Mkurugenzi wa TALGWU, Mhasibu na Mkuu wa Mikopo wafikishwa Mahakamani kwa Ubadhirifu wa Tsh. Milioni 133.5

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
DAR: Watumishi 4 wa akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) akiwemo Mkurugenzi Mtendaji, Jackson M. Ngalama, Emmanuel G. Mdoe (Mhasibu), Pamela M. Sellemia (Mkuu wa Idara ya Mikopo), Timothy P. Mashishanga (Dereva) wamefikishwa Mahakamani kwa Ubadhirifu wa Tsh. 133,584,000.

Washtakiwa wote kwa pamoja wamekushtakiwa kwa Matumizi Mabaya ya Madaraka, Kusaidia Kutenda Kosa na Ufujaji wa Fedha, makosa ambayo ni kinyume na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na Sheria ya Uhujumu Uchumi.

Baada ya kusomewa mashtaka, Washtakiwa walikana makosa yote na kurejeshwa Mahabusu kwasababu wanakabiliwa na kesi nyingine ambayo haina dhamana. Kesi imeahirishwa hadi Februari 14, 2024 kwaajili ya kusomwa hoja za awali.
 
Vifaranga wa mwewe ndio wamendaliwa kukaangwa kikaangoni ila mwewe wakubwa wanapishana bank na takukuru na mkono wa pongezi wanapewa.
 
Hawa viongozi wa chini wanawajibishwa sawa, Vipi kuhusu hawa wajuu wanaoiba mabilioni..!!

Mwaka jana mwishoni Kuna shehena ya jezi feki za yanga zilikamatwa mwenye shehena hakujulikana kesi haijulikani iliishia wapi, Mzigo ulipitaje bandarini ! Taarifa za mwenye mzigo TPA hawakuzijua ! Hata mtoto huwezi mdanganya, ukiachilia hilo Fedha nyingi zinapotea serikalini na watu hawawajibishwi, kama sheria iliwekwa kwaajiri ya watu wote basi haki itendeke.

Note: Si kwamba nawatetea hawa waliofanya ubadhilifu, bali wasimamizi wa sheria wasiifanye sheria ipo kwaajiri ya watu fulani na sio watu fulani
 
DAR: Watumishi 4 wa akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) akiwemo Mkurugenzi Mtendaji, Jackson M. Ngalama, Emmanuel G. Mdoe (Mhasibu), Pamela M. Sellemia (Mkuu wa Idara ya Mikopo), Timothy P. Mashishanga (Dereva) wamefikishwa Mahakamani kwa Ubadhirifu wa Tsh. 133,584,000.

Washtakiwa wote kwa pamoja wamekushtakiwa kwa Matumizi Mabaya ya Madaraka, Kusaidia Kutenda Kosa na Ufujaji wa Fedha, makosa ambayo ni kinyume na Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na Sheria ya Uhujumu Uchumi.

Baada ya kusomewa mashtaka, Washtakiwa walikana makosa yote na kurejeshwa Mahabusu kwasababu wanakabiliwa na kesi nyingine ambayo haina dhamana. Kesi imeahirishwa hadi Februari 14, 2024 kwaajili ya kusomwa hoja za awali.
Hiyo kesi isiyo na dhamana ni ya kutakatisha fedha?
 
Back
Top Bottom