Kama mtu humpendi mkatae kistaarabu tu

Kama mtu humpendi mkatae kistaarabu tu

Khantwe

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2012
Posts
61,180
Reaction score
124,849
Habari ya wakati huu Great Thinkers.

Leo naomba niongee kidogo na wadogo zangu wa kike, (kama mtu mzima mwenzangu unafanya haya tafadhali acha mara moja).

Hivi karibuni niliangalia muvi moja hivi ya kiswahili (bongo muvi)....nilijikuta natumia wiki nzima kufikiria kile nilichokiona.

Kwa kifupi ni kwamba alikuwepo huyo mrembo anakwenda kwa jina la Jack, wakatokea wakaka wa mtaani kwao wakawa wanamtongoza, alichokuwa anawajibu sasa, 'huna hadhi ya kuwa na mrembo kama mimi', mkome kunifuatilia nyie vinuka-mkojo, wachafu kuoga' na mengine mengi ya dharau nimeyasahau.

Kifupi maneno hayo yaliwakera sana wale vijana lakini hawakuwa na la kufanya (watafanyaje sasa, shule hawana, pesa inawakimbia).

Ila mmoja kati yao alijua cha kufanya, akaenda kwa mjomba wake kuomba mtaji, akapewa na akazalisha vya kutosha akawa young bilionea.

Alichofanya alitumia kila mbinu (na kusema kweli alitumia nguvu kubwa) hadi akampata yule dada, akatoa posa na tarehe ya ndoa ikapangwa.

Siku chache kabla ya ndoa akamshawishi dada wakazini (bahati mbaya au nzuri mdada wa watu alikuwa bikra) na mimba ikaingia.

Ilipofika siku ya harusi yule kijana hakutokea kumbe amepanda zake ndege, ameenda nje ya nchi kupumzika.

Lengo lake la kumkomoa mdada likawa limetimia.

Sitaelezea mbele ilikuwaje maana siko nilikotaka kuzungumzia.

Kwanza naomba kujifunza kwenu wadada, ni kwa nini huwa mnatumia maneno ya shombo au matusi kukataa watu?

Mbona kuna majibu ya kistaarabu yanayoeleweka? Mdada anamtukana mkaka wa watu hadi anajiona useless yeye,wazazi wake na ukoo wake wote kisa nini?

Msifanye hivyo bwana, kuna watu wana roho za visasi shetani anaomba poo. Sina hakika kama kwenye maisha yetu halisi mtu anaweza kulipa kisasi kwa kiwango hiki ila mimi ninachojua ni kwamba VISASI VIPO!

Mtu anaweza akakomaa na wewe miaka kadhaa kwa lengo la kulipa kisasi tu, akudhalilishe kama wewe ulivyomdhalilisha.
Hata kama mtu yupo below your standards Mjibu kistaarabu tu....mwambie nina mchumba (hata kama huna), ukamweleza kuwa hujavutiwa nae kwa namna ya kiungwana au sababu zingine unazoona wewe zinafaa.

Haya maneno ya dharau yanaweza kukukost ukajuta maisha yote.

Lakini na ninyi kaka zangu niwaambie kitu, mapenzi ya mwanamke yanazaliwa na kukua kulingana na mazingira.

Mwanamke anaweza asikupende wakati unamtokea kwa mara ya kwanza lakini ukafanikiwa kumshawishi akupende.

Mimi nimeona watu huwa wanatukana mitusi ya nguoni (na wanakuwa wanamaanisha kweli) lakini mwisho wa siku wanakuja kuolewa na wanaume haohao tena wakiwa wanawapenda kwa dhati kabisa.

Kama mtu alikutukana baadae akakupenda samehe yaliyopita msonge mbele.

Thanx (Nimekopi hii swaga)
 
Haipendezi ila na wakaka nao wawe wepesi kusoma majira. Sio mtu anakomaaalia mpaka iwe kero... Ukishaona mazingira hayakubali we jisepeshe tu sio mpaka yakufike...
 
Haipendezi ila na wakaka nao wawe wepesi kusoma majira. Sio mtu anakomaaalia mpaka iwe kero... Ukishaona mazingira hayakubali we jisepeshe tu sio mpaka yakufike...

Kuwa mwanaume tabu kweli ....... Unakuta umeshapigwa vibuti kibaooo ukifika kwa huyo mmoja unasema hapa lazima kieleweke ndio maana wengine tunakomaa hata kama ulimwanza form 1 hadi chuo ukimkuta unamkumbushia mistari tu
 
Ehee tusimulie ulimfanya nini dada wa watu...teh

My case sounds a lot familiar issue is ilikua high school hapa hapa dar....i was chasing ths chick for like 3 years...that was when love and crashes wer at its peak...

Dem alintosa, kashan dhalilisha sanaa, dharau, majibu ya ovyo sumtyms mbele za watu, alikua na crew lake rafiki zake walikua ma pashkuna balaa... I loved tha chick so badly...nimelia sanaa mwenyewe maghetoni....one day i said to my self " f*ck ths shit ".

Tumemaliza high school tukingoja taratibu za kuingia ma chuo....i remember nlifight sanaa nimvue chup.i yule mtoto...siku kama zali akakubali kutoa game baada ya ku insist sanaa.....ile tumebaki kama tulivyo zaliwa....nikamwambia " yan kuringa kote huko ni huu uozo unataka kunipa ?? K*ma yenyewe inanuka kaa choo ( nikitema mate kwa kinyaa pembeni ) ". Sikumla wala nn...nikavaa nguo zangu alaf huyo nikajikataa.

Bwana weee.....yule mwanamke ikawa ni kilio kila siku.....kila akiniona hana amani na raha kabisa...she was extremely cute nd fine. Yule mtoto ikafika kipindi nikawa nakula kama nimemtolea mahari....as we speak mpaka leo wern't close kama zamani but nikiomba mchezo milele yote hachomoi.
 
Nimejikuta nacheka mwenyewe.huyu niliye nae pembeni hapa wakati namfuatilia aliwahi kuniambia hivi unanionaje. Anyway ndio mikasa ya wanaume hiyo kwenye mambo ya mapenzi. Thanks mtoa mada
 
Mi nikipewa jibu naachana naye sisumbui,tatizo ukitoboa huyo huyo anaanza kujileta,lazima ule umwache akae na broken heart
 
My case sounds a lot familiar issue is ilikua high school hapa hapa dar....i was chasing ths chick for like 3 years...that was when love and crashes wer at its peak...

Dem alintosa, kashan dhalilisha sanaa, dharau, majibu ya ovyo sumtyms mbele za watu, alikua na crew lake rafiki zake walikua ma pashkuna balaa... I loved tha chick so badly...nimelia sanaa mwenyewe maghetoni....one day i said to my self " f*ck ths shit ".

Tumemaliza high school tukingoja taratibu za kuingia ma chuo....i remember nlifight sanaa nimvue chup.i yule mtoto...siku kama zali akakubali kutoa game baada ya ku insist sanaa.....ile tumebaki kama tulivyo zaliwa....nikamwambia " yan kuringa kote huko ni huu uozo unataka kunipa ?? K*ma yenyewe inanuka kaa choo ( nikitema mate kwa kinyaa pembeni ) ". Sikumla wala nn...nikavaa nguo zangu alaf huyo nikajikataa.

Bwana weee.....yule mwanamke ikawa ni kilio kila siku.....kila akiniona hana amani na raha kabisa...she was extremely cute nd fine. Yule mtoto ikafika kipindi nikawa nakula kama nimemtolea mahari....as we speak mpaka leo wern't close kama zamani but nikiomba mchezo milele yote hachomoi.

Aiseeee.....
 
Mi nikipewa jibu naachana naye sisumbui,tatizo ukitoboa huyo huyo anaanza kujileta,lazima ule umwache akae na broken heart

Wewe unakuwa umefaidika nini?
 
Kuna wanaume wanajua kugandaa hao ndo wengi huambulia matusi
 
Mmh ngoja siku wakutane na vichaa wenzao. Unamtukana mtu anakutemea mineno ya shombo hadi utalamba ndimu. Ustaarabu kitu cha muhimu sana, na kama mtu humtaki unaweza kumuavoid bila hata kumdhalilisha
 
Back
Top Bottom