Kahama VS Njombe/Mafinga

Hicho kichwa chako kina upungufu wa akili, huwezi kufananisha michembe na biliani.🀣🀣🀣
 
Mimi sio Msukuma na siishi Kahama, kwetu Kaskazini, siongei kwa sababu ya Ubena au Ukinga. Nimefanya kazi Kahama miaka sita iliyopita. Sina msukumo wa ukanda au ukabila kwenye huu uzi.
 

Yan ukiongelea magari ya mizigo nk hii barabara ya TAZAM huwezi kulinganganisha na barabara nyingine yeyote Tanzania hii ndo barabara yenye gari nyingi TANZANIA ipo busy masaa 24 inapita miji ya iringa ,mafinga ,makambako ,mbeya na tunduma na hayo malori 300 hayo Ni idadi ya kitoto Sana Ni sawa na yanayopakia makaa ya mawe mgodi mmoja mbinga songea
 
Mimi sio Msukuma na siishi Kahama, kwetu Kaskazini, siongei kwa sababu ya Ubena au Ukinga. Nimefanya kazi Kahama miaka sita iliyopita. Sina msukumo wa ukanda au ukabila kwenye huu uzi.
Hakika hawajui kuwa na ww ni mchaga mwenye itikadi zako za ukweli na uwazi, shukurani kwako Moses Swai, wanazani kila mtu anayetetea Mwanza au sehemu yoyote ya kanda ya ziwa basi ni msukuma.
 
Kampuni za mabasi Dar-Njombe hapo sitaki kugusa zile Dar-Njombe-Songea/Mbinga au Dar-Njombe-Makete.
Au Yale ya Dar-Makambako(Njombe) mbeya,Rukwa,Halale,Lilongwe,Lubumbashi au Lusaka.

1.Njombe express(two in one)
2.ABC safaris
3.Luwinzo Bus service(two in one)
4.Japanese bus services
5.Galaxy exodus.
6.Mwalimi(Wende lipwela) safari
7.Sweet Africa express.(two in one)
8.Super HD.
Ongezea sana yanayopita kama vile
Superfeo Dar Njombe Ruvuma.
Selous bus services- Dar Njombe Ruvuma
New force Dar Njombe Ruvuma.
Kilimanjaro express Dar -Njombe -Ruvuma etc
Ongezea pia
Jacob Bus services Dar-Njombe- Makete.

Tukija kwa safari nyingi kama Njombe- Dodoma/Singida/Arusha kuna kampuni kadhaa
Another G Njombe-Dodoma
Kapricon
Kimbinginyiko etc....

In short Njombe is among of the busiest region on transport business.Ukichukua tena kwenye Cargo huko ndio usiseme.Bado safari fupi fupi za Njombe-Moro,Njombe-Tunduma,Njombe-Songea,Njombe-mbinga,Njombe-mbeya,Njombe-Iringa etc
 
kahama noma wana kesha, ni centre point ya kupoa kwa gari za dar-bukoba na kigoma
1.fursa ya malaya ipo
2. migodi pia ipo
3.wasukuma wapo
 

Hapana, kwa sasa Kahama inaizidi Njombe tuseme tu ukweli. Njombe mjini bahati mbaya haiko barabara kuu ya TANZAM ambako magari uliyoyataja yanapita. Ingekua Njombe ni Makambako, issue ya Magari uliyoyataja ni sawa. Lakini Kahama inapokea mabasi mengi sana ya kutoka Dar. Na mabasi mengi kutoka:
1. Geita
2. Mwanza
3. Dodoma
4. Musoma
5. Bukoba
6. Shinyanga
7. Tabora
8. Moshi
Mimi ni mdau wa corridor letu la Kusini lakini kwa hili, Kahama inaizidi Njombe mji!
Madini na ujio wa wageni wengi umeisaidia Kahama
 
Kwa hiyo barabara kuu hapa Tzn ni Tanzam pekee? Punguza kula viporo vya mchembe na mapanki..

Njombe iko barabara kuu ya Makambako-Songea-Mbamba Bay/Tunduru-Masasi-Mtrwara.

Kana kwamba haitoshi Njombe ni mzalishaji mkubwa wa Mazao ya miti sawa na Mafinga kwa hiyo malori na mabasi yako kama yote..

Mabasi yote yanayoanzia Songea kwenda Mikoa ya Kati,Kanda ya Ziwa,magharibi nk lazima yapite Njombe and vice versa ukiacha yanayoanzia Njombe penyewe.

Mfano Sumbawanga-Songea.

Tunduma-Mbinga/Mbamba bay.

Mbeya-Tunduru-Masasi.

Songea-Mwanza via Dom.

Songea -Arusha.

Njombe-Dom-Arusha.

Songea-Dodoma.

Songea-Dar via Iringa .

Mbeya -Mtwara via Songea-Masasi.nk nk
 
Jamaa wa Kahama anazungumzia population ya Kahama ambayo ni maskini kusafiri hadi wapate msiba πŸ˜‚πŸ˜‚..

Njombe ni Mkoa wa biashara na wenye watu wenye stable income kumbuka wametapakaa kila Kona ya Tanzania kwa hiyo ndio maana kuna mabasi mengi.

Mkuu umesahau na lile bus linaanzia Makete-Njombe-Dar.

Twende Kazi πŸ‘‡



 
Sasa nimepata updated land value 2021, tutaenda kuangalia CBD ya Kahama na Njombe thamani ya kila eneo. Nadhani kwa eneo hilo tunaweza funga huu mjadala.
KAHAMA CBD vs NJOMBE CBD

( Land Value as per Ministry of Lands )



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…