikiri kwenye ndoa watabadilika. Mwisho wa siku wanabeba mzigo wote wenyewe.

Hivi kwa nini umuhonge mwanaume? Kwa nini uwe na mwanaume asiyetambua wajibu wake?

mimi hata sishangai mambo ya kudai pesa wanaume wamekua "MARIOO". Nina rafiki yangu nae anaishi nchi ya jirani, mume yuko bongo na ni mfanyakazi pia. mke ana rotation ya 9 weeks kazini, 3 weeks likizo, utashangaa akija bongo, hizo 3 weeks, analipa madeni kibao yameachwa dukani na wapi sijui. halafu akiondoka after likizo, ni kwamba anaacha pesa za matumizi ya nyumbani kwa 9 weeks ambazo hatakua nchini, hii ni pamoja na luku, bill ya maji, mshahara wa maid, fuel ya gari ambalo mtumiaji ni mume, na upupu wote mnaojua wa ndani. ana mume huyu ambaye ni muajiriwa pia. nilisema mimi hadi shoga kaninunia kiaina, maana mie niliona ni u stupid na ushenzi fulani. huyo mwanaume kazi yake as a man ni kukuparamia tu au? ujinga mwingine tunaendekeza sisi wanawake, then baadaye kuacha inakua tatizo. wanaume wa siku hizi nao wakipata mteremko ni kwamba gear inawekwa free ateremke taratibu. hivyo huyu baba kudai pesa kwa mkewe, huenda mke alizoea hizo wakati wa malovi davi ya nguvu, sasa yakipungua unaanza kuona kero.
Ladies naomba tusiwazoeshe wanaume tabia ambazo hatutaweza kuendelea nazo. from day one, mwanaume ajue wajibu wake ndani ya nyumba, nikifanya mimi namsaidia tena haste haste. baba ndio kichwa cha nyumba na sio mama, yeye ndio akune kichwa tule, tuvae na tulale kwa raha.
 
kumbe kuna wanaume wanapenda dezo eeeh yaani unaishi na mume ndani then mabill yote unacleaer wewe hata ukiwa nje ya nchi mabill yanakufata? Hii kali
heri mtu uzae watoto wako ukae kwenu

Mbona wapo wengi tuu
Tena unamnunulia mpaka boxer
Yaani yeye kazi yake akiamka asubuhi ni kula na kulala na kucheza na laptop
Kuna dada namfaham yeye amefungua duka na ni mfanyakazi wa kuajiriwa
Ana mume ambaye kwa sasa hana kazi yuko tuu nyumbani
Unaambiwa hata kumsaidia yule dada kuuza pale dukani wakati mkewe yuko kazini ni issue
Yeye akiamka akute chai na kitafunwa, chakula cha mchana kipo house girl amepika, jioni atoke akakae baa kwa hela ya mkewe anywe bia na washkaji zake
Mchana kutwa yeye ni movies na laptop
 
Bigirita unakubaliana na DA kuwa kuna kitu cha ziada hapa eh?

Sio MJ1 hapo kuna kitu cha ziada wala si uongo.

Atakuwa amepata "Small house" inampa kiburi na utakuta jamaa alivyo bwe.....anakwenda kumsimulia matatizo yake na mkewe hicho kismall house haiwezekani mtu akawa na maneno makali namna hiyo
 
Hawa watoto wa siku hizi bwana...hata sijui wanaumwa nini???

Jando zimekufa na ha JKT nayo ndo hivyo tena...

Huko walau watu walikuwa wanafundishwa maana ya maisha!! Siku hizi vijana wana definitions za ajabu ajabu kuhusu maisha...Hutashangaa mtu anakueleza kuwa maisha ni kukaa na wife/husband na kuangalia movies au tamthilia za ajabu ajabu kila week end utadhani hakuna blue and black days...

Ngoja kwanza niishie hapa,

Babu DC!!
 
Mh!Nafikiri nahitaji kujua zaidi ili nichangie,something is missing here,plz don't ask me what!
 
Na hapo mimi ndo ninaposemea kuwa inaelekea toka mwanzo dada wa watu alikuwa analipa kila kitu ndani ya nyumba
Kutegemea jamaa abadilike katika kipindi kifupi ni issue
Na kama amemchoka sioni sababu ya kushikilia kulipana au kudaiana mambo ya bills

Hilo nalo nenooo!!!!!!!!!!!!!
 
sijacheka siku nyingi ila hii thread imenifurahisha jamani
yaani mama unasafiri mzee yupo home anakusanya bill za maji,umeme ,kingamuzi, watoto walitoka out wkend flani uje kuclear
kwanini jamani? kisa?
bado simu unapewa masaa ya kumpigia?
hapa ndo utaona kuna wanaume wa aina nyingi tena wabaya zaidi ya wa kwako
ngoja nimsamehe tu yule sharo wangu hana ubaya huu loh
 
sijacheka siku nyingi ila hii thread imenifurahisha jamani
yaani mama unasafiri mzee yupo home anakusanya bill za maji,umeme ,kingamuzi, watoto walitoka out wkend flani uje kuclear
kwanini jamani? kisa?
bado simu unapewa masaa ya kumpigia?
hapa ndo utaona kuna wanaume wa aina nyingi tena wabaya zaidi ya wa kwako
ngoja nimsamehe tu yule sharo wangu hana ubaya huu loh

Ha ha ha Smile bana si jana ulisema humtaki tena unatafuta Babu kama Asprin na DC???
 
Back
Top Bottom