Kagera: Viongozi wa Chama cha Ushirika Karagwe wahukumiwa kwa Ubadhirifu wa Tsh. Milioni 40

Rare Sapphire

JF-Expert Member
Jul 24, 2021
576
1,626
KAGERA: Mahakama ya Wilaya Karagwe imewahukumu waliokuwa waajiriwa wa Chama cha Ushirika Caisalius Mathias Rugemalira (Kaimu Meneja), Renatus Gerald, (Kaimu Mhasibu) na Revelian M. Makune, (Mwenyekiti wa Bodi) kwenda jela Miaka 2 au kulipa faini ya Tsh. 1,800,00 kwa Ubadhirifu wa Fedha za Chama hicho.

Pamoja na makosa mengine ya ubadhirifu, viongozi hao walishtakiwa kwa kosa la wizi wa fedha za Chama cha Ushirika Karagwe (KDCU) kiasi cha Tsh. 40,000,000 .

Aidha, pamoja na hukumu hiyo washtakiwa wameamriwa kurejesha kiasi chote cha fedha kilichoibiwa (Tsh. 40,000,000/=).
 
Vipi wale waliotajwa kwenye report ya CAG watahukumiwa lini?
 
Nchi ya kisenge sana hii, watu wanapiga mabilioni ya pesa huko wanakuja kuhangaika na milioni 40 ya kuhongea mwanamke gari.
 
Back
Top Bottom