Kama ni kweli, ni picha gani unapata hapa??

MwanajamiiOne

Platinum Member
Jul 24, 2008
10,470
6,562
Dears,
Wakati MJ1 mie naomboleza na ya kwangu, leo asubuhi nakutana na simu ya rafiki yangu ambaye alikuwa analia simuni kiasi cha kumwomba anisms tatizo ni nini. Akaamua kuniandikia mail ya kilichomsibu;

Yeye na Mr wake wanaishi mbalimbali kutokana na kutafuta maisha. Dada Suzzy (Si jina lake halisi) anaishi nje ya nchi lakini within EAC na mumewe anaishi nchini.

Juzi jumapili Da Suzzy anasema kapigiwa simu na shemeji lakini kwa bahati mbaya alikuwa amejipumzisha hakuisikia (ilikuwa ni jioni kwenye saa kumi na mbili jioni). Lakini alipoamka na kukuta missed call, akataka kucall back, only to realize kuwa hana credit kwenye simu na huko anakokaa ni mbali na maduka. So hakuweza kupiga but akajihimu alfajiri kwenda mjini kununua voucher akampigia shemeji hakupokea, akatuma sms ya kuomba radhi ya kushindwa kuwasiliana hakupata majibu. Lakini baada ya masaa mawili, akiwa kazini akakutana na e-mail ilotoka kwa Mr wake ikisema-
kuanzia muda sasa hatokuwa anapokea simu za mkewe hovyo, na muda alioamua ni fridays mchana na mwisho saa nne tu.


Da Suzzy a
nasema amechanganyikiwa, hajui la kufanya maana anajiona kama anatumika tu kwani kwa muda wamekuwa na matatizo na Mr wake (Haya sikuwa nayajua hadi leo). Anasema mumewe kwa sasa anamdai pesa ambazo amezitumia kwa kulipia matumizi ya nyumbani huku TZ kama maji na umeme, Mama ni among ya wale ambao wanatake care kila kitu ndani ya familia, mf. matengenezo/insurances za gari la familia, chakula cha familia n.k.

Silaumu lakini ninayo mawazo juu ya hili, ila kabla sijamweleza lolote ninaomba tusaidiane, maana ninaweza kuwa ninachokifikiria sicho.
 
Khaaa!!! Huyu mwanaume kiboko sasa anamuandika email mke wake yenye hayo maneno ina maana mke wake amekuwa secretary siku hizi, halafu kudai hela uliyolipa umeme urudishiwe hii nayo kali sasa kama wana watoto si ajabu akilipa ada ya mtoto atadai mke wake pia amrudishie hela pia, ngoja niendelee kutafakari maana kuna ndoa zingine zina viroja kama sio vioja
 
huyo sio mwanaume ni gumegume.

Matatizo mengine wanawake mnayalea. Kama majukumu yote ya nyumba unayafanya wewe, mwenzi wako anaspend ujue huna kitu.
Ni muhimu majukumu ya nyumba mkakubaliana.

Mwambie Suzy asitume pesa ya matumizi. Huyo ni mwanaume atafute.

Pia aendelee kumpigia akipata nafasi. Asipopokea wiki nzima basi achune mpaka mumewe atakapoona umuhimu.

Hv ni mapenzi gani ya kuishi kwa mashaka? Wanaume wa siku hizi mbona hovyo? Kutwa kutaka kulelewa, na wanawake kama wamerogwa utamuhongaje mwanaume?

All in all mpe pole huyo dada. Asitishe matumizi amfundishe mwanaume kujitegemea na kutimiza wajibu wake. Yaani hata umeme anaotumia mwenyewe pesa itoke kwa mkewe? Lets say mkewe anahongwa hiyo hela akirudi nyumbani ataipokea?

Loh kweli kuna ndoa nyingine ndoano!
 
Aisee...

Well kwanza kabisa huyo mume ana kiburi...pili anaonyesha kumchoka mkewe...tatu ana visa si kidogo.

Swala la yeye kutopokea simu za mkewe alipojaribu kumpigia na kumtumia email ya kumtaarifu kuhusu mpango wao mpya wa mawasiliano unaonyesha kabisa huyo mume amemchoka mkewe. Inawezekana mke akawa amempa sababu za kufanya hivyo (yani ni zaidi ya hilo la kutokupokea simu) ama inawezekana akawa anatafuta sababu ya kukorofisha ndoa yao. Pengine anatafuta kisingizio cha kutafuta nyumba ndogo...hamna namna ya kujua hilo kwa uhakika.

I mean haileti maana kupangiana muda wa kuwasiliana bila sababu maalumu (kazi ..safari..tofauti ya masaa n.k). Na hilo la kumdai pesa ya matumizi ya nyumbani ndio kabisa lenye uzito zaidi. Kwanini amdai?? Yeye hatumii hivyo vitu?? Yeye hana kazi/mshahara??

Dada amkalishe chini amuulize tatizo haswa ni nini, au kama anajua tayari atafute namna ya kulitatua.
 
Kuhusu kumdai hela mwambie amwambie huyo mwanaume aende polisi asilipe
na simu mwambie avumilie pia kuna machik wakutosha mbona?
 
Aisee...

Well kwanza kabisa huyo mume ana kiburi...pili anaonyesha kumchoka mkewe...tatu ana visa si kidogo.

Swala la yeye kutopokea simu za mkewe alipojaribu kumpigia na kumtumia email ya kumtaarifu kuhusu mpango wao mpya wa mawasiliano unaonyesha kabisa huyo mume amemchoka mkewe. Inawezekana mke akawa amempa sababu za kufanya hivyo (yani ni zaidi ya hilo la kutokupokea simu) ama inawezekana akawa anatafuta sababu ya kukorofisha ndoa yao. Pengine anatafuta kisingizio cha kutafuta nyumba ndogo...hamna namna ya kujua hilo kwa uhakika.

I mean haileti maana kupangiana muda wa kuwasiliana bila sababu maalumu (kazi ..safari..tofauti ya masaa n.k). Na hilo la kumdai pesa ya matumizi ya nyumbani ndio kabisa lenye uzito zaidi. Kwanini amdai?? Yeye hatumii hivyo vitu?? Yeye hana kazi/mshahara??

Dada amkalishe chini amuulize tatizo haswa ni nini, au kama anajua tayari atafute namna ya kulitatua.
Nafikiri mume anatafuta sababu ya kukorofisha ndoa, halafu pia anatumia advantage ya mwenzake kuwa mbali kama rungu lake lakini why all the fuss sidhani kama imeishafikia hatua ya wao kushindwa kukaa chini na kuona tatizo liko wapi
 
Duh mpe pole kwanza rafiki yako kwa kupata "mke" ambae hana shukrani kama anayosema ni kweli kuhusu kudaiwa pesa zilizotumika kwenye familia
.

Nimemwita huyo jamaa "mke" kwa jinsi anavyojiwakilisha kwenye hii ndoa.

Hapa tumepata upande mmoja wa shillingi kwahio majibu yatakuja kiupande mmoja na mara nyingi sidhani kama yanaweza kuleta solution yoyote kati ya hawa wawili zaidi ya kumshauli rafiki yako afanye maamuzi mazito ya kutengana nae.

Je kuna watoto kwenye familia? Sijasikia wakitajwa kwahio nachukulia hawapo na hivyo basi rafiki yako ndio anamuhudumia jamaa na lazima huyu jamaa anahudumia sehemu nyingine.

Mwambie rafiki yako AW anasema mapenzi sio kama kandanda, kwamba lazima kuwe na mshindi na mshindwa; mapenzi ni mchezo ambao matokeo yake yanatakiwa yawe draw na hakuna overtime. Haya matokeo yanapatikana kwa pande zote mbili kushirikiana kwa pamoja na kamwe kama mmoja hataki kutoa ushirikiano basi hakuna future yoyote zaidi ya mmoja kuhisi anatumika na kuleta mikwaruzano.

Ushirikiano unaweza kupatikana pale kunapo kuwa na mawasiliano ndani ya nyumba, kama mtu anaona kuna jambo lina msumbua ni vizuri kumwambia mwenzake hata kama ata chukia lakini mwisho wa siku itamuingia akilini na kama ana kosa ata sahihisha. Wakati huo huo tegemea na yeye kutoa mambo yanayomsumbua kwani utakuwa umejenga uhuru wa kuwasiliana ndani ya nyumba na wewe utapata nafasi ya kusahihisha yale yanamsumbua mwenzako.

Hakuna mtu aliye perfect kwenye mapenzi na kwenda kulalamika nje haisaidii kupata solution ndani ya nyumba kwani watu unao wapelkea malalamiko wanasikia upande mmoja tu.

Mpe pole rafiki yako na mwambie mda umefika wa maamuzi mazito na inabidi aje nyumbani kuangalia kwa undani kinachoendelea na kujipanga kufanya maamuzi mazito.
 
Duh ndoa nyingine ni balaa
So mume ametumia umeme na anamdai mke wake amlipe pesa alizotumia kulipia umeme
Naamini kuna tatizo kubwa hapo kakti ya wawili hao na sio hili la kuandikiwa email
 
Khaaa!!! Huyu mwanaume kiboko sasa anamuandika email mke wake yenye hayo maneno kwenye blue ina maana mke wake amekuwa secretary siku hizi, halafu kudai hela uliyolipa umeme urudishiwe hii nayo kali sasa kama wana watoto si ajabu akilipa ada ya mtoto atadai mke wake pia amrudishie hela pia, ngoja niendelee kutafakari maana kuna ndoa zingine zina viroja kama sio vioja
The Finest, nimeogopa kutoa mtazamo wangu mimi kwani nilijua wengi wanaweza wasiamini but kumbe kuna wanaume wa aina hii. Mimi picha ninayoipata hapa, kama ni kweli haya anayofanyiwa Da Suzzy, basi huyu ameendekezwa sana. Anajua fika kuwa Suzzy hapindui kwake.
 
duh ndoa nyingine ni balaa
so mume ametumia umeme na anamdai mke wake amlipe pesa alizotumia kulipia umeme
naamini kuna tatizo kubwa hapo kakti ya wawili hao na sio hili la kuandikiwa email
umeona kaka
mwishowe atakuta na risiti ooh nilienda saluni na watoto
nilimlipa h/girl
nilinunua soksi na boxer lipa hana AKILi huyo
 
Naona mnakuwa wakali tu hapa............mumemsikiliza huyo mwanaume??

kama huyo mwanaume ndo alivyo, basi inakuwaje alimpenda alivyo na sasa hivi anahisi anakuwa kero?

Come clean wewe Suzy wa kuchonga!!
 
umeona kaka
mwishowe atakuta na risiti ooh nilienda saluni na watoto
nilimlipa h/girl
nilinunua soksi na boxer lipa hana alili huyo
Mnamdanganya mwenzenu ee!!!
Mnajua walipotoana?? waacheni bana...........mapenzi yao kama ya mbwa!

''Suzy''......toka huko, tafuta kazi bongo uje kukaa na mumeo...sweet potato wako bana!!
 
Back
Top Bottom