Kakobe apinga waraka wa wakatoliki

Kakobe apinga waraka wa wakatoliki

HM Hafif

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2009
Posts
1,359
Reaction score
20
Na Waandishi Wetu

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe amemhisi Rais Jakaya Kikwete, kuvunja ukimya na kuzima mijadala kuhusu nyaraka za kidini, inaoendelea nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Askofu Kakobe alisema nyaraka hizo zinaelekea kuwagawa watu na hatua zisipochukuliwa, zinaweza kusababisha vita ambavyo havitakwisha.

“Rais wetu ni mpole sana, mcheshi na ni mtu wa watu, hilo si tatizo kubwa kwake, lakini ukiwa na rais mpole sana ni tatizo, hata ukiwa mkali sana ni tatizo pia, namhisi hili aliingilie kati,” alisema Kakobe.

Kakobe alisema baadhi ya viongozi wa kisiasa, wamekuwa wakiogopa kukemea vitendo vinavyofanywa na viongozi wa dini kwa sababu tu wanawaogopa.

“Napenda kusema kuwa, viongozi wa kisiasa kunyamazia maovu yanayofanywa na viongozi wa dini kwa sababu tu kuwaogopa, kunaweza kuwaingiza watu wote kwenye uovu,” alionya Kakobe.

Mbali na hayo Kakobe amepinga vikali tamko la kiongozi mmoja wa kanisa aliyejibu hoja ya kiongozi mmoja wa kisiasa aliposema wanasiasa hawawezi kuwafundisha kazi maaskofu.

“Nichukue nafasi hii kukemea vikali tamko la kiongozi mmoja wa dini, ambaye alitamka rais akiwa jukwaani kwamba wanasiasa hawapaswi kutufundisha wachungaji. Alitamka maneno hayo kwa jeuri, kuonesha kabisa ana msimamo usioyumba na hataki kushauriwa,”alisema Kakobe.

“Kama tunasema maadili ya viongozi wa serikali yamemomonyoka wa kwanza kukemewa ni viongozi wa dini kwa sababu wao ndio chanzo kikubwa,” alisisitiza.

Pia Kakobe alimpongeza mwanasiasa mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru, kwa hatua yake ya kuupinga hadharani, waraka wa Kanisa Katoliki na kwamba kiongozi huyo, anaona mbali.

Alisema kwa huyo hiyo, mzee Kingunge amedhihirika kuwa hata watu wasio na dini, wanaweza kuongoza vizuri.


Habari imendikwa na Hussein Kauli, Levina Chengula na James Magai

Chanzo: Gazeti la Mwananchi
 
Kweli mchungaji Zacharia kakobe umenena.

Nakupa tano mkuu
 
We huoni anajigonga gonga? kaanza vizuri kuongea mwishoni kaharibu!!


Inanikumbusha suwala lililoulizwa hapa jamvini eti ..".kwanini BAKWATA wanaupinga waraka wa Maimamu".
Isipokuwa sina budi kukiri kuwa KAKOBE ana point lakini BAKWATA wanatafuta favour kwa Serikali.
 
Pia Kakobe alimpongeza mwanasiasa mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru, kwa hatua yake ya kuupinga hadharani, waraka wa Kanisa Katoliki na kwamba kiongozi huyo, anaona mbali.

Alisema kwa huyo hiyo, mzee Kingunge amedhihirika kuwa hata watu wasio na dini, wanaweza kuongoza vizuri.

Nimependa sana maneno hayo ya Askofu.
 
kakobe hajasoma huo waraka,angesoma angeona kuwa unaelekeza jinsi ya kuchagua viongozi wasio MAFISADI.Vinginevyo naye atakuwa sehemu ya hao MAF.........kama anavyofanya yeye kwa kuwaregister waamini wake wanapata shilingi ngapi hata kama anauza mihogo mitaani kariakoo
 
Inanikumbusha suwala lililoulizwa hapa jamvini eti ..".kwanini BAKWATA wanaupinga waraka wa Maimamu".
Isipokuwa sina budi kukiri kuwa KAKOBE ana point lakini BAKWATA wanatafuta favour kwa Serikali.

Jamani mbona sisi ni watu wa kusahau kirahisi?! Juzi juzi tu Kakobe amenukuliwa na magazeti nchini akihamasisha watanzania tususie uchaguzi wa serikali za mitaaa na baadee uchaguzi mkuu na sikuona hata comment moja toka serikalini au kwa wanaharakati. Leo hii waraka wa wakatoliki unaowaelimisha wananchi kuchagua viongozi bora imekuwa nongwa? Nani mchochezi kati ya Kakobe anayewambia wananchi kususia uchaguzi au waraka unaotoa elimu ya uraia? Labda niulize swali. Kama ingekuwa ni Kardinali Pengo amesema wananchi wasusie uchaguzi mwaka huu na 2010, reaction ingekuwaje? Si angeitwa mhaini? Mbona Kakobe haijaitwa hivyo? Why should people see a "snake" in every little shrub?

Anachoifanya Kakobe ni opportunist ya hali ya juu. kama alivyosema Askofu Kilaini leo Kanisa Katoliki na Kakobe ni paka na chui kwa hiyo Kakobe amepata mwanya wa kuleta uchonganishi tu kati ya Pengo na serikali. Hata hivyo nina imani kanisa litampuuza na hakuna haja ya kuendelea na malumbano kwa sasa.
 
kakobe hajasoma huo waraka,angesoma angeona kuwa unaelekeza jinsi ya kuchagua viongozi wasio MAFISADI.Vinginevyo naye atakuwa sehemu ya hao MAF.........kama anavyofanya yeye kwa kuwaregister waamini wake wanapata shilingi ngapi hata kama anauza mihogo mitaani kariakoo
Amenena ili na yeye aonekane yupo...
 
Kakobe ni sawa na jambazi tu, hata wanaabudu ktk kanisa lake nina wasiwasi nao. Dhahabu alizokuwa anakusanya amepeleka wapi? kwanza anatakiwa ashitakiwe.

Hata siku moja mhuni kama kakobe hataweza kujilinganisha na Pengo mpaka atakufa, wala hiyo FGBF haitaweza kuifikia RC mapa mwisho wa dunia. Wataishia kupora sadaka za waathirika na wagonjwa wengine tu, na hii ni dhambi.

Huwezi kuwa na akili timamu ukaenda kuabudu kwa kakobe, labda uwe mgonjwa na umekata tamaa ya kuishi.
 
kakobe hajasoma huo waraka,angesoma angeona kuwa unaelekeza jinsi ya kuchagua viongozi wasio MAFISADI.Vinginevyo naye atakuwa sehemu ya hao MAF.........kama anavyofanya yeye kwa kuwaregister waamini wake wanapata shilingi ngapi hata kama anauza mihogo mitaani kariakoo

kwanza kakobe ni darasa la ngapi mpaka akosoe waraka ulioandaliwa na wataalam waliobobea?

Nakumbuka wakati anauza kanda za nyimbo pale temeke, sijui kama alienda shule zaidi.
 
Habari za shughuli wana JF. Nimesoma habari ya huyu bwana Askofu kuhusu waraka wa wakatoliki nimebaki kujiuliza kama huyu Askofu ameenda shule au laa. Fikiri mtu anayejiita askofu anapoteza muda wake kuwakalisha waandishi wa habari kujadili jambo ambalo kurasa zake zilishafungwa. Je anataka kujiosha kwa JK? Mtakumbuka wakati wa Mkapa alimuunga mkono sana mzee wa Kiraracha na kuikandia sana serikali ya Mkapa. Leo hii namshanga kukandia waraka ambao unawaelimisha wananchi wote na siyo wakristu tu kiongozi anayefaa kuchaguliwa. Najiuliza kama ameenda shule kwa sababu mtu aliyeenda shule akiusoma waraka husika hawezi kuukandia hata kidogo. Jambo la kushangaza amekaa muda mrefu sana tangu waraka huu utoke bila kusema chochote ndo anakumbuka shuka wakati kumekucha na mbu wameshamtafuna kisigino. Nawaomba waumini wake wale wasomi wamshauri asiwe anazungumza na waandishi wa habari bila kushauriana na wasomi kwa maana naamini atakujaishia pabaya. Anaweza kujilinganisha na Pengo mwenye PhD na anayefikiri kabla ya kusema ama kutenda. Aende shule kwanza huyu ndo ajiite askofu.Anasema anachukua nafasi ya waandishi wa habari kumkemea Pengo kwa kuthubutu kutamka bila woga mbele ya Rais kuwa kuwa wanasiasa hawawezi kufndisha wachungaji kuhusu nyaraka zao. Je hii si kweli? Kama ni kweli kwa nini ajifarague mbele za watu? Naamini ni ujinga na umemtawala na kutojua wajibu wake kama mchungaji mbele ya wanasiasa. Aache kuficha madhambi yake kwa kujipendekeza kwa Rais. Hebu tujadili jambo hili kwa wale wenye nafasi. Karibuni.
 
Atakuwa hajasoma waraka,kasikiliza tu malumbano.Hajatuambia kama alishatubu alipowadanganya watz kwa mrema ni chaguo la mungu.Mapepo tu tamemjaa......
 
alipokosa dili la kuuza kanda za ASSMBLESS OF GOD KARIAKOO ndio akaamua kujitoa na kuanzisha DHEHEBU lake linalokataliwa na Viongozi wengine wa dini
 
Kakobe sasa anatapatapa, tumweke upande gani?

Na Waandishi Wetu

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe amemhisi Rais Jakaya Kikwete, kuvunja ukimya na kuzima mijadala kuhusu nyaraka za kidini, inaoendelea nchini.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Askofu Kakobe alisema nyaraka hizo zinaelekea kuwagawa watu na hatua zisipochukuliwa, zinaweza kusababisha vita ambavyo havitakwisha.

“Rais wetu ni mpole sana, mcheshi na ni mtu wa watu, hilo si tatizo kubwa kwake, lakini ukiwa na rais mpole sana ni tatizo, hata ukiwa mkali sana ni tatizo pia, namhisi hili aliingilie kati,” alisema Kakobe.

Kakobe alisema baadhi ya viongozi wa kisiasa, wamekuwa wakiogopa kukemea vitendo vinavyofanywa na viongozi wa dini kwa sababu tu wanawaogopa.

“Napenda kusema kuwa, viongozi wa kisiasa kunyamazia maovu yanayofanywa na viongozi wa dini kwa sababu tu kuwaogopa, kunaweza kuwaingiza watu wote kwenye uovu,” alionya Kakobe.

Mbali na hayo Kakobe amepinga vikali tamko la kiongozi mmoja wa kanisa aliyejibu hoja ya kiongozi mmoja wa kisiasa aliposema wanasiasa hawawezi kuwafundisha kazi maaskofu.

“Nichukue nafasi hii kukemea vikali tamko la kiongozi mmoja wa dini, ambaye alitamka rais akiwa jukwaani kwamba wanasiasa hawapaswi kutufundisha wachungaji. Alitamka maneno hayo kwa jeuri, kuonesha kabisa ana msimamo usioyumba na hataki kushauriwa,”alisema Kakobe.

“Kama tunasema maadili ya viongozi wa serikali yamemomonyoka wa kwanza kukemewa ni viongozi wa dini kwa sababu wao ndio chanzo kikubwa,” alisisitiza.

Pia Kakobe alimpongeza mwanasiasa mkongwe nchini Kingunge Ngombale Mwiru, kwa hatua yake ya kuupinga hadharani, waraka wa Kanisa Katoliki na kwamba kiongozi huyo, anaona mbali.

Alisema kwa huyo hiyo, mzee Kingunge amedhihirika kuwa hata watu wasio na dini, wanaweza kuongoza vizuri.
Habari imendikwa na Hussein Kauli, Levina Chengula na James Magai
http://www.mwananchi.co.tz/newsrids.asp?id=14333
 
sipendi kuwazungumzia watumishi wa mungu lakini hili la Kakobe nitalizungumzia. Kakobe anapenda kuja na vitu contraversial ili kutafuta attention n
 
Na Waandishi Wetu








“Napenda kusema kuwa, viongozi wa kisiasa kunyamazia maovu yanayofanywa na viongozi wa dini kwa sababu tu kuwaogopa, kunaweza kuwaingiza watu wote kwenye uovu,” alionya Kakobe.



Habari imendikwa na Hussein Kauli, Levina Chengula na James Magai

Chanzo: Gazeti la Mwananchi

Uovu uliopo katika waraka wa RC upo wapi? mbona hajautaja?
 
Kuna nyeti kuwa huyu bwana Kakobe ni msilamu, na jina lake ni Zahoro. Hivyo sistushwi saaana na sarakasi zake. Tutegemee kuona mengi kabla ya 2010.
 
Kwanza hao waandishi wameishia darasa la ngapi? mara mbili wameandika amemhisi badala ya amemsihi...maana mbili tofauti kabisa!

Pili, kakobe anajulikana, wala watu wenye akili zao hawawezi kupoteza muda kumsikiliza. Ndo maana anamsifia Kingunge. Ni opportunist tu hana lolote, anatafuta attention
 
Kakobe ni sawa na jambazi tu, hata wanaabudu ktk kanisa lake nina wasiwasi nao. Dhahabu alizokuwa anakusanya amepeleka wapi? kwanza anatakiwa ashitakiwe.

Hata siku moja mhuni kama kakobe hataweza kujilinganisha na Pengo mpaka atakufa, wala hiyo FGBF haitaweza kuifikia RC mapa mwisho wa dunia. Wataishia kupora sadaka za waathirika na wagonjwa wengine tu, na hii ni dhambi.

Huwezi kuwa na akili timamu ukaenda kuabudu kwa kakobe, labda uwe mgonjwa na umekata tamaa ya kuishi.
Magezi,
Angalia hayo maneno highlighted;Toa hoja,usitukane,tujadili hoja ya Kakobe!Je viable? au ina utata gani? usiwe na hasira.
 
Back
Top Bottom