Tatu, Ngeleja, Werema na Pinda, wote hawa ni wanasheria na wanajua wanasema nini, achilia furahisha genge!
Nyambala, mikataba yote inatawaliwa na sheria ya mikataba, 'law of contract' hata ndoa ni mkataba. Ikishafungwa, hata kama ni illegal marriage, ni mahakama tuu ndio yenye mamlaka ya kutamka it is illegal, sio bunge, sio kamati ya bunge na sio mtu yoyote.Pasco pamoja na uelewa wangu mdogo wa sheria lakini nnakumbuka vizuri kipengele kinachosema hamuwezi kukubaliana kuvunja sheria. Hii maana yake nini? Nni kwamba mfano kima cha chini cha mshahara ni Tshs 90,000.00 Lakini mimi kwa shida zangu tukakubaliana na kusainishana kulipwa Tshs 50,000.00 Halafu say baada ya miaka 5 nikaibuka kukushtaki kunipunja mshahara hakuna mahakama itakayoamuru eti sina kesi kwa sababu tulisainishana. Kifupi ni kwamba mkataba wetu ulikuwa illegal.
Tuje kwenye Dowans, ukiisoma vizuri hoja ya Mwakyembe, objectively na bila ushabiki utagundua kwamba mkataba kati ya Tanesco na Dowans ulikuwa illegal, simply kwa sababu Dowans ni kampuni ya kitapeli na hilo lilithibitishwa na kamati ya bunge yeye akiwa mwenyekiti. Sasa sijaelewa hapo upopulist uko wapi. Please nieleweshe.
too little too late!Dr Mwakyembe atueleze yale yaliyofichwa na kamati yake ili kuiepushia aibu serikali!
Hakuna alininunuwa ila kama hatuna ukweli kwenye nyoyo zetu hatutoweza kuendelea kwa kujidanganya, lazima tuwe realists na kutazama ukweli uko wapi.
Kwa hili la Dowans ukweli ni kwamba, Dowans wamefanya kazi waliyokubaliana na Tanesco na piga uwa utawalipa tu, kama huwalipi, hutatuwi tatizo itazidisha. Hakuna kampuni duniani itaingia tena mkataba na wewe, kwani inajuwa itakuwa hailipwi. Na hiyo itashinikizwa na ICC, utakuwa kwenye cold list.
Ukiyajuwa hayo, utaona, bora ulipe kuliko kujitenegezea matatizo yatakayo kugharimu kuliko haya.
Sasa wanaopiga debe Dowans isilipwe ndio hao waliopiga debe mkataba uvunjwe. Matokeo ndio haya. Na kila mtapodhani kutolipa ni ushindi, mjuwe mnajidanganyan mnajiongezea matatizo.
And we dare say we are "great thinkers", mashudu.
Mag3, mikataba ni makubaliano huru baina ya watu wawili.Wana Jf, mimi si mwanasheria lakini hii hapa chini imekaakaaje ? Hakuna kifungu kinachoweza kutunasua ? Kwa nini hela yetu na jasho letu liwanufaishe hawa wezi, matapeli na mafisadi ?
Grounds for Refusal to Enforce Arbitral Awards
Generally, a court must comply with a request to enforce an arbitration award. The grounds upon which a court can refuse to enforce an award are very narrowly defined. Generally, there are seven grounds for refusal to enforce, which fall into two categories:
1. Problems with the conduct of the arbitration itself. The party against whom enforcement is sought must furnish proof that the award is flawed due to:a. Incapacity of a party;2. State sovereignty issues
b. Failure to give proper notice to a party, or the inability of a party to present his/her case;
c. The award fell outside the scope of the arbitration agreement;
d. The selection of the arbitrators violated the agreement; or, if the agreement did not address selection, the selection process violated the law; or
e. The award was set aside or annulled.
a. The law of the country in which enforcement is sought prohibits arbitration on the subject matter of the issue in dispute; or
b. The recognition or enforcement of the award would be contrary to the public policy of that country.
Je, katika kuilinda na kuitetea sovereignty yetu, Mahakama yetu haiwezi kuikomalia hiyo hukumu kwa misingi hii ?
Nyerere alishawahi kumwambia Rais Kabila Sr. usilipe madeni ya nje ya hovyohovyo kwa manufaa ya nchi yake ya Kongo. Hilo linashindikanaje hapa kwetu wakati aina ya mikataba ni ile ile? tena nafuu hata ile ya Kongo ilikuwa na kauwazi kidogo kuliko huu uliogubikwa na wizi wa dhahiri? Nadhani shida ni Uthubutu wa viongozi na pengine malipo hayo yanakwenda kwao wenyewe.
Nyambala, mikataba yote inatawaliwa na sheria ya mikataba, 'law of contract' hata ndoa ni mkataba. Ikishafungwa, hata kama ni illegal marriage, ni mahakama tuu ndio yenye mamlaka ya kutamka it is illegal, sio bunge, sio kamati ya bunge na sio mtu yoyote.
Baada ya kamati ya bunge kutambua kuwa richmond was illegal company, serikali ilipaswa kwenda mahakamani fasta na kuuvunja mkataba huku mahakama ikitangaza mkataba ule ni illegal. Kwa vile hakuna chochombo chochote kilichotangaza kuwa mkataba ule kuwa ni illegal,pamoja na illegality yake, umeendeleav kuwa legal mpaka leo tunapolipishwa!.
ICC pia imeponda hoja za usajili na legality ya richmond kwa sababu subject mater hapa sio nani ni nani, wala kampuni ipi imesajiliwa wapi, subject matter ni majereta ya kuzalisha umeme wa dharura, ni majereta ya ukweli na umeme wa ukweli. Msingi wa fidia ndipoo ulipolalia hapo!.
Suala hili limefanywa kisisas sana kulika kihalisia, serikali ilivunja mkataba wa kuilipa dowans capacity charge ya shilingi milioni 150 kwa siku, lakini tukakubali kuilipa IPTL shiling milioni 300 kwa siku na lita za mafuta laki 6 kwa siku!.
Si uliona shida na dhili tuliokuwa nayo wakati wa Nyerere kwa ubishi wake? Mwisho akasalimu amri, rejea LONRHO wakati wa Nyerere.
Pitia tena ujue nimeandika nini kabla kujibu. Una haraka sana katika kujaribu kutetea wizi huu wa mchana.Si uliona shida na dhili tuliokuwa nayo wakati wa Nyerere kwa ubishi wake? Mwisho akasalimu amri, rejea LONRHO wakati wa Nyerere.
Mkuu nadhani ulimaanisha wakilipwaDowans wasipolipwa naomba mwanasheria mkuu,waziri wa nishati na madini,katibu mkuu,amiri jeshi,rex attoney firm,msemaji wa ikulu ,wote wanapaswa kupelekwa mahakamani kwa kujaribu kuhujumu uchumi. Pia waache nafasi zao wazi ili waadilifu waongoze taifa! Narudia kama dowans wasipolipwa kwa kugundua wazi kuwa ni vibaka na matapeli,na hawa hapa tajwa juu ni wenzao,waende nao!
Mwizi ni yule aliyeletewa mali akakataa kuilipia na ICC wameliona hilo hakuna pa kukwepa.
Dowans wasipolipwa naomba mwanasheria mkuu,waziri wa nishati na madini,katibu mkuu,amiri jeshi,rex attoney firm,msemaji wa ikulu ,wote wanapaswa kupelekwa mahakamani kwa kujaribu kuhujumu uchumi. Pia waache nafasi zao wazi ili waadilifu waongoze taifa! Narudia kama dowans wasipolipwa kwa kugundua wazi kuwa ni vibaka na matapeli,na hawa hapa tajwa juu ni wenzao,waende nao!
we mtoto wa lowassa kwani ckujui,eti unajiita zomba,malizia zomba lowassa
Kwani Lonrho nayo ilikuwa kampuni ya kitapeli?