Kama mbinguni wanaenda wenye ndoa,basi sitaenda

Kama mbinguni wanaenda wenye ndoa,basi sitaenda

giningi

Member
Joined
Jun 12, 2011
Posts
52
Reaction score
27
Mwenzenu nimeamua kuondoka kwangu,mume huyu wangu alinioa kihalali kanisani,leo nimenyoosha mikono najiandaa kuanza maisha peke yangu na wanangu,nimeshindwa,siko tayari kufa kwa ukimwi kwa kuwa sistahili,alinioa bikira na simjui mwanaume yeyote zaidi yake katika dunia hii.
Uzinzi,umalaya,matusi anayonipa,dharau,kejeli na kutokunijali vinanifanya niondoke kwangu,kuanzia leo nimedhamiria kuondoka rasmi,hata nikisikia umeoa chelenje sitakwenda kulalamika popote,kwa sababu najua utakuwa umemuoa mwanamke unayempenda,nimelia sana sasa nimeamua kufuta machozi na kusonga mbele,najua MUNGU HATANIACHA!:wave:
 
Vizuri, endelea hivyo hivyo na msimamo wako. Ikiwa hutojali tafuta mwingine uishi nae, maisha ya kuwa single yanahitaji moyo mgumu kama bati la South Africa.
 
natumaini uamuzi umeufanya ukiwa na akili timamu bila kushurutiwa, kulubuniwa na bila kulazimishawa. nakutakia maisha mema.
 
CHELENJE na wewe umezidi bana wenzako wanajenga na kucheza kwa step wewe unabomoa.
 
Pole sana. Wanaume ndivyo walivyo, hawatosheki hata uwape nini?

2nd kwa nn unajiita giningi? hili jina nijuavyo lina maana mbaya sana
 
Alikuwa kalewa ndio maana. Msamehe bure. Hilo la kuchana nje ahhh. Ajabu hata wewe utachana nje baada ya kuondoka kwake. Na huyo wa pili atakuwa na chain refu kama reli ya kati. Then atakuja na mwingine na mwingine maana huna kizuizi. Nao watakuita malaya maana ni ukweli. jifunze kuvumilia na kuongea na mwenzio.
 
mtoa mada hiyo avatar yako unaiish kweli ama unaihubiria tu??

manake kama unaniish huo msalaba wa YESU KRISTO, ni dawa ndio mana umewekwa kwenye bomba la sindano ili kukuponya na kuponya ndoa yako.
 
Angalia sana uamuzi wako,
Maisha siyo mepesi kama unavyowaza rafiki,
Kama hauwezi kuwa na msimamo dhabiti na maisha yako na wanao utajikuta unaolewa kila baada ya mwaka mmoja tena na wanaume tofauti.

Napenda kukuambia tena,
angalia kwanza uamuzi wako.
 
Pole, pengine uliolewa na ubavu ambao haukustahili kuwa wako...
 
Kama unamwamini Mungu jua kwamba everything happens for a reason! Mungu ni mwema kila wakati hayo ni mapito tu! na umeamua vizuri najua umevumilia sana na umeomba ushauri ! may be tht was a wrong choice! na Mungu anataka kukuepusha na balaa hilo! God b wth u in whtver your do'
 
Mwenzenu nimeamua kuondoka kwangu,mume huyu wangu alinioa kihalali kanisani,leo nimenyoosha mikono najiandaa kuanza maisha peke yangu na wanangu,nimeshindwa,siko tayari kufa kwa ukimwi kwa kuwa sistahili,alinioa bikira na simjui mwanaume yeyote zaidi yake katika dunia hii.
Uzinzi,umalaya,matusi anayonipa,dharau,kejeli na kutokunijali vinanifanya niondoke kwangu,kuanzia leo nimedhamiria kuondoka rasmi,hata nikisikia umeoa chelenje sitakwenda kulalamika popote,kwa sababu najua utakuwa umemuoa mwanamke unayempenda,nimelia sana sasa nimeamua kufuta machozi na kusonga mbele,najua MUNGU HATANIACHA!:wave:

Hatari kwa kingereza ni DANGER na Hasira kwa kingereza ni ANGER, maana yake ni kwamba maamuzi ya hasira hupelekea hatari. Nakushauri kama avatar yako inavyosema TRY JESUS, hebu izingatie hiyo maana kwake YOTE YAWEZEKANA.
 
kila mwanamke aliyekwenye ndoa huwa anadai alikutwa na bikra.....mhhh
 
Pole kwa hilo..Nimeumia san kam Story inanihusu mim...Mungu hawez kukuacha kam kwel ulipata mateso..Be strong lea wanao.
 
Just do this, before you pack your bags and leave for good from your marriage with your kids, he is still your husband, ask him for a one month leave that should tally with the work leave only if you are working. Hapo waweza kwenda hoteli yoyote kutokana na uwezo wako na kama inawezekana muombe na yeye akufinance huko enjoy with your kids na usiwe na mawasiliano na mtu yeyote yule yaani uwe wewe tuu na watoto. Kama ni mama wa nyumbani au mjasiriamali au umejiri na biashara zako unaweza kaa zaidi ya miezi 2, ukiwa huko kwenye hiyo likizo waza mara mbili je unaweza kaa bila mumeo au utaanza kummiss na kuona bora awepo hata kama ni mzigo.
Usifikiri watu wengine wanaenda kwenye harusi pamoja wamevaa wamependeza ujue wanalea watoto na mapenzi yalishaisha siku nyingi. Wakiingia chumbani kwao wanalala mzungu wa nne au kila mtu analala kitanda chake na wengine vyumba tofauti kabisa ila hawaachani.
Think twice before you leave your marriage. Namuomba BAK aje akuwekee kibao cha celine dion cha think twice may be kitakubadili mawazo yako.
All the best mamy.
 
Last edited by a moderator:
Once a player always a player
maisha yenyewe mafupi haya kuishi na mwanaume full stress ya nini!!!!!

ita hard lakin sometimes inabidi tu
chelenje hope ujumbe wa giningi umekufikia
 
Last edited by a moderator:
kama kweli unachosema ni kweli i can be of help hata hapo ulipofikia! nina ushuhuda kama wako na jinsi tatizo lilivyo tatuliwa.
 
Back
Top Bottom