Kahama VS Njombe/Mafinga

Kahama VS Njombe/Mafinga

We bado tunakwambia kwa kuhusu suala makazi na future ya mkoa kwa rasilimali ilizo nazo geita kwa njombe imesha achwa tayar Yan geita kinacho wainuaga muonekane NI madini tu Tena ya aina moja tofauti na njombe ambayo kwa Sasa Ina kila fursa na eneo hili ndilo litakalo unda jiji la njombe kulingana na UWEKEZAJI una endelea na ndio miji inavotakiwa kuwa Sasa jamaa unaanza kutuletea kambi za wachimbaji wa madini unasema mji madini yakiisha wanakimbia hakuna uchumi endelevu njombe wametengeneza uchumi endelevu unao mgusa hata raia wa chini huji kusikia analia njaa
Katoro itakuwa jiji kabla ya njombe save hii post
 
Endelea kujifariji, unaijua vizuri Katoro!? Kwa kanda ya ziwa miji ya kibiashara ukiacha Mwanza na Kahama the next ni Katoro, Masumbwe, Runzewe na Ushirombo ni balaa jingine kanda ya ziwa.
Tanwat viwanda vinazidi kutanuliwa
Sabasaba.png
 
Endelea kujifariji, unaijua vizuri Katoro!? Kwa kanda ya ziwa miji ya kibiashara ukiacha Mwanza na Kahama the next ni Katoro, Masumbwe, Runzewe na Ushirombo ni balaa jingine kanda ya ziwa.
Mwanza itaendelea kuwashikilia miaka yote Kanda ya ziwa hakuna mji wenye future kidogo shinyanga wanajitahidi kwa viwanda mingine ni kambi za migodi madini yakiisha biashara inawakata
 
WAWEKEZAJI WA PAULOWNIA WAKUTANA NA MKUU WA MKOA WA NJOMBE

Njombe, 28 Aprili 2024 — Wawekezaji kutoka kampuni ya Now Investment Partners Inc ya Marekani kwa kushirikiana na Cetawico Ltd ya Dodoma wakiongozwa na Dr.Fiorenzo Chesini na Mrs. Katherine Mwimbe Kamm wamekutana na Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Hillside Hotel Njombe. Katika kikao hicho, wawekezaji hao wamewasilisha nia yao ya kuwekeza katika mkoa wa Njombe kwa kulima miti ya Paulownia, kama walivyofanya katika nchi mbalimbali duniani.

Wakiongozwa na Dr. Sören Buttkerreit na Daniel Povel, wawekezaji hao wameeleza kuwa wanahitaji eneo la takribani hekta 4000 kwa ajili ya kuanzisha mashamba ya miti hiyo, kutokana na kuvutiwa na ardhi yenye rutuba na hali ya hewa ya Njombe inayofaa kwa kilimo cha Paulownia. Wameeleza kuwa uwekezaji huo unalenga kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kuongeza fursa za ajira kwa wakazi wa mkoa huo.

Mhe. Mtaka aliwapongeza kwa kuchagua Mkoa wa Njombe kuwa sehemu ya uwekezaji wao na kuahidi kuwapa ushirikiano wa karibu, huku akisisitiza dhamira ya mkoa wa Njombe ya kuendelea kuvutia wawekezaji wenye tija kwa maendeleo endelevu ya wananchi na taifa kwa ujumla.

View: https://www.instagram.com/p/DJANE9eO-us/?igsh=MXNueWhid2ZuMjZyag==
IMG-20250429-WA0034.jpg
 
Mwalimu Mathew Levi Alex ambaye ni Meneja wa shule ya @thegloryschools amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa umoja wa wamiliki wa shule na vyuo binafsi {TAMONGSCO} kanda ya Nyasa, kupitia uchaguzi uliofanyika leo Aprili 30,2025 kwa kupata kura 16 kati ya kura 18.

Mathew Levi Alex ameibuka mshindi baada ya kumshinda mgombea mwenzie Madam Bahati wa shule ya @brightstarschoolstz aliyepata kura 2 kati ya kura 18.

Mara baada ya kushinda katika nafasi hiyo Mathew, amewashukuru wanachama wa umoja huo kwa kumuamini kuwa mwenyekiti huku akiahidi kuwa hata waangusha katika kutumikia nafasi hiyo.

@makambakotc
FB_IMG_17429553741739260.jpg
 
Back
Top Bottom