Kagera: Mlipuko wa bomu Wilayani Ngara waua Wanafunzi 05, zaidi ya 45 wamejeruhiwa

Poleni sana wana Ngara na Watanzania wenzetu. Nikiangalia hali za hao watoto hao naamini ule usemi kuwa CCM itatawala milele navuta picha za wazazi wao nachoka.
 
R.I.P watoto wetu. Mungu awajie na kuwaponya majeruhi wote. Pole kwa wazazi, ndugu, jamaa, walimu na marafiki. Mungu awatie faraja
 
Hivi Kagera Kuna Nin Aithee Mana Mambo Mengi Kwa Miaka Ya Sasa yanatokea Huko Ok Asante Kwa Taarifa

Kiviere Wa Usangi
 
Poleni sana wana Ngara na Watanzania wenzetu. Nikiangalia hali za hao watoto hao naamini ule usemi kuwa CCM itatawala milele navuta picha za wazazi wao nachoka.
Acha kuleta uchama kwenye haya mambo
 
Mi nahisi ilo bomu chanzo chake ni vita vya kagera..kwan yanaeza kukaa muda mrefu ardhini
 
Takribani wanafunzi 3 wameripotiwa kufariki dunia mpaka sasa na wengine kadhaa kujeruhiwa kufuatia mlipuko wa bomu wilayani Ngara.

Diwani wa Kata ya Kibogora wilayani humo, Ndg Adronizi Burindoli ameeleza kuwa jitihada za kuokoa uhai wa majeruhi zinaendelea..

Taarifa zaidi zitafuata...

Mwendelezo:

========



=> Wanafunzi sita wa shule ya msingi Kihinga mkoani Kagera Kaskazini Magharibi mwa Tanzania wamefariki dunia na wengine zaidi ya 25 wamejeruhiwa baada ya kulipukiwa na bomu wakicheza.

Kamanda wa polisi wa mkoa, Augustine Orom huo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na tayari wananchi wamejitokeza kuchangia damu kwa ajili ya kuwasaidia majeruhi.

Kwa mujibu wa Dokta Mariagoreth Fredrick ambaye ni mganga mkuu hosipitali ya Rulenge, amethibitisha kupokea miili hiyo na majeruhi ambao baadhi wako katika hali mbaya na tayari wanapatiwa matibabu.

"Tulionao hali ya sio nzuri. Wengine wameumia matumbo, wengine wamechanika bandama, wengine wamevunjika miguu, wengine vichwa vimepata majeraha, wengine wameumia macho." Dokta Mariagoreth ameiambia BBC.

Inaelezwa kwamba kabla ya kulipukiwa na kifaa hicho kinachoarifiwa kuwa ni bomu, wanafunzi hao walikuwa wanakichezea.

=> Mganga wa Hospitali ya Rulenge wilayani Ngara, Kagera Sister Mariagoreth Fransis amesema wamepokea majeruhi 45 waliotokana na mlipuko unaodhaniwa kuwa ni bomu. Kati ya majeruhi hao, 13 wamejeruhiwa vibaya na wawili wamefariki

Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya msingi Kihinga,iliyopo wilayani Ngara mkoani Kagera walionusurika wakiwa Hospitali ya misheni Rulenge wilayani humo.
Madaktari wa Hospitali ya Mission Rulenge wakiendelea na Matibabu kwa Majeruhi.

Kamanga wa Jeshi la Polosi mkoani Kagera Agustino Olomi amesema chanzo cha wanafunzi hao kujeruhiwa kwa bomu ni zoezi la kuuza vyuma chakavu ambapo mwanafunzi aliliokota na kuja nalo shuleni ili alipeleke kwa mnunuzi na kupewa madaftari.

Hata hivyo Kamanda wa Kikosi cha Kulinda mipaka cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania JWTZ wilaya ya Ngara ,Meja TR Mutaguzwa amesema Bomu hilo lilikuwa na vipande 36 na lingelipukia ndani ya darasa wangeleta athari zaidi .


Kamanga wa Jeshi la Polosi mkoani Kagera Agustino Olomi amesema chanzo cha wanafunzi hao kujeruhiwa kwa bomu ni zoezi la kuuza vyuma chakavu ambapo mwanafunzi aliliokota na kuja nalo shuleni ili alipeleke kwa mnunuzi na kupewa madaftari.

Biashara ya vyuma chakavu siyo chanzo, bali chanzo ni hilo bomu kuwa mahali lisipostahili, limesaidiwa na uelewa pungufu wa mtoto.

Hata biashara ya chuma chakavu isingekuwepo, msafisha barabara au muhunzi n.k. wangeweza pia kupata au kusababisha madhara

Mapungufu kwenye surveilance, uelimishaji uma hasa sehemu za mipakani hasa kwenye migogoro ya kisiasa ndio chanzo.

Hivyo, tuepuke kutoa sababu za kuepuka kuwajibika, kwa kutoa visingizio.

On the other hand, hiyo biashara ya vyuma chakavu na madaftari ina maana imekuwepo kwa muda na main suppliers ni watoto! hivi mtoto wa Ngara ana source gani ya vyuma chakavu zaidi ya kuwapa vishawishi vya kuiba?
samahani kwa lugha kali.
Hivi tunazungumzia ajira kwa watoto, hivi kuwa na supplier wa bidhaa kama hii mtoto sio ajira kwa watoto na hata mbegu ya uhalifu?
 
Wanafunzi watano wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Kihinga wilayani Ngara mkoani Kagera wamefariki na wengine 18 kujeruhiwa baada ya kulipukiwa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu la kurushwa kwa mkono asubuhi ya leo wakati wakiingia darasani.

Kwa mujibu wa diwani wa kata ya Kibogora wilayani humo Adronis Bulindoli amesema kuwa kitu hicho kinachodhaniwa kuwa ni bomu kiliwalipukia wanafunzi hao kabla ya kuingia darasani na wengine18 kujeruhiwa ambapo wamekimbizwa katika hospitali ya Misheni ya Rurenge kwa ajili ya kupata matibabu.

Aidha Bulindoli amesema kuwa waliofariki wana umri kati ya miaka 8 hadi 9 ambapo amewataja majina yao kuwa ni ........
Kati ya hao wanafunzi watatu, wamefariki pale pale huku wawili wakipoteza maisha wakiwa njiani wakati wakipelekwa hospitali ya Rurenge.



Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmshauri ya wilaya ya Ngara Erick Nkilamachumu amesema kuwa wauguzi wa hospitali ya Rulenge wanaendelea na jitihada za kuokoa maisha ya wanafunzi waliojeruhiwa wa kata za Bugarama na Kibogora ilipo shule ya msingi Kihinga.
Shule ya msingi kihinga iko mpakani mwa nchi jirani ya Burundi ambapo baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo wanadai huenda bomu hilo lililetwa na wanafunzi wanaokuja shuleni kuuza vyuma chakavu.

Aidha Mganga mkuu wa Hospitali ya Misheni Rulenge Mariagolet Francis amekili kupokea wanafunzi 18 majeruhi na miili ya wanafunzi wawili walipoteza maisha wakiwa njiani kupelekwa hospitalini hapo

Kwa upande wa mkuu wa Wilaya hiyo Luten kanali Michael Mntenjele akiwa Wilayani Missenyi katika zira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania John Magufuli amethibitisha kutokea kwa tukio hilo. "Nimepigiwa simu kutoka Ngara nikaambiwa kwamba kuna tukio kitu kinachofanana na bomu kulipukia watoto na kutokea vifo ila sijajua ni wangapi wamejeruhiwa na vifo sijajua vingapi ila nimeagiza wataalam wangu waende kuona na kujilidhisha kama ni bomu,hivyo namie najiandaa kurudi Ngara kwa ajili ya tukio hilo kwahiyo nitatoa taarifa baadaye nikiipata taatifa kamili" alisema Mntenjele.
Wanatunzi 5 Walipukiwa Na Bomu Mkoani Kagera Na Wengine 18 Kujeruhiwa
 
Mambo ya wakimbizi hayo.
Loo!!!! mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi Amen, Habari mbaya na ni msiba mkubwa. Mungu awape wazazi moyo wa subira. Nashauri elimu itolewe kwa wananchi kuhusu kuokota vitu tusivyivifahamu vizuri, elimu hii itolewe mashuleni pia hasa katika maeneo yaliyoathirika na ujio wa wakimbizi
 
Poleni sana. Zile nduki alizoondoka nazo rais nadhani ni baada ya kupata hii taarifa labda anakuja kuwapa mkono wa pole
 
Back
Top Bottom