dogo kubwa
JF-Expert Member
- May 21, 2016
- 798
- 697
- Thread starter
- #21
Big up kiongoziAngalau wewe umeuliza. Inashangaza hadi sasa hivi kuna watu wengi sana ambao hawaamini kuwa mtu anaweza akatengeneza mkwanja kwa internet tu... Japokuwa stori na shuhuda ni nyingi ila bado watu wabishi.
YouTube ni njia moja wapo tu. Kama una kismati na ngekewa unatengeneza mamilioni ya pesa kabisa. Cha msingi ni content ambazo zitashika watu.
> Ilivyo ni kwamba, Google inalipa asilimia 68% za mapato yake ya matangazo kwa chaneli husika ambayo imesajiliwa kulipwa. Kwa hivyo kwa kila shilingi 100 za kitanzania, kwa mfano, Google inawalipa wamiliki wa content husika shilingi 68.
Hiyo ni kwa mujibu wa taarifa niliyoipata Google.
> kama YouTube channel inao uwezo wa kutengeneza hadi shilingi 41,500/= za kitanzania kwa view 1,000. Hiyo ni asilimia 100% ya mauzo. Je asilimia 68% ya hiyo 41,500/= ni shilingi ngapi? 41,500 × 68 ÷ 100 = 28,220. Hivyo kwa kila views elfu moja, mtu anatengeneza 28,220 za kibongo.
Turejee kwenye swali lako: Views milioni 1 ni sawa na shilingi ngapi? 1,000,000 × 28,220 ÷ 1,000 = 28, 220,000.
Sent using Jamii Forums mobile app