Julieth Robert (ITV) Ulikosa Khanga msibani?

Julieth Robert (ITV) Ulikosa Khanga msibani?

Kwenye taarifa ya habari ya ITV,reporter wao wa kike ameonekana akiwa amevaa suruali tena ya kubana kwenye kuriport kuwasili kwa mwili wa marehemu Samuel sitta pale JNA.
Haya si maadili yetu, kwa mwanamke wa kitanzania, kuonekana amevaa suruali pekee kwenye misiba pasipo kuvaa angalau mtandio.Hebu nyie waandishi wa kisasa zingatieni pia maadili ya mila na tamaduni zetu.

Ukiona hata kwenye vyombo vya habari hakuna maadili ujue nchi imekwisha kimaadili.
 
Mlete uzi acha hizo.
Mama yako mzazi mara ya mwisho umenunulia lini khanga?
kwani khanga ina maana gani kwako?
kwetu kina mama wanavaa khanga kwenye harusi tu!
 
Ahsante NDESSA, nadhani mlete mada atakua ameelewa
Mleta mada umeksa kitu cha kukosoa, JNIA sio msibani lakini kubwa zaidi pale mwandishi yuko kazini tofauti na watu wengine ni sawa na kusema na askari wa kike aende pale na khanga, kwa mazingira ya kuchukua habari kwenye msongamano wa watu lazima avae nguo itakayomfanya awe flexible kutimiza majukumu yake kukimbia huku na huko kupata habari, sio aanze kushikilia kanga zinapodondoka.
 
Ni kweli kuvaa hata vyombo vya habari vinavyoheshika kama CNN BBC, DW etc huwezi kuona aliyekosa maadili kama huyu. hata kama sio sehemu ya msiba ndiyo kuonyesha nanii yake pale? Hapana. ITV angalieni maadili ya Maripota wenu. NB: Kuna reporter mmoja anaripoti habari kutoka mkoa wa mara sijui wa ITV au Star Tv anaboa sana anaweza akatangaza habari nzuri sana lakini anapomalizia anaweka mbwembwe mpaka ninadhani labda hana akili vizuri. Samahani lakini kwa mtazamo wangu tu kwake.
 
Kwenye taarifa ya habari ya ITV,reporter wao wa kike ameonekana akiwa amevaa suruali tena ya kubana kwenye kuriport kuwasili kwa mwili wa marehemu Samuel sitta pale JNA.
Haya si maadili yetu, kwa mwanamke wa kitanzania, kuonekana amevaa suruali pekee kwenye misiba pasipo kuvaa angalau mtandio.Hebu nyie waandishi wa kisasa zingatieni pia maadili ya mila na tamaduni zetu.
Alienda kikazi au alienda kuombokeza...... Kama ni hivyo mbona mkapa hakulia wala hata kutoa mchozi kidogo
 
Ni sheria gani inayosema uvae khanga msibani? usitake kila mtu aamini unachoamini.... usitake kila mtu awe na tamaduni zako..... usitake kila mtu aamini mafundisho ya dini yako.. Tanzania is multicultural state kila mtu ni sovereign kwa kila anachokiamini ilimradi asivunje sheria. Dont make your believe to be supreme over others .
Hv kuvaa vimini na suruali za kubana huko upande wako ruksa?
 
Pale airport sidhani kama kulikuwa na tatizo
 
Wengi watakukosoa lakini huo ndio ukweli...mavazi lazima yaendane na tukio na mahali ulipo
 
Naskia kipindi hicho ukimuongea Mwl Nyerere kwa ubaya hata kama upo ndani na mke wako unamuongea kwa ubaya kesho yake asubuhi wazee wapo mlangoni kwako ni kweli mkuu
TISS ilikuwa ina maajenti hadi wavuta ugoro na wanywa mataputapu. Halafu kila kijiji alikuwepo bila kufahamika. Ndiyo maana aliweza kuwaadabisha wapinzani wake kwa kuwatupa uhamishoni nyumbani kwao wasitoke. Na walipokiuka maramoja walifahamika. Hilo la kunong'ona na mkeo halafu kesho unafuatwa yawezekana kukawa na ukweli, maana huyo unayemuita wewe mkeo yaweza kuwa ni ajenti mwenyewe.
 
MTOA MADA WASIO ELEWA ETHICS ZA TAALUMU YA UANDISHI WA HABARI WNAKUPINGA,LAKINI KUSEMA UKWELI YULE DADA ALIROCHA KUPITA MAELEZO
Kurocha ndiyo kufanyaje? Inamaana sikuhizi hata kikurya kinatumika humu jf?
 
ACHA WIVU, hutaki mashemeji nasisi tuone???
 
kuna tofauti kubwa kati ya kazin na msibani, nguo maalum ya msibani ni nyeusi hajalishi umevaa suruali au T-shirt
 
Back
Top Bottom