Kama ndivyo, kuna shida. Kubwa!

Kama ndivyo, kuna shida. Kubwa!

Vyovyote vile:
Kama hiyo barua ilikuwa ni ya kughushi, ni kwanini mamlaka husika (Msajili) haikukanusha habari hizo?
Unyumbu wa kisiasa ni mfumo unao wezesha wanaopewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi ambapo hufanya hivyo kwa kujipendekeza ama kwa uoga wa kuigiza, (unafiki), a.k.a kujizima data kwassa uchawa tuseme kuahirisha kufikiri kizalendo
 
Ni mimi sijaelewa au watu wameamua kutazama upande mmoja?
Baada ya waziri kusema sio halali, ametoa maelekezo gani? Ameeleza nini kifanyike? Ameeleza hatua zinazochukuliwa na wizara juu ya hilo?
Kama hakuna alichosema, then hiyo ni punch usoni kwa Kibatala ili kusiwe na rufaa, maelekezo ya barua yaendelee kutekelezwa.
Ndio maana kama barua si hali hivyo hakuna rufaa yakushuhulikia.

Naona watu mmejikita kivingine kabisaa
Rufaa ikifanyika kwa haki itarudishia waumini na kiongozi wao haki yao. Ndio maana imepigwa juu kwa juu.
Kuna mambo kadhaa yanakupiga chenga. Ukiyaelewa, utajua nini kipo nyuma ya upuuzi huu wa serikali;

1. Barua ile inayofanyiwa utekelezaji na DC Albert Msando, Afande Muliro na Polisi wake imekuwa addressed kwenda kanisa linaitwa The Glory Of Christ Church - GCC (hili sio kanisa linaloongozwa na Askofu Gwajima)...

2. Mpaka sasa kanisa linalodaiwa kufutiwa usajili wake lenye jina la The Glory Of Christ Tanzania Church - GCTC maarufu kama "Jumba la Ufufuo na Uzima" (ambalo ndilo kanisa halali linaloongozwa na Askofu Josephat Gwajima) halina barua yenye jina lao lakini wakati huohuo linaathirika kwa adhabu au matokeo yatokayo na barua ile ambayo siyo yao...

3. DC Albert Msando na wengine wanadai kuwa, barua halisi yenye jina la kanisa la Askofu Josephat Gwajima (GCTC) na kusainiwa na Registrar of Civil Society - Wizara ya mambo ya ndani ndugu Emmanuel Kihampa kwa ukamilifu wake wanayo wao kina DC Msando na Muliro na sababu wanayotoa (wasikilize kwa makini wanavyoongea) ni kwa kuwa uongozi wa kanisa unadaiwa ulikataa kuipokea barua hiyo😕😕

4. At the same time, uongozi wa kanisa la GCTC unakanusha kuwa, hawajawahi kuletewa barua yao kuwataarifu kuwa hawana uhalali tena kisheria kufurahia haki yao ya kikatiba ya kuabudu kwa kuwa wamefutiwa usajili wa taasisi yao achilia mbali kukataa kuipokea hiyo barua. Lakini kumbuka na liweke hili akilini kuwa, pamoja na yote hayo kanisa linaendelea kuathirika na adhabu wasiyohusika nayo..!!

Maswali yaliyo kwenye vichwa vya wengi ni haya:
Kama ni hivyo, kanisa lilienda mahakamani na kufungua kesi kwa base ipi?

• Vivyohivyo lilikata rufaa kwa Waziri kwa msingi upi au kwa kutumia taarifa/barua ipi?

• Lilitumia taarifa ya barua gani maana wao hawajafutiwa usajili..
?

MAJIBU YA MASWALI HAYA NI RAHISI SANA:

1. Wewe unafikiri wangefanyeje? Maana Polisi wame trespass kwenye eneo lao, wamezuia shughuli zote zisiendelee kwa madai na taarifa potofu zilizosambaa mitandaoni na kwenye vyombo vingine vya habari. Obvious huwezi kuanza kupigana nao kimwili na mtu kichaa asiyejua anafanya nini. Ni lazima utaratibu wa kudai haki yako kisheria ufuatwe Ili kuepusha athari zingine..

2. Kwa kuwa Kuna barua inayosambaa mitandaoni na ndiyo inayosemekana kufanyiwa kazi na Polisi na DC Albert Msando, unaichukua hiyo na kuitumia kama kielelezo ili kama sio halali, basi waseme wao..

3. Ndiyo maana Wakili wa kanisa, akakata rufaa kwa Waziri. Jibu la Waziri likawa very clear kuwa, haijui barua na haijatoka wizarani kwake, Kwa hiyo hawezi kuamua rufaa ambayo kesi yake haipo ofisini kwake. Bahari mzuri ni kuwa mahakama nayo imesema hivyo hivyo, kuwa, GCTC ni taasisi halali as it is for now na ambapo maana yake waendelee na shughuli zao kama kawaida...

4. Wakili Kibatala hakuishia hapo, aliwataka wasimamizi wa sheria Polisi waliohusika na vurugu hizo kanisani pamoja Wizara kupitia ofisi ya Msajili wa taasisi za kiraia waitoe barua hiyo inayowapa uhalali wa kufanya hayo wanayoyafanya kisheria..

KWA HIYO:

√ Msingi wa mchakato wote wa kanisa ni barua iliyosambaa mitandaoni na kwenye mainstream medias zote isiyowahusu lakini ikiwaletea athari hasi wao. Kama barua imekanwa na mamlaka za serikali zinazodaiwa kuitoa, basi maana yake kila kilichofanyika ni batili na wote waliofanya hayo kwa kukosa umakini, wawajibike kulipia gharama ya hasara ya mali na muda walioisababishia taasisi

√ Na hili nadhani, Afande Jumanne Muliro RPC wa Kanda maalumu DSM anaweza kuwa kwenye position nzuri zaidi kulitolea ufafanuzi. Kwa kujibu swali moja tu. Polisi wake wanafanya nini kwenye kanisa la GCTC wakati barua inawaelekeza kwenda kwenye kanisa la GCC bila kujali ni halali au siyo halali.?
 
Leo, nimemuona na kumsikia Wakili Msomi mwenzangu Peter Kibatala (kupitia video clip) akizungumzia uhalali wa barua iliyotumika kufungia makanisa yanayoongozwa na Askofu Gwajima.

Kwa mujibu wa Kibatala na muktadha wa mazungumzo yake ndani ya Mahakama Kuu kule Dodoma, Kanisa lililofungiwa lilijaribu kukata rufaa juu ya uamuzi huo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani kwa mujibu wa sheria.

Kibatala akaeleza kuwa Waziri husika ametamka kuwa barua husika, pamoja na mambo mengine, SI HALALI. Waziri amesema kuwa hakuna rufaa ya kuishughulikia kwakuwa barua ni batili na uamuzi uliobebwa humo ni batili.

Barua inayosemwa ni batili/si halali ndiyo iliyotumiwa na mamlaka za kiserikali wakiwemo polisi kutekeleza kinachobebwa na barua hiyo. Makanisa Dar es Salaam na Mbeya (penginepo sifahamu) yamefungwa chini ya ulinzi mkali wa jeshi la polisi.

Tumeona na kusikia kuhusu hili. Sasa, imewezekanaje barua batili/isiyo halali kusababisha kufanyika kwa yote haya? Nani huyu aliyeghushi barua hii na kusababisha yote haya? Amefanya haya kwa faida ya nani?

Kama hivyo ndivyo, tupo kwenye tatizo kubwa. Sana! Serikali itusaidie kubaini jambo hili na kukomesha kujirudia kwa jambo kama hili.
Serikali inaongozwa na walevi
 
Hao akina Gwajima nao si hata wa kuwapa support kivile, maana wakati sheria mpya ya usalama wa taifa inapitishwa alikuwa ndani ya bunge na hakupinga. Ama mkuu umesahau kuna sheria ya usalama wa taifa ambapo unaweza kushughulikia bila watu hao kuwajibishwa popote?
Wakati mwingine akili ya kuwa nilifanya kosa huja baada ya majuto fulani
 
Tulipokuwa tunasema kuhusu wanaoteka watu na hadi watu wana details zao watu waliona ni maigizo.

Sasa kama mkuu wa wilaya wanavyoitwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa wilaya anaulizwa una details za utekaji wa mwananchi wako anajibu" No Comment" sasa nani aulizwe na nani ajue.

Na akiitwa mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama hataki kabisa kuitwa hivyo .
View attachment 3368353
Haa😀😀haa

Huyu ndiye DC? Hataki kabisa kuulizwa baadhi ya maswali
 
Tatizo ni vuombo vya serikali kufanuia kazi barua haramu.
Hiyo ni uwongo. Polisi na mkuu wa wilaya hawafanyi kazi kwa barua za mitandaoni tu (bila maagizo maalum). Serikali imeamua kufanya kazi kihuni kwa mtindo wa kihuni.
 
wamebadilisha gia angani barua isingekuwa yao siku ileile wangetoa taarifa kwa umma kuwa ni feki lakini walikaa kimya siku zaidi ya week na tena police wanatejeleza amri pamoja na yule dc eti leo sio yao ni yao ila wamepima upepo wameona italeta shida
Huko sahihi kabsa, au ilitoka bila kuwa na makubaliano.
 
Hiyo ni uwongo. Polisi na mkuu wa wilaya hawafanyi kazi kwa baraua za mitandaoni tu (bila maagizo Mwalimu). Serikali imeamua kufanya kazi kihuni kwa mtindo wa kihuni.
True. Ni mchezo wanaufanya in the Name of ....!!
 
Kusema barua ni FAKE huo ni Uongo na wanatafuta Kichaka cha Kujificha, Mpaka IGP ame deploy forces pale kwenda kuhalt operation za kanisa si inamaana alipata ile barua na akatekeleza? Au tafsiri yake ni kuwa hata copy ya IGP nayo ni fake aliyopewa? Ina maana kuna watu wanawez kuwasiliana na Jeshi la Polisi tena Ofisi ya IGP kwa Mawasiliano fake? yani Polisi wameshindwa kufanya authentication ya barua waliyopewa kama ni Legit

Mbona inatisha sasa
Wajinga wanaposhika madaraka, na kuwatumia wajinga zaidi kusimamia Sheria utayaona ya wale waliowashambulia raia kisutu mahakamani na kwenda kuwatupa mabwepande, mahakama ikarule ni Haki yao kwenda mahakamani, Bado polisi wakarudi na kuonekana kuwapiga watu kama wanapiga punda!
Usisahau DC ni mjumbe wa kamata ya siasa ya Wilaya kama alivyo RC kwemye Ile ya Mkoa, na ni hivi msimamo wa Chama Cha mapinduzi ni kuhakikisha aliyeko agaisnta abduction anakua halali ya Watawala kisheria na kiharamu.
 
Iwapo ni sahihi alyoyasema Msomi Kibatala waliosimamia utekelezaji wa barua hiyo wanatakuwa wajiuzulu kutoka kwenye nyadhifa zao. Vinginevyo mamlaka za uteuzi ziwafukuze kazi.
 
Very SIMPLE wanaoteka na kuua umewaona popote!?, Gwajima alisema wazi hawana weledi ila wanashirikiana na polisi. Hapahapa jamii forums, barua ya kwanza kabisa kuletwa humu ilikuwa hata sahihi hakuna, tulipohoji ghafla Moderators wakaufuta Uzi ukapotea, baada ya kama nusu saa hivi Uzi ukaachiwa tena ukiwa na barua yenye sahihi. Nilisema humu kuwa Ile barua imetoka kwa wahuni wanaoshirikiana na polisi wenye vyeo, nao wakafata maelekezo bila kujiridhisha. Mwisho wa siku serikali imeikana barua. Hakuna mamlaka yoyote ya kiserikali iliyowahi kujihusisha na Ile barua directly zaidi ya polisi na mkuu wa wilaya walioingizwa mkenge na wahuni. Ile sahihi ni fake.
Kuna habari za ndani kabisa Ila kila nikitaka kuziweka humu moyo unasita kabisa.

Ngoja nitulie TU.
 
Iwapo ni sahihi alyoyasema Msomi Kibatala waliosimamia utekelezaji wa barua hiyo wanatakuwa wajiuzulu kutoka kwenye nyadhifa zao. Vinginevyo mamlaka za uteuzi ziwafukuze kazi.
IMG-20250614-WA0045.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom