Kahama VS Njombe/Mafinga

Kahama VS Njombe/Mafinga

FB_IMG_17440137566615734.jpg
 
MKUU WA MKOA WA NJOMBE, MHE. ANTHONY MTAKA, ASHIRIKI KILELE CHA MAADHIMISHO YA WIKI YA AFYA KITAIFA 2025 – NJOMBE YAIBUKA MSHINDI WA JUMLA

Dodoma, Aprili 8, 2025
Na. Chrispin Kalinga

Maadhimisho ya kilele cha Wiki ya Afya Kitaifa mwaka 2025 yamefanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma, yakibeba kaulimbiu isemayo: “Tulipotoka, Tulipo na Tunapoelekea; Tunajenga Taifa Imara Lenye Afya.” Tukio hili limehudhuriwa na viongozi wa kitaifa, wataalam wa afya, wadau wa maendeleo pamoja na washiriki kutoka mikoa yote ya Tanzania.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Anthony Mtaka, ameungana na viongozi wengine wa kitaifa kushiriki tukio hili muhimu akiwa ameambatana na viongozi kutoka Njombe. Miongoni ni: Eng. Joseph Mutashubilwa – Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Mhe. Juma Sweeda – Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Dkt. Juma Mfanga – Mganga Mkuu wa Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri za Njombe Mji, Njombe DC na Makambako, Wenyeviti wa Halmashauri za Wilaya ya Njombe, Makambako na Njombe Mji, Waganga Wakuu wa Halmashauri, Maafisa Afya wa Halmashauri, Waganga Wafawidhi wa Vituo vya Kutolea Huduma za Afya, Watendaji wa Vijiji na Kata, Wenyeviti wa Vijiji na Mitaa.

Ushiriki wao umeonesha dhamira ya dhati ya Mkoa wa Njombe katika kuboresha afya ya jamii na mazingira bora kwa wananchi, sambamba na kuendeleza sera ya afya inayomgusa mwananchi moja kwa moja.

Katika kilele hicho, Mkoa wa Njombe umeibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya Afya na Usafi wa Mazingira kwa mwaka huu, baada ya kung’ara katika makundi mbalimbali ya mashindano. Taasisi kutoka Njombe zimepata ushindi katika zaidi ya makundi tisa, hatua iliyosababisha mkoa huo kutunukiwa gari aina ya Toyota Landcruiser Hard Top kama zawadi ya heshima.

Miongoni mwa washindi kutoka Njombe ni:

Halmashauri ya Mji wa Njombe

Halmashauri ya Wilaya ya Njombe

Mtaa wa Nazareth na Mtaa wa Sido Njombe Mjini

Kijiji cha Ikuna na Kijiji cha Kidegembye Njombe DC

Shule ya Msingi Kakora

Shule ya Sekondari ya Wasichana Njombe

Hospitali ya Wilaya ya Njombe – Kibena

Ushindi huu mkubwa ni matokeo ya juhudi za pamoja kati ya viongozi wa mkoa, watendaji na wananchi, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera za afya na mazingira.
 
Kwa Sasa kama unataka kusafiri na treni halafu upo Mbeya inatakiwa upande gari kutoka Mbeya mpaka Makambako ndipo upande treni maana kwa Sasa Tazara wamefulia abiria wa kule Mbeya wengi waliacha kupanda treni kwa hiyo treni inaishia Makambako maana abiria wa kwenda Mbeya ni sawa na basi Moja tu kwa treni nzima... Hili ni anguko kubwa sana na inasemekana kutokuepo kwa Mukuba express kumechangia abiria wengi kupotea maana asilimia kubwa ya abiria wa huku Tanzania wanaipenda Ile Mukuba express kwa kuwa treni ya Kilimanjaro imeshapitwa na wakati imechakaa sana kwa ufupi ni kuwa Mukuba express ina wateja wengi sana Tanzania kuliko Zambia ndio maana isipokuepo na abiria wanapotea kama Hali ilivyo Sasa...
FB_IMG_17442771041215713.jpg
 
RASMI MJI WA NJOMBE NA MAKAMBAKO INAENDA KUUNGANA SASA KUPITIA HII PROJECT 👇👇👇KIWANJA CHA NDEGE CHA KISASA KUJENGWA NJOMBE KARIBUNI

Naibu Waziri wa Uchukuzi David Kihenzile amesema kwa mwaka wa fedha 2025/2026 Serikali inatarajia kutenga fedha kwa ajili ya kukamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa kiwanja cha ndege cha kisasa cha Njombe, na tayari Serikali imeidhinisha taarifa za awali za upembuzi yakinifu na usanifu wa kina ambapo zaidi ya shilingi milioni 800 zilitengwa kwa mwaka 2024/2025.

Akijibu swali la Mbunge wa Njombe Mjini, Deodatus Mwanyika bungeni Dodoma Aprili 10, 2025, Kihenzile amesema mara baada ya taratibu hizo kukamilika, ujenzi utaanza kulingana na upatikanaji wa fedha.

Akielezea umuhimu wa Kiwanja cha Ndege cha Njombe, Kihenzile amesema ni muhimu kimkakati hususani kwenye kukuza uchukuzi katika usafiri wa anga kijamii, kiuchumi na kibiashara ikiwemo biashara ya mazao ya misitu, mbogamboga, matunda (maparachichi) ambayo yote hayo huzalishwa na kusafirishwa nje ya nchi.

Aidha, kufuatia uboreshwaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) uliopelekea manunuzi ya ndege kubwa ya mizigo aina ya Boeing 767-300 F, Serikali kupitia Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA) kwa kushirikiana na Mkoa wa Njombe imekamilisha uchambuzi wa eneo jipya la TANWAT kwa ajili ya ujenzi wa kiwanja kipya cha ndege, na sasa Serikali inaendelea na taratibu za utwaaji wa ardhi.
 
MAKAMBAKO TC Ujenzi wa kumbi na hotel upo Moto hii NI kutokana na ku host mikutano mingi ya Kanda kitu ambacho miaka ya nyuma hakikukepo jiografia imejieleza
FB_IMG_17446858177853734.jpg
FB_IMG_17446857547406080.jpg

Chama Cha ACT Wazalendo Nchini Tanznaia Katika Kuelekea Uchaguzi Mkuu Wa Rais Wabunge Na Madiwani Mwaka Huu 2025 Kimeendesha Mafunzo Ya Uongozi Kwa Viongozi Wake Wa Mikoa Ya Nyanda Za Juu Kusini Mwa Tanzania Ambayo Ni Iringa, Mbeya, Songwe Na Njombe.

Mafunzo Hayo Ya Siku Moja Yamefanyika April 13,2025 Mjini Makambako Na Yalufunguliwa Na Kiongozi Wa Chama Wa Chama Hicho Bi Dorothy Semu Ambae Amewataka Viongozi Wake Kwenda Kuhakikisha Wanakiimarisha Chama Hicho Katika Maeneo Yao.

Aidha Kiongozi Huyo Amewataka Wanachama wa Chama Act Wazalendo Kufahamu Ya Kwamba Kuhusu Suala La Kushiriki Au Kutokushiriki Uchaguzi Mkuu mwaka huu 2025 Suala Hilo Imeachiwa Kamati Ya Viongozi Baada Ya Kufanyika Kwa Tathmmini Ya Mambo Ote Muhiu Ambayo Yamewekewa Mkazo.
FB_IMG_17446887987047474.jpg
 
MKUTANO WA KANDA WA TATHMINI YA HUDUMA ZA AFYA YA UZAZI NA MTOTO WAANZA NJOMBE

Na. Chrispin Kalinga, Njombe | Tarehe: 14 Aprili 2025



Washiriki kutoka mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma wamekusanyika kujadili utekelezaji wa huduma hizo muhimu katika kipindi kilichopita, pamoja na kuweka mikakati ya pamoja ya kuboresha huduma hizo katika mwaka unaofuata.

Katika mkutano huu wa Kanda, taarifa mbalimbali zimewasilishwa na kujadiliwa, zikiwemo:

1. Taarifa Halisi ya Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto kwa Kanda

2. Taarifa kutoka kwa kila Mkoa (Njombe, Iringa na Ruvuma)

3. Taarifa ya Utekelezaji wa Mfumo wa M-Mama

4. Taarifa ya Ukusanyaji wa Damu Salama

Mkutano huu wa Kanda unatarajiwa kutoa fursa kwa wadau kubadilishana uzoefu, kubaini changamoto, na kuimarisha ushirikiano katika utoaji wa huduma bora kwa wanawake na watoto katika kanda ya Nyanda za Juu Kusini.
 
Back
Top Bottom