JWTZ na taarifa ya Mabomu Gongo la Mboto

JWTZ na taarifa ya Mabomu Gongo la Mboto

Kwa kweli hakuna la maana hapa! Kumbe 2005 kuna mlipuko tena ulitokea hapohapo gongo la mboto!
 
Watanzania kwa ujumla wetu lazima tuanze kuwalazimisha viongozi wetu kujiuzuru kwa lazima. Hii si nchi ya CHADEMA, ni nchi ya watanzania. Waliokufa, kujeruhiwa na kupoteza makazi Niwatanzania. Pesa zitakazotumika kwa shughuli zote mpaka kulipa fidia Nizawatanzania.Lazima tuhoji, tupewe maelezo ya kutosha na kuwalazimisha wazembe wajiuzuru hata kwa lazima.

Hivi kama hatutawalazimisha viongozi hawa wazembe wajiuzuru kwa suala zito kama hili (tena limetokea mara mbili), ni suala gani ambalo litatusukuma kuwalazimisha hawa wazembe wawajibike. Wamelewa starehe na maisha ya juu kwa gharama ya kodi zetu mpaka hawajui wala kutekeleza wajibu wao.

Watanzania tuamke na tuache kulea upumbavu.
 


Hivi hawa jamaa walijiandaa kweli? Mbona vigugumizi vingi?
 
najua una hasira mkuu, ila ustaarabu jamvini ni bure huna hata haja ya kuulipia.

Kwa Kiswahili cha Kisasa sentensi inayosomeka "Kyabushaija and Tonge ni mashoga" maana yake ni marafiki wa karibu sana!

Sawa wanaJamvi?
 
Maswali kwa kweli ni mazuri sana laikini majibu....
 
Kwa vyovyote hii thread imepoteza mashiko kwani katika kurasa zote 7 hakuna kinachoonekana kueezwa zaidi ya mabandiko ya mwanzo ya Halisi. Nadhani mngeitendea hadhira fadhila kwa kuandika kilichojiri ili kiweze kujadilwa kuliko kujaza mambo yasiyokuwa ya muhimu, hasa kwa kutilia unyeti wa suala lenyewe
 
Ahaaa, anasema kwamba tukio hili na Gongo la Mboto siyo kama lile la Mbagala kwa hiyo wananchi hawajadanganywa kwamba ya mbagala hayatajirudia

Tume ya mbagala ilipendekeza kuweka makambi mbali na wananchi
 
JF nimewakubali.... yani in a few minutes mmeweza kurusha powerpoint slide muhimu.... hebu fungueni TV yaishe, tuachane na hizi TV feki dizaini ya TBC

huyo mjeshi mwenyewe anayekontroo laptop ni member wa JF!!!!!!!
 
Eti taarifa ya mbagala ilitolewa na ilihusu jeshi tu, haikuhusu wananchi!
 
suala la umeme kukatika haihusiki... anasema mabomu yanastahimili temperature kubwa

taarifa za tume yambagala ni ya jeshi sio ya wananchi
 
Kwa vyovyote hii thread imepoteza mashiko kwani katika kurasa zote 7 hakuna kinachoonekana kueezwa zaidi ya mabandiko ya mwanzo ya Halisi. Nadhani mngeitendea hadhira fadhila kwa kuandika kilichojiri ili kiweze kujadilwa kuliko kujaza mambo yasiyokuwa ya muhimu, hasa kwa kutilia unyeti wa suala lenyewe
Ni kwa sababu hakuna jambo la maana linalozungumzwa, maswali hayajibiwi inavyotakiwa, kifupi ni kama kijiwe fulani watu wanapiga stori.
 
Kumbe mabomu yenyewe yalikuwa mapya, je ni ya kichina au ufisadi ulipita hapo?
yatakuwa ya kichina, maana hii nchi kila kitu matatizo kwenye fedha za note fake kibao, za shilingi ukiziasha siku tatu zikiwa na unyevunyevu utakuta kutu kibao na zenye fake....ndiyo Tanzania zaidi ya uijuvyo....
 
yaani hapa ndo palikuwa pa kutokea.......pale uwanja wa uhuru si kuna watu pale.....ilitakiwa wote twende pale na hatutoki mpka jk ameomdoka madarakani.....vinginevyo hawa jamaa watatusumbua sana na sias za kishenzi na maneno ya jk ( machungu yenu ni machungu yangu)
 
Eti tukio la mbagala na gongo la mboto ni tofauti, sijamuelewa.
 
Eti waandishi wagoogle taarifa za nchi ambazo ajali kama hii imewahi kutokea.
 
Majibu ya Brigadia General Meela "Ni kweli waliahidi halitojirudia tena lakini walikuwa wanamaanisha kuwa halitotokea huko Mbagala" hakuna chumvi iliyoongezwa hapa
Kumbe hawawezi kujiuzulu kwani tatizo hili halikujitokeza Mbagala


NIMECHOKA
 
Back
Top Bottom