Kagame aburuzwe ICC

Kagame aburuzwe ICC

Naweza kusema Tanzania imekuwa inajihusisha na tatizo hilo kidiplomasia. Usisahau hiki kinachoitwa great lake region initiative ni sehemu ya kutafuta suluhu. Bado imebeba mzigo wa wakimbizi pengine kuliko nchi nyingine kutokana na instability ya Kongo.

Kuingia kwa majeshi ni baada ya kubaini kuwa huwezi kukaa meza moja na mtu kama Kagame ukawa na outcome nzuri. Kwa mataji wa mkataba wa Kampala ambao ni kumhifadhi Kagame aendeleze uuaji huwezi kuwa na muafaka. Tanzania kupitia SADC block imeamua kusaidia in that way.
Siwezi kusema imefanya 100% lakini ukilinganisha na mauaji ya watu milioni 3 yanatofanywa na coward Kagame, Tanzania is much better
Nguruvi3,

..lakini tulikuwa tunasafirisha silaha nzito za Uganda kupitia bandari ya Dsm.

..sasa ktk mazingira hayo kweli unafikiri we were working for peace, au??

..tukubali kwamba tulikosea.

cc Kabaridi
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,

..lakini tulikuwa tunasafirisha silaha nzito za Uganda kupitia bandari ya Dsm.

..sasa ktk mazingira hayo kweli unafikiri we were working for peace, au??

..tukubali kwamba tulikosea.

cc Kabaridi
Uganda is a sovereign nation. Na Uganda si kitisho kwa usalama wa Tanzania. Hatukuwa na sababu za kukataa kusafirisha mizigo yao hata kama ni silaha za kijeshi.
 
Uganda is a sovereign nation. Na Uganda si kitisho kwa usalama wa Tanzania. Hatukuwa na sababu za kukataa kusafirisha mizigo yao hata kama ni silaha za kijeshi.

..yes, lakini vurugu za Uganda ndani ya DRC zinaendelea kuathiri usalama wa Tanzania.

..wananchi wa maeneo ya Kigoma ni mashuhuda kwamba hali ya usalama mkoani kwao imekuwa mbaya tangu Rwanda na Uganda waivamie kijeshi DRC.

..hata kiuchumi naamini tumeathirika. badala ya kufanya biashara na wananchi wa DRC, tumekuwa busy kuhudumia wakimbizi, na kupambana na tatizo la proliferation of small arms.

..Zaidi, how could we be neutral wakati mwanachama mwenzetu wa SADC amevamiwa? How could we be neutral wakati majirani zetu wa DRC walikuwa wanauwawa kikatili na rasilimali zao kuporwa?

..I am not suggesting kwamba tulipaswa kuingilia kijeshi, lakini nasema tulipaswa kulaani kwa sauti na nguvu kubwa zaidi.
 
Nguruvi3,

..lakini tulikuwa tunasafirisha silaha nzito za Uganda kupitia bandari ya Dsm.

..sasa ktk mazingira hayo kweli unafikiri we were working for peace, au??

..tukubali kwamba tulikosea.

cc Kabaridi
Mkuu labda tusingesafirisha zingepitia Mombasa au kwingine, je tungekuwa tume solve tatizo. Pili, inaweza kuwa silaha ziliingia kwa jina la Uganda au Rwanda in good will kumbe zinatumika kinyume chake. Hapa nina maana kama ndivyo basi Egypt nao watapaswa kukagua silaha pale Nile na wakiona zinakuja Tanzania wana uwezo wa kuzuia kwasababu wanashaka zinaweza kutumika Congo in other way round, ndivyo tunataka?
 
Mkuu labda tusingesafirisha zingepitia Mombasa au kwingine, je tungekuwa tume solve tatizo. Pili, inaweza kuwa silaha ziliingia kwa jina la Uganda au Rwanda in good will kumbe zinatumika kinyume chake. Hapa nina maana kama ndivyo basi Egypt nao watapaswa kukagua silaha pale Nile na wakiona zinakuja Tanzania wana uwezo wa kuzuia kwasababu wanashaka zinaweza kutumika Congo in other way round, ndivyo tunataka?
Nguruvi3,

..well, kuna nchi kama Uingereza ziliiwekea Zimbabwe vikwazo vya kijeshi na ununuzi wa silaha na spare parts.

..Je, Uingereza walipaswa kuchukua uamuzi tofauti kwa kisingizio kwamba wasipouza silaha kwa Zimbabwe, Warusi, Wamarekani, na Wachine, wangewauzia Zimbabwe silaha??

..Tungeweza kuwashawishi Kenya nao wasisafirishe silaha za Uganda. Binafsi naamini Wakenya wangetuelewa.

..i am still of the opinion kwamba tungezuia silaha za Uganda, na kulaani uvamizi wa Congo waziwazi, hali ingekuwa tofauti.
 
Last edited by a moderator:
Nguruvi3,

..well, kuna nchi kama Uingereza ziliiwekea Zimbabwe vikwazo vya kijeshi na ununuzi wa silaha na spare parts.

..Je, Uingereza walipaswa kuchukua uamuzi tofauti kwa kisingizio kwamba wasipouza silaha kwa Zimbabwe, Warusi, Wamarekani, na Wachine, wangewauzia Zimbabwe silaha??

..Tungeweza kuwashawishi Kenya nao wasisafirishe silaha za Uganda. Binafsi naamini Wakenya wangetuelewa.

..i am still of the opinion kwamba tungezuia silaha za Uganda, na kulaani uvamizi wa Congo waziwazi, hali ingekuwa tofauti.
Mkuu Kenya inaweza kusimama na kusema huu ni udhalimu?
 
TZ and the international community are also guilty for having no commitment to restrain kagame by watching him reigning havoc in DRC wakati watu millioni tatu kapoteza maisha na makao yao. There several interests from outside the border from far and wide. DRC might be overwhelmed and are helpless to defend themselves, given this factmillion dollar question:what has been tzs plan of action since these killings began? cc JokaKuu
Spoton Mkuu Kabaridi, We're as guilty as HELL!! Mkuu Kabaridi hebu fikilia watu waliopoteza maisha nchini Congo sio million tatu tu ni million tano na ushee na wanaendelea kupoteza maisha - kinacho sikitisha ni Dunia kukaa kimya inawahacha wahusika wakuu wanao chochea vita na vurugu nchini DRC bila ya kuwafikisha kwenye mahakama ya kimataifa ya kushughulikia WAR criminals, badala yake ICC inakwenda kukimbizana kimbizana na akina Uhuru na RUTO wamewakalia kooni kweli kweli! Mimi naona ajabu sana kwa ni tuwe na double standard kwenye masuala ya uharifu wa kivita. Rais ambaye alikuwa anaelewa vizuri plan za akina PK na M7 kuhusu DRC na nchi jirani ni Mh Robert Mugabe. PK na M7 wanalipo vamia DRC kwa mara ya pili, Mzee Mugabe alimuomba Mh.Mkapa ampe base ya kuishambulia Rwanda akitokea Tanzania naona Mzee Mkapa alimkatalia 4 some reasons ambazo haziko clear!! Nia ya Mzee Mugabe alitaka amuondoe kabisa madarakani PK nafikili, alishajua kabisa kwamba jamaa huyu akiachwa kuendela na adventures zake in East and Central Africa, hakuna nchi ambayo atabaki salama! - Naona Utabili wa Mzee Mugabe utatimia siku si nyingi. Mimi sio mtume wala nabii lakini nataka kuwapa tahadhali Watanzania wenzangu kwamba jamaa huyu anaweka mikakati ya ku-wreak havoc katika Taifa letu - iwe covertly au overtly na uwezo huo anao sana, atashirikiana na M7 indirectly, hawa wote wanaona Tanzania ni kikwazo kwa malengo yao; kwa bahati mbaya Mh.Uhuru ajaliona hilo! Asifikili mzozo wa kisiwa cha Magingo umekufa a natural death wana buy time tu. Mh.Kenyatta anapashwa kuwa mwangalifu sana na jamaa hawa(sina hakika na spelling kisiwa) - Yale madege ya Shukhoi MK30 Museveni hakuyanunua kulinda nchi yake wala nini - aliyanunua kwa madhumuni ya kuyatumia katika vita vya kuvamia DRC kwa mara ya tatu kwa kuwa aliona Airforce ya Mugabe ilivyo chachafya majeshi ya Rwanda na Uganda nchini DRC, fundisho walilo lipata ndilo liliwafanya wanunue ndege za kwao wanafikili wanaweza ku-counter Airforce ya Zimbabwe wanasahau kwamba wakijitia wajuaji watapashwa kukabili Airforces za South Africa na Angola (i.e SADC) na kusema kweli nchi zote za SADC zimekwisha choshwa na viburi na vurugu za jamaa hawa, wakianzisha vita kwa pretext yoyote ile wajuwe itakuwa mbaya sana ambayo haijawahi kushuhudiwa barani Africa na matokeo yake kila mtu mwenye akili timamu anajua itawa-cost dearly Uganda na Rwanda, nataka kuwakumbusha wakina M7 na PK kwamba William Clinton hana tena madaraka/Mamlaka ya kuwasaidi kwa lolote hata ndege za Hercules za kubeba wanajeshi wao na silaha watakuwa wanazisikia kwenye Radio! Nataka kurudia kuwapa ushauri wa bure kwamba inapokuja katika ufanisi wa kutumia jet fighter effectively kwenye war theater what counts ni skills za fighter pilots sio ndege. Looking back now naona Lt General Weather kwenye Mount Kenya alitusadia sana kupunguza ma-Chopper Gunships ya Uganda, jamaa hawa hawapashwi kuwa na such sophisticated flying machines - uwezi kujua kesho watafanya nini! Ni wapenda vita kupindukia.
 
Lo,kumbe hata hujui FDLR or interahamwe then post zako zote PK is to blame,then unauliza kwenu mtarudi lini?you need help and go educate your azz na akili yako fupi kama panya.
lakini nyie si ndio wachokozi ni kwanini muwafuate INTARAHAMWE mpaka katika Ardhi ya DRC na kumuua Laurent Kabila?
Hivi ndio maana Tanzania inawaogopa Watutsi mnachokoza halafu mnakuja huku mkijua DRC hawezi wafuata Wakimbizi katika makambi ndani ya Tanzania.
Kaeni meza moja na wenzenu Wahutu km mlivyotoka Ethiopia na kuwakuta wakiwa na Watwa kumbukeni hamuwezi panua Himaya yenu ya HIMA tena katika Maziwa makuu
Na SIRI ya PK inaanza julikana ajiandae The Hague
 
Kituko,

..unajua hata Angola walitaarifiwa na Rwanda kuhusu mipango yao michafu.

..inasemekana jamaa wa intelligence ya Angola walitoa go ahead, lakini suala lilipofika kwa Raisi Dos Santos alipiga "veto."

..ndiyo maana ukaona majeshi ya Angola yaliingia on DRC side, na kwa kweli ndiyo waliiokoa jahazi mpaka pale Zimbabwe walipoingia na kufanya kazi kubwa zaidi.

Kaka JokaKuu, Angola au Zimbabwe walikuwa hawana direct effect ya hiyo vita, Tanzania walikuwa wanajua Uganda na Rwanda wana Silaha gani na walikuwa wana nguvu gani, ule mziki Tanzania ungemsumbua sana na solution ilikuwa ni kutoka tu DRC na kuwaacha Angola na Kisha Zimbabwe wapambane wa Wanyarwanda

the way inavyoonekana sasa Tanzania wako tayari kwa lolote, labda washeshapima uwezo wa nchi zote (Rwanda na Uganda) ama anategemea support ya SaDCC na Wamarekani ndio maana Nchi inakiburi cha kupeleka Askari front line pale Goma
 
Last edited by a moderator:
The only reason Rwanda waliingia DRC ni security yao,interahamwe,all genociders,defeated army etc wote walikimbilia Congo baada ya kufanya 94 genocide,kibaya zaidi walianza kujipanga kurudi kuvamia Rwanda tena na Mobutu alikuwa akiwapa support,solution ilikuwa ni kuingia na kupeleka battle yote ndani ya Congo na kuwamalizia huko huko...hayo mengine ya kuingia kuiba madini or Hima empire is just BS na hakuna kitu kama hicho.
 
the way inavyoonekana sasa Tanzania wako tayari kwa lolote, labda washeshapima uwezo wa nchi zote (Rwanda na Uganda) ama anategemea support ya SaDCC na Wamarekani ndio maana Nchi inakiburi cha kupeleka Askari front line pale Goma
Hii idea ya kufikiri Uganda or Rwanda wana majeshi ndani ya Congo na TZ inaenda kupigana nao sijui mmeipata wapi?hakuna wanajeshi wa hizo nchi huko wala bases,ni rebels tuu wamejaa kule kuanzia maimai,M23,FDLR etc na kuna groups zaidi ya 10 kila mtu na territory yake.
 
Hii idea ya kufikiri Uganda or Rwanda wana majeshi ndani ya Congo na TZ inaenda kupigana nao sijui mmeipata wapi?hakuna wanajeshi wa hizo nchi huko wala bases,ni rebels tuu wamejaa kule kuanzia maimai,M23,FDLR etc na kuna groups zaidi ya 10 kila mtu na territory yake.

Kaka unafikiri kuna Mpambuvu humu kwenye hii thread, wala sio siri, Kuanzia Goma mpaka Manyema nchi ya ahadi ya Wanyarwanda(Nord Kivu, Sud Kivu na MAnyema)wanajeshi wote wanaoongoza vikosi vya DRC ni Watusi wakutoka Rwanda, sio Watusi wale waliokuwa DRC kipindi cha Nyuma, Ni raisi sana kuwatambua, Lugha rasmi ya Jeshi la DRC ni Kilingala, hata kama utajua lugha zote bila kujua kilingala huwezi kuwa mwanajeshi DRC cha ajabu hao MaColonel wote wanajua Kinyarwanda na Kifaransa tu.
 
Kaka unafikiri kuna Mpambuvu humu kwenye hii thread, wala sio siri, Kuanzia Goma mpaka Manyema nchi ya ahadi ya Wanyarwanda(Nord Kivu, Sud Kivu na MAnyema)wanajeshi wote wanaoongoza vikosi vya DRC ni Watusi wakutoka Rwanda, sio Watusi wale waliokuwa DRC kipindi cha Nyuma, Ni raisi sana kuwatambua, Lugha rasmi ya Jeshi la DRC ni Kilingala, hata kama utajua lugha zote bila kujua kilingala huwezi kuwa mwanajeshi DRC cha ajabu hao MaColonel wote wanajua Kinyarwanda na Kifaransa tu.
Uraia kwako unaangaliwa kwa sura ya mtu na lugha anayoongea inaonekana,huku tulipo kuna wengi hawajui hata neno moja la Kiingereza lakini ni American citizen,watu kama nyie ndio mwanzo wa matatizo ya ukabila na vita nyingi.
 
Uraia kwako unaangaliwa kwa sura ya mtu na lugha anayoongea inaonekana,huku tulipo kuna wengi hawajui hata neno moja la Kiingereza lakini ni American citizen,watu kama nyie ndio mwanzo wa matatizo ya ukabila na vita nyingi.

Hao unaosema unakutana nao mitaani hawajuhi kiingereza na bado ni raia hilo wala sio Tatizo, Tanzania kuna wazungu na wahindi wengi ambao ni raia na Kiswahili hawajuhi, lakini ukae ukijua hata uko Marekani hao wasiojua Kiingereza wana limit, na kamwe hawezi kupewa sensitive positions Kama Regional commander, Sector Commander na vyeo vingine sensitive bila kujua Lugha husika ya nchi husika.

Katika jeshi Mawasiliano ni kitu namba moja, bila proper communication huwezi kuwa na jeshi Imara, Uganda wao waliamua kuwa kila mwanajeshi lazima aseme Kiswahili ili kurahisisha mawasiliano, lakini Congo ndio nchi ya kwanza duniani kuwa na top layer ya Jeshi isiyojua lugha ya nchi hiyo, Ni kama vile tuseme Tanzania inawanajeshi wasiojua Kishwahili kabisa itawezekana hiyo mkuu

sio kila kitu unatetea tu mkuu, kama kuna Ukweli inabidi ukubali tu
 
bukyanagandi said:
Spoton Mkuu Kabaridi, We're as guilty as HELL!! Mkuu Kabaridi hebu fikilia watu waliopoteza maisha nchini Congo sio million tatu tu ni million tano na ushee na wanaendelea kupoteza maisha - kinacho sikitisha ni Dunia kukaa kimya inawahacha wahusika wakuu wanao chochea vita na vurugu nchini DRC bila ya kuwafikisha kwenye mahakama ya kimataifa ya kushughulikia WAR criminals, badala yake ICC inakwenda kukimbizana kimbizana na akina Uhuru na RUTO wamewakalia kooni kweli kweli! Mimi naona ajabu sana kwa ni tuwe na double standard kwenye masuala ya uharifu wa kivita. Rais ambaye alikuwa anaelewa vizuri plan za akina PK na M7 kuhusu DRC na nchi jirani ni Mh Robert Mugabe.

PK na M7 wanalipo vamia DRC kwa mara ya pili, Mzee Mugabe alimuomba Mh.Mkapa ampe base ya kuishambulia Rwanda akitokea Tanzania naona Mzee Mkapa alimkatalia 4 some reasons ambazo haziko clear!! Nia ya Mzee Mugabe alitaka amuondoe kabisa madarakani PK nafikili, alishajua kabisa kwamba jamaa huyu akiachwa kuendela na adventures zake in East and Central Africa, hakuna nchi ambayo atabaki salama! - Naona Utabili wa Mzee Mugabe utatimia siku si nyingi. Mimi sio mtume wala nabii lakini nataka kuwapa tahadhali Watanzania wenzangu kwamba jamaa huyu anaweka mikakati ya ku-wreak havoc katika Taifa letu - iwe covertly au overtly na uwezo huo anao sana, atashirikiana na M7 indirectly, hawa wote wanaona Tanzania ni kikwazo kwa malengo yao; kwa bahati mbaya Mh.Uhuru ajaliona hilo!

Asifikili mzozo wa kisiwa cha Magingo umekufa a natural death wana buy time tu. Mh.Kenyatta anapashwa kuwa mwangalifu sana na jamaa hawa(sina hakika na spelling kisiwa) - Yale madege ya Shukhoi MK30 Museveni hakuyanunua kulinda nchi yake wala nini - aliyanunua kwa madhumuni ya kuyatumia katika vita vya kuvamia DRC kwa mara ya tatu kwa kuwa aliona Airforce ya Mugabe ilivyo chachafya majeshi ya Rwanda na Uganda nchini DRC, fundisho walilo lipata ndilo liliwafanya

wanunue ndege za kwao wanafikili wanaweza ku-counter Airforce ya Zimbabwe wanasahau kwamba wakijitia wajuaji watapashwa kukabili Airforces za South Africa na Angola (i.e SADC) na kusema kweli nchi zote za SADC zimekwisha choshwa na viburi na vurugu za jamaa hawa, wakianzisha vita kwa pretext yoyote ile wajuwe itakuwa mbaya sana ambayo haijawahi kushuhudiwa barani Africa na matokeo yake kila mtu mwenye akili timamu anajua itawa-cost dearly Uganda na Rwanda, nataka kuwakumbusha wakina M7 na PK kwamba William Clinton hana tena madaraka/Mamlaka ya kuwasaidi kwa lolote hata ndege za Hercules za kubeba wanajeshi wao na silaha watakuwa wanazisikia kwenye Radio!

Nataka kurudia kuwapa ushauri wa bure kwamba inapokuja katika ufanisi wa kutumia jet fighter effectively kwenye war theater what counts ni skills za fighter pilots sio ndege. Looking back now naona Lt General Weather kwenye Mount Kenya alitusadia sana kupunguza ma-Chopper Gunships ya Uganda, jamaa hawa hawapashwi kuwa na such sophisticated flying machines - uwezi kujua kesho watafanya nini! Ni wapenda vita kupindukia.

Hapa wa kulaumiwa zaidi ni serikali ya DRC; baada ya kupata msaada wa kijeshi kutoka angola tanzania mozambique na zimbabwe, wangepanga mikakati ya kuflush rebels wote nje ya mipaka na kurudisha hali ya amani, usalama, na kufanya uchaguzi wa kidemokrasia kutafuta rais atakayeongoza serikali. Kumbe mpaka leo imebainika wazi hakujakuwa na serikali yenye kutoa sera congo tangu kuangushwa kwa serikali ya mobutu.

Pili, baada ya mobutu kuifilisi nchi aliyotawala kifedha na kuhamisha hazina za congo zote kwenye benki za uzunguni, vibaraka wa mobutu walisalia hapo na kugundua jamii ya kimataifa (Un) ilitamani congo kuendelea kusambaratika, waliendelea kupokea ufadhili wa mobutu kutoka benki za uswizi kuzidi kureclaim ground na ndio labda kagame kwa hofu ya ushirikiano wa vibaraka wa Mobutu ssese seko pamoja na inter-haramwe hutu rebels, akachukua jukumu la kuivamia congo na kuweka polisi wa kirwanda kupatrol kufanya kazi na serikali ya DRC kuzuia possibilty ya inter-haramwe hutu genocidaires kupenya katika nyadhifa za 'serikali' ya congo....

System ya kufadhili vita vya africa congo has been systematically expensive, kiasi ambacho kingetumika kama msaada, ingeipa DRC matumaini ya kupata maendeleo.... na sasa mzozo huu umezidi kuwa mbaya miaka nyingi kulazimu kujiuliza maswali, itakuaje rebels wa mai mai, M23, wale wanakuwa sponsored na FDLR ya rwanda....isipokuwa kuna mkono mkubwa usioonekana. Mataifa ya SADC (tanzania) are not innocent here to be spared kwa kuruhusu DRC kuendelea kuharibika mpaka wakati huu and Rwanda on the other hand is not very innocent either!

Tatu, kumekosekana uaminifu kutoka kwa nchi za tanzania na rwanda. Sababu kubwa ikiwa si vyema kuwe na taifa la kiafrika kuharibu matumaini ya taifa lingine la kiafrika kupata amani. Kihistoria ni mataifa tu ya kikoloni zinazoeneza ideologyia hii.

lazima tanzania kureview sera zao ndani ya congo, kabla kugeuka kuwa national shame, na isiwe inagonganishwa kichwa pamoja na kagame kwenye huu mzozo.

….kama JWTZ inaogopa matokeo ya ukosefu wa usalama pande za kigoma, it is only at JWTZ best interests to act swiftly and desicively kuondoa threats zote..... cc JokaKuu...

Sadc looks formidable though fractious.....................dialogue cannot thrive kati ya matiafa husika ya SADC kwa hayaonani macho kwa macho
.....but tanzania is not in a safe spot tight federation ingawa Ni hivi majuzi imejikuta kwenye mvutano wa kidiplomasi na malawi japokuwa muungano huu ndio unajivunia kuwa na mataifa mengi zaidi barani..........It is easy kwa mataifa ya ulaya to cripple mataifa ya SADC with economic sanctions rendering them innefective diplomatically than it is to EAC....mugabe's case is real..where he can only speak from his backyard.... if mugabe is the SADC pitbul and he's confined then to his backyard then Tz can only tread delicately in DRC.....though it is easier to legally complicate matters internationally for EAC via ICC................

Ni kama kumfungia kuku kamba mahindi.....I suspect M7 will throw himself in the DRC mess very soon...but let not uhuru do this mistake kwa sababu it will be very costly in the end and probably because there is equally something from the international community to gain for pacifying rwanda and also for its destabilization! I don't know kama that makes sense lakini lazima kuangalia mambo kiundani...
......
Nne, kuna uwezekano jamii ya kimataifa imepata ishara zote Africa mashariki, janga ya kimizozo na kivita inabadilika kwa kasi; hii ni baada ya alshabab kuondolewa somali kwa kipindi kifupi mno, na ndio uhuru na ruto kawekewa vikwazo vya ICC maskudi kuwa na compund effect sio ndani kenya pekee, kama njia pia ya kuzuia geo-political consequences of resolve ya serikali za kiafrika hasa zilizostawi kiulinzi, kiuchumi na kisiasa (IGAD nations). Mugabe himself yaujua he has been carefully isolated into zimbabwe na hawezi operate outside borders mpaka pale atakapoondolewa mzigo wa economic sanctions.

Tano, (nasema mara ya pili sasa) DRC itaweza kurekebiswa pale tu palipo na mkataba wa amani. lakini kwa wakati huu haiwezekani jamii ya kimataifa kukubali uchaguzi wa kidemokrasia kufanyika. Mikataba ya amani huwekwa pale tu kuna serikali iliyochaguliwa. Huwezi kamwe kumweka ex-rebels mamlakani kwasababu hatakubali demokrasia. Yeye hujipenyeza mamlakani kutumia bunduki

Sita, Huyu political activist alice gatebuke ningetarajia moja ya mtazamo wake uwe pia kuzungumiza DRC kupata serikali iliyochaguliwa kidemokrasia kama suluhu ya pekee ambao itamaliza huu mzozo na kuzuia mengine kutokea.

Saba, Most of these political activists do not work out of sincerity, lakini wanatumia nafasi walizopata kama njia ya kupata ufadhili kusimamia mahitaji ya matumbo binafsi. kama alice gatebuke alikuwa na mawazo ya rwanda moyoni na Congo kurekebika, inambidi kufanya shughuli zake hapa barani africa. Kama the 'true daughter of rwanda' ataifia rwanda kwa sababu anaipenda, tunapaswa kumwona barani mara kwa mara. Lakini kama ni maswala ya tumbo lake mwenyewe anaangazia..... hamna lolote hapo!

My Take
Kwa maoni yangu nitakosoa SADC kwa kukosa uaminifu inaposhughulikia Kurejesha hali ya kawaida DRC , na ndio inafanya EAC to be, on a technically superior level kidiplomasia. bado EAC has not been tested.
 
Mkuu Kenya inaweza kusimama na kusema huu ni udhalimu?
Nguruvi3,

..I don't think Tanzanians and Kenyans have seriously engaged each other on matters relating to foreign policy.

..inavyoelekea ile migogoro ya miaka ya 70, and the fact that we were on the opposing camps during the cold war, bado inaendelea ku-affect mahusiano ya Tanzania na Kenya ktk miaka ya sasa.

..we need to find a way kuwa na mahusiano mazuri zaidi baina yetu, kwa faida ya wananchi wa pande zote.

cc Kabaridi, Ab-Titchaz, Jasusi
 
Last edited by a moderator:
The only reason Rwanda waliingia DRC ni security yao,interahamwe,all genociders,defeated army etc wote walikimbilia Congo baada ya kufanya 94 genocide,kibaya zaidi walianza kujipanga kurudi kuvamia Rwanda tena na Mobutu alikuwa akiwapa support,solution ilikuwa ni kuingia na kupeleka battle yote ndani ya Congo na kuwamalizia huko huko...hayo mengine ya kuingia kuiba madini or Hima empire is just BS na hakuna kitu kama hicho.

na sasa wanafanya nini DRC? au genocide dhidi ya watusi bado inaendelea?
 
Nguruvi3,

..I don't think Tanzanians and Kenyans have seriously engaged each other on matters relating to foreign policy.

..inavyoelekea ile migogoro ya miaka ya 70, and the fact that we were on the opposing camps during the cold war, bado inaendelea ku-affect mahusiano ya Tanzania na Kenya ktk miaka ya sasa.

..we need to find a way kuwa na mahusiano mazuri zaidi baina yetu, kwa faida ya wananchi wa pande zote.

cc Kabaridi, Ab-Titchaz, Jasusi
Uhusiano wetu na Kenya ni wa machale sana hasa ukichagizwa na tamaduni. Kenya wana aina ya superiority complex waliyokuwa nayo bila kujali kuwa ime expire katika zama hizi

Viongozi wamejaribu kurudisha mahusiano kama ulivyoshudia wakati wa uchaguzi uliopita akina Kenyatta na Odinga walikuwa hawaishi kukanyaga Dar es Salaam

Tena watu hawafahamu kuwa katika viongozi waliomtetea sana Uhuru JK ni mmoja, vinginevyo mataifa yalishaweka ngumu asigombee. Nadhani unakumbuka kila mwezi walikuwa Magogoni.
Hilo ndilo eneo la foreign policy pamoja na lile la kusuluhisha vita niyaonayo wamefanyakazi pamoja

Kwa upande mwingine mambo ya uchumi yanazidi kuwa magumu hasa baada ya vita ya pembe za ndovu Qatar na mradi wa bara bara wa Serengeti. Nakubaliana kabisa nawe kwa hilo, kwamba kunahitajika improvement

Kuna kitu kinaitwa Ukenya, kwa maana urafiki na mkenya lazima uwe na faida kwake baada ya hapo hakuna urafiki tena na hilo ndilo chanzo cha machale ya Tanzania.

Sasa hivi kuna triple K inayoendelea na EAC.
Kenya wanaangalia uchumi tu baada ya dili kukamilika utaona wanarejea Tanzania.

Watarejea TZ na kuwatosa wenzao kwasababu katika EAC sisi ndio wenye mpaka mkubwa, trade kubwa na Kenya na wao ni second investors katika TZ. Mfano, single entry visa na Kagame itamsaidiaje Mkenya! lakini akiwa na TZ ni dili. In short urafiki wa Kenya ni wa 'convinience'
 
Nguruvi3,

..lakini tulikuwa tunasafirisha silaha nzito za Uganda kupitia bandari ya Dsm.

..sasa ktk mazingira hayo kweli unafikiri we were working for peace, au??

..tukubali kwamba tulikosea.

cc Kabaridi
mkuu nikikumbuka vizuri silaha hizo zilipoingia kupitia dar, mapigano yaliyo kuwa yamepamba moto yalikuwa dhidi ya LRA ya joseph kony.
 
Last edited by a moderator:
PK hatokwepa mkono wa ICC kwasababu yote hayo yaliotokea Rwanda na DRC anahusika kabisa yeye jamaa yake Mu7 ndo maana wanang'ang'nia madarakani na kutaka kurithisha familia zao ili kujilinda! Kuna Ripoti Moja iliwahi kutolewa katika miaka ya 2000 na sehemu hivi na Mwanasheria mmoja wa Ufarasa akimtuhumu PK moja kwa moja kuhusika na mauaji ya Kimbari ya 1994. Na repoti ile ilipelekea kutokua na uhusiano mzuri kati ya Kigali na Paris!
 
Back
Top Bottom