Jumuia ya wasio na ajira

wakuu itabidi tufanye mchakato wa kukutana , sasa tukutane wapi? na lini nadhani tutoe maoni ili tuone wapi tutakutana
 
Hili ni wazo au kichekesho? Nikiwa mwanachama wa jumuiya hii leo wakati sina kazi, vipi kesho nikipata ajira! Itakuwa jumuiya ya kwanza na ya aina yake. Wakati katibu na mwenyekiti wanaandaa mkakati fulani, unakuta katibu kapata kazi kwa hiyo mipango yoote inabidi ianze upya, tehe tehe tehe!
 
Wakuu nimeshapata sms nyingi ila watu wengi wanashauri kikao cha kwanza kifanyike jumamosi ijayo, nadhani nadhani ni wakati wa kukusanya mawazo, tungependa kupata mawazo mapya kwa maslahi ya kujenga taifa letu na kuboresha au kutatua matatizo yanaowakuta wasio na ajira
 
Nadhani ni wakati wa serikali kutoa elimu kwa vijana juu ya ujasiliamali

Kila kitu lawama kwa serikali, hivi huu muda wanaokaa kwenye internet si wangeutumia kusoma 'enterpreneurial skills'? siku elimu ni kama bure labda kama unataka vyeti ndio inabidi uende chuo lakini kama unajua kusoma na kuandika kuna fursa nyingi sana za kujielimisha. Sasa mtu kutwa anashinda kusoma magazeti ya udaku halafu unadai serikali ikuelimishe, tena wengine wana elimu ya chuo kikuu ambayo siku hizi pamoja na mambo mengine wanafundisha pia somo la enterpreneurship.
 
Kila kitu lawama kwa serikali, hivi huu muda wanaokaa kwenye internet si wangeutumia kusoma 'enterpreneurial skills'? siku elimu ni kama bure labda kama unataka vyeti ndio inabidi uende chuo lakini kama unajua kusoma na kuandika kuna fursa nyingi sana za kujielimisha. Sasa mtu kutwa anashinda kusoma magazeti ya udaku halafu unadai serikali ikuelimishe, tena wengine wana elimu ya chuo kikuu ambayo siku hizi pamoja na mambo mengine wanafundisha pia somo la enterpreneurship.
ni wajibu wa serikali ndio maana watu wanalipa kodi, pia kuelimisha vijana ni bora kuliko unavyodhani , katika wasio na ajira wanatofautiana malengo na kiwango cha mahitaji, kuna mwingine hana ajira lakini ni mtu mwenye ngazi ya elimu ya juu na mwingine Hana ajira na pia ajui kusoma wala kuandika, hivyo unavyoliangalia tatizo ili lazima uliangalie kwa undani
 
Hili ni wazo au kichekesho? Nikiwa mwanachama wa jumuiya hii leo wakati sina kazi, vipi kesho nikipata ajira! Itakuwa jumuiya ya kwanza na ya aina yake. Wakati katibu na mwenyekiti wanaandaa mkakati fulani, unakuta katibu kapata kazi kwa hiyo mipango yoote inabidi ianze upya, tehe tehe tehe!

kuna kitu lazima ukitambue kazi ya taasisi hii ni ya kisera zaidi , kwani kazi yake ni kuweka mazingira mara ya watu kuweza kukabiliana na tatizo la ajira. na kwa mfumo wake itakuwa na bodi ambayo wajumbe wake watatoka sehemu mabali mabali , kwa ufupi mchanganuo wa mfumo wa bodi hii

1. Kutoka katika kundi la wasio na ajira

2. muwakilishi kutoka bungeni

3.muwakilishi kutoka katika wizara ya ajira/utumishi

4.Wawakilishi katika vyama vyote vya siasa

5.muwakilishi kutoka taasisi ya msajili wa kampuni na biashara

6.muwakilishi kutoka makampuni mbali mbali


LENGO LA JUMUIA HII

1. Kusaidia vijana kutuma maombi ya ajira kwenda sehemu mabali mbali

2. kutafuta ajira na fulsa za kibiashara sehemu mbali mbali na kuziweka wazi kwa wasio na ajira

3.Kuwasiliana na serikali hili kutoa usajili na utoaji wa leseni za kibiashara kwa wasio na ajira kwa gharama ndogo au bure kabisa

4.kuwawezesha vijana walio katika biashara ndogo ndogo kutambulika na kuweza kukopesheka

5.Kutafuta mitaji kutoka katika taasisi mbali mbali ikiwemo kujaribu kushauri makampuni makubwa ya madini, mabenki na makampuni ya simu kuchangia angalau 1% ya faida kama ruzuku kwa vijana wasio na ajira

5. kusimamia ajira za umma kutotolewa kwa upendeleo au rushwa
 
cna ajira naunga mkono ajira weyeeeeeeeeeeeeeeee!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
kwa maoni ya nini kifanyike kuhusu wasio na ajira tuma sms kwenda namba 0752798074, pia muundo wa jumuia hii na namna ya uendeshwaji wake
 
wakuu jumamosi ijayo kikao wamependekeza kifanyike biafra kinondoni

Ingawa sijui ni jumamosi ya tarehe gani!!

Binafsi nadhani kuna mambo yamsingi yanatakiwa kufanyiwa kazi na kuwekwa sawa kabla ya mkutano huo.

Kwanza, ilitakiwa kuwasiliana na taasisi hizo ulizozitaja zitakazo husishwa na uundwaji wa bodi hiyo juu ya jumuia hiyo na malengo yake. Hii itasaidia kujua kama hakuna jumuia au taasisi inayofanya kazi zinafanana na hizo ambazo jumuhia hii mpya inataka kufanya(Kupunguza duplication ya jumuia/taasisi).

Pili , Ajenda za mkutano hazipo wazi, hajulikani nini kitazungumzwa huko mkutanoni ili washiriki waweze kuandaa hoja za msingi vinginevyo mkutano huo utakuwa kama "kijiwe" cha watu wasio na ajira jambo ambalo nadhani hukusudii liwe.
 
Ingawa sijui ni jumamosi ya tarehe gani!!

Binafsi nadhani kuna mambo yamsingi yanatakiwa kufanyiwa kazi na kuwekwa sawa kabla ya mkutano huo.

Kwanza, ilitakiwa kuwasiliana na taasisi hizo ulizozitaja zitakazo husishwa na uundwaji wa bodi hiyo juu ya jumuia hiyo na malengo yake. Hii itasaidia kujua kama hakuna jumuia au taasisi inayofanya kazi zinafanana na hizo ambazo jumuhia hii mpya inataka kufanya(Kupunguza duplication ya jumuia/taasisi).

Pili , Ajenda za mkutano hazipo wazi, hajulikani nini kitazungumzwa huko mkutanoni ili washiriki waweze kuandaa hoja za msingi vinginevyo mkutano huo utakuwa kama "kijiwe" cha watu wasio na ajira jambo ambalo nadhani hukusudii liwe.


nadhani ajenda kuu ziwe malengo ya jumuia na kadri majadiliano yatavyoendelea ndio kuingia kwa undani na maamuzi yafikiwe kidemokrasia kwa wanachama kuchagua kitu cha kufanya
 
Mawazo mazuri ni mengi sana na mchakato unaendelea vizuri na wajumbe ni wengi na inatia moyo jinsi umoja huu utavyokuwa na nguvu na ushawishi mkubwa kwenye taifa letu
 
Back
Top Bottom