Kama ndiyo, Kibatala naye kaenda kufungua kesi dhidi ya nani na kulalamikia nn iwapo barua siyo halali?
Ulijipa nafasi ya kumsikiliza Kibatala?
Kama SIVYO jipe nafasi ya kumsikiliza kidogo Ndio uje ucomment! Nchi imekua banana republic, Yale Yale aliyoyasema Josephat Gwajima Ndio hayo hayo yametokea.
Kwakua Jeshi la Polisi lilijinasibu Kwa mbwembwe na pia mkuu wa Wilaya alijinasibu Kwa mbwembwe kusimamia maagizo yaliyotolewa na serikali, Kwa maana ya kulifungia kanisa, walijiona wako sahihi, Kwa kuwa hakuna clear coordination sababu ya kufanya mambo bila kuzingatia utawala Bora.
Kibatala hajashitaki sehemu yoyote au mtoto yoyote. Muliro alikaza fuvu na kusema kwamba ikiwa kama kanisa inahisi haijaridhika na maamuzi ya serikali kufunga kanisa na wao askari kulizingira kanisa basi wakate rufaa Kwa aliyeweka zuio ambaye ni waziri Kwa mujibu wa barua iliyokua in circulate kwenye mitandao.
Kibatala kama wakili ndiye aliyepewa jukumu Hilo, na Kwa kuzingatia kwamba polisi wanashuoaza shingo na Msando naye anashupaza kipara kwamba kanisa lilikua served with a letter of suspension of services, Kibatala aliomba hiyo barua Ili aitumie kukata rufaa kuonesha kutokurudhika na maamuzi yaliyotolewa na Msajili.
Kwakua barua ya kwanza haikua na sahihi, ya pili haikua na sahihi Ila haikutaja majina ya kanisa Kwa ukamilifu na usahihi, na aibu inayoendelea kulikumba taifa kutokana na wajinga kushika madaraka, waziri wa mambo ya ndani ya nchi haraka amekana barua hiyo kwamba haijatokea wizarani kwake hivyo Kibatala kuonekana anakata rufaa ya hukumu au agizo ambalo halipo.
Kama nchi inaweza kuwa na kikundi Cha wajinga na wapumbavu ambao wanaweza kuandika barua yenye official seal of the state tena yenye Amri, na polisi na mkuu wa Wilaya wakaifanyia utekelezaji bila kuhoji au kujiridhisha it's authenticity, ujue Hilo taifa mambo yake katika uongozi yanaenda arijojo.
Watu wajinga walioshika madaraka hufanya mambo ya kijinga kuonesha kwamba Wana nguvu na madaraka.