Kagera: Mlipuko wa bomu Wilayani Ngara waua Wanafunzi 05, zaidi ya 45 wamejeruhiwa

Alitoka arusha ikatokea ajali ikaondoka na watoto 32. Katoka kagera alafu nn kinatokea
 
Mlipuko Kagera Tanzania waua wanafunzi 9


Wanafunzi 9 wa shule ya msingi Kihinga mkoani Kagera kusini magharibi mwa Tanzania wamefariki dunia na wengine zaidi ya 25 wamejeruhiwa baada ya kulipukiwa na bomu.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Augustine Orom huo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na tayari wananchi wamejitokeza kuchangia damu kwa ajili ya kuwasaidia majeruhi.

Kwa mujibu wa Dokta Mariagoreth Fredrick ambaye ni mganga mkuu hosipitali ya Rurenge, amethibitisha kupokea miili hiyo na majeruhi ambao baadhi wako katika hali mbaya na tayari wanapatiwa matibabu.

"Tulionao hali ya sio nzuri. Wengine wameumia matumbo, wengine wamechanika bandama, wengine wamevunjika miguu, wengine vichwa vimepata maijraha, wengine wameumia macho." Dokta Mariagoreth ameiambia BBC.

Inaelezwa kwamba kabla ya kulipukiwa na kifaa hicho kinachoarifiwa kuwa ni bomu, wanafunzi hao walikuwa wanakichezea.

Taarifa zaidi zinafuata

Chanzo BBC
 
Inna lillaj wainna ilayh raajuun!!

Mungu awatie nguvu wazazi wa wafiwa na wenye majeraha kwenye kipindi hiki kigumu
 
Elimu ya salama mashuleni msiishie to trafic issues. Issues za landmines ni muhimu mno hasa mikoa ya mipakani.
 
Wadau,
Habari Kutoka Mkoani Kagera Zinaeleza Kuwa Wanafunzi Watano Wa Shule Ya Msingi Kihinga Wamefariki Na Wengine 18 Kujeruhiwa Baada Ya Kulipukiwa Na Bomu Mapema Leo.Shule Hiyo Ipo Mkoani Kagera Wilayani Ngara Na Wahanga Hao Walikuwa Wakikichezea Kifaa Hicho Kabla Ya Kulipukiwa.

Chanzo: Gazeti Mwananchi
Kwa Mujibu Wa BBC Waliofariki Hadi Sasa Ni 6 Wakati Waliojeruhiwa Ni Zaidi Ya 25.
Zoezi La Uchangiaji Damu Linaendelea Kuwasaidia Manusura Wa Mlipuko Huo.
Karibuni
 
So far walofariki wamefikia 6 na like 40 ni majeruhi na wengine hali zao siyo nzuri. Baadhi ya Wanafunzi wa shule za RHEC, St Alfred Rulenge na St Joseph Mbuba wamejitolea damu ktika hosp. ya Kristo Mfalme Rulenge.

Chanzo inasadikiwa kuwa ni bomu la mkono lililookotwa na mwanafunzi ktk shule ya Msingi Kihinga (mpakani mwa Tz na Burundi) kutoka kwenye sehemu ya kukusanyia vyuma chakavu!
 
Back
Top Bottom