View attachment 258248
Kahawa ziko kila bei na kila ladha. Tanzania tunalima sana aina ya arabica kuliko robusta.
Katika picha nimenunua Japan, yen 1300, kama usd 12.
Tatizo kubwa ni bei kwa wakulima. Middle man ndiyo anachukua faida. Mkulima anapata $1-3 kwa kilo. Hiyo ya picha ni gram 200 tu, $12 ikifika madukani.
Afrika Mashariki, Uganda ndiyo bingwa wa kuzalisha, akifuata Tanzania na mwisho Kenya.
Mabingwa wa uzalishaji duniani ni Brazil.
Kahawa zao zipo katika migahawa kama zetu lakini pia zinauzwa na makampuni ya kimataifa kama nestle. Hapo ndiyo kuna pesa. Ukiweza kuwauzia hao, umeshinda game.
Inabidi ujipange katika biashara hii. Bila kuuza mwenyewe nje, hutapata faida.
7-11 wananunua jumla kutoka kwa mtu wa Kati. Mkulima wetu hapati kitu hapo. Sawa sawa na kahawa ya picha juu. Faida karamba mjanja.
View attachment 258257
View attachment 258258