Juliana Shonza ni hatari kuliko tunavyodhani

Juliana Shonza ni hatari kuliko tunavyodhani

unahangaika na mke uliyemfukuza?mbaya yule anayeanza kukukimbia CDM ina kila sababu ya kupuuza makapi haya
 
Ni tahadhari maana hata mbuyu ulianza kama mchicha.

.......

Umevutiwa na nini hasa rafiki? huo mkorogo au hiyo jeans? mwambie avae dira na aache mkorogo kama utamwita tena mzuri. kwa kulinganisha na warembo mi namwona wa kawaida mno, sura ya kichina zaidi
.
 
Shonza ni Zaidi ya ZZK na CHACHA WANGWE...ameisoma CHADEMA vizuri na kutoa report how to kill this party !
 
Juliana kazi yake inaanza wakati wa kampeni kuna maneno mengi yapo kwa ajili ya Dr Slaa mambo aliyokuwa anataka kuanyiwa Dr Slaa na Mbowe pamoja na Lema ikifika muda wake atafunguka.

Pekundu ni kikwere ama ni kinyaturu?
 
Juliana Shonza....ameamua kujiua kisiasa kutoka na njaa zake na tamaa za madaraka hakika hawezi kufika popote yaani hana tofauti na wapumbavu wa mitaani wanaosoma matangazo ya waganga wa kienyeji..eti tunakupa utajiri, akili darasani....mafanikio siku 3 na yeye ndio amejiunga na hilo kundi la wajinga.... Ngoja tumuone ataweza? Maana nakumbuka moto wa Kafulila na Nakaaya Sumari ulivyozimika......
 
hakuna anyemfahamu Juliana, she is not popular and was never popular

hata ndani ya chadema alipata chance kwasababu chama kilikua bado kwenye kukua, there were few good people in there

Amini nakuambia, Juliana hata akisimama kariakoo sokoni au pale ferry hakuna atakayemtambua wala kupoteza muda kumsikiliza

anahitaji safari aweze kupata pesa ya kula, na baadhi ya waratibu wa hizo safari wanataka wawe wa kwanza kula kiporo kipya... unajua uhusiano uliopo kati ya hizo safari na masuala ya ngono
 
Sina uhakika na mleta mada kama alifanya vizuri tathimini zake kwa maana CHADEMA ni taasisi na si mtu mmoja mmoja hivyo kwa binti shombo kuiathiri CHADEMA hapo nadhani hujapafanyia kazi vizuri kwa maana kwangu nazan yahitajika NEC na CC kwa pamoja wakeshe na kuomba wakiongozwa na mtoto wa mtabiri ili wazigeuza akili za Watanzania ila kwa huyu binti bado sana hana hadhii hiyo.
 
Hana lolote huyu dada CHADEMA ni chama makini cha watu makini mi naona hata ku comment hata tunampa tu misifa isiyofaa!! kuna dhana moja ya kifalsafa kuwa ukuwa nae ambatana nae usipokua nae msahau!! agghhh! hasira tu
 
Nakubaliana na Makamanda wengi kuwa huyu dada anaweza kuwa kafa kisiasa kwa ajili ya usaliti, LAKINI, angalia penye red.Kuna uwezekano Magamba wakampa resouces, kitu ambacho ni hatari. Pili, atatumia jinsia yake kueneza SUMU, yeye kama mwanamke kisaikolojia ataingiza huruma kwa watu, na watu wasio jua kupembua mambo watamuamini kufuata hisia zao kuliko akili. HII NI HATARI. Hili sio lakupuuzia. Lazima tupange counter attack.
1. Safari ya Juliana kuzunguka Tanzania nzima kueneza sumu dhidi ya chadema ndio imeanza.
2. Juliana ni hatari kuliko Mwigulu na Nape.
3. Juliana ana hasira za kweli (japo ni kwa upuuzi wake) juu ya cdm na viongozi wake.
4. Juliana atakachoomba toka ccm kwa ajili ya kuikandamiza cdm atapewa. Kumbuka huyu ni Delila.
5. Watu watavutika kumsikiliza huyu binti kwa kuwa ni mwanamke na ana mvuto. Atajenga huruma kwa wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
6. Kwa bahati mbaya kila atakachosema sasa na baadaye kitakuwa habari, hivyo athari yake si ndogo.
 
Raia Fulani umeweka angalizo la maana sana kwa CHADEMA.
Lakini tangu wameruhusu kuwakilishwa na vijana wa Lumumba ambao wamejivika koti la mashabiki wa CHADEMA, basi lazima hii hoja ionekane kituko.

Huyu binti Shonza amekuwa anatumika hata kabla ya kuibukia CHADEMA, ni miongoni mwa makada wengi wa CCM ambao wametumwa upinzani kuvuruga huko ili kuipa nafasi CCM inayotweta kutawala.

Dhambi kubwa kwa CCM ni kuhaini maamuzi ya Watanzania 2010 waliofanya maamuzi kwenye sanduku la Kura, na sasa wanachokifanya ni kuua dhana ya upinzani nchini ndo maana usione ajabu kwa akina Apson kujiingiza kwenye siasa za chama tawala wakati katiba imewakataza.

Tufike mahala tukubali kuufumua mfumo mzima na tuanze upya. Siyo hasara kuanza upya kwa sababu hivi tunavyoendelea ni wazi shimo la kuangukia lipo karibu mno.
 
Last edited by a moderator:
Hatari? Condom ikishatumika inafaa nini? Hizo ni condom za CCM
 
Huyu ni binti mwenye tamaa sana,alivyohama ghafla sikushangaa.
 
Wakuu nimekuwa nikifuatilia mtiririko wa matukio tangu kuibuliwa kwa hoja ya masalia hadi kufukuzwa na hatimaye kufikia hatua ya kuhamia chama tawala baadhi ya masalia akiwepo Juliana na Mwampamba. Kuibuka kwa ile hoja ni jambo ambalo japo lilijadiliwa sana, chanzo chake ni tata. Waliohamia CCM ni wawili; Juliana na Mtela lakini anayesikika zaidi ni huyu dada. Awali alisema yeye bado ni BAVICHA na hautambui utenguzi uliofanyika. Mara tukasikia yuko CCM na kapokelewa na Rais! Akiwa yeye na mwenzake. Mara anatoa kauli kuwa yeye ni mzawa wa Ubungo na yuko tayari kupambana na Mnyika.

Niseme tu kwamba kazi aliyotumwa sio kwamba ameikamilisha. Ndio kwanza inaanza. Huyu ni Delila. Ni mzuri wa sura na umbo lakini ana akili ya nyoka. CHADEMA itambue yafuatayo;
1. Safari ya Juliana kuzunguka Tanzania nzima kueneza sumu dhidi ya chadema ndio imeanza.
2. Juliana ni hatari kuliko Mwigulu na Nape.
3. Juliana ana hasira za kweli (japo ni kwa upuuzi wake) juu ya CHADEMA na viongozi wake.
4. Juliana atakachoomba toka CCM kwa ajili ya kuikandamiza cdm atapewa. Kumbuka huyu ni Delila.
5. Watu watavutika kumsikiliza huyu binti kwa kuwa ni mwanamke na ana mvuto. Atajenga huruma kwa wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
6. Kwa bahati mbaya kila atakachosema sasa na baadaye kitakuwa habari, hivyo athari yake si ndogo.

CHADEMA watambue sasa kuwa hawajaondoa tatizo bali wamezaa tatizo. Wamezaa si kwa kosa lao bali wakati mwingine inatokea tu. Wajipange katika kudhibiti athari zitakazotokana na kauli za huyu msichana. Historia isijeandikwa kupitia sumu ya huyu mtoto na kamwe asipuuzwe. Harakati zake kipindi cha masalia na PM7 dhidi ya CHADEMA zinajulikana, nazo zilikuwa za faragha na ziliathiri chama. Sasa hizi za hadharani nazo zikipuuzwa si balaa?

hakuna lolote.GANDA LA MUA LA JANA.........
 
Mi naona mnamkuza bure tu huyu, kama yeye ni mzawa wa Ubungo, wenzie sisi sio tu wazawa, bali ni waasisi wa Ubungo, yeye ameikuta kwasababu labda kazaliwa hapa lakini yeye si zaidi ya sisi tulioiasisi ubungo. Yeye kakuta ubungo tayari kumeshajengwa barabara nne, sie enzi zile huku ubungo ni mashamba tu ya mikoroshi, huko kimara ilikuwa ni pori tu. walokuwa wanathubutu kufika Kimara walikuwa wanaishia kunyonywa damu na mumiani, sasa huyo dada asitubabaishe na uzawa wake. Atueleze kwa uzawa wake amechangia nini katika maendeleo ya Ubungo?? Aache kubwabwaja. Halafu na sie naona tunakuwa wajinga kama yeye kwasababu tunam[andisha sana chati kwa kumjadili. Tumuache aende kwa amani kwa magamba wenzake huko ndo kunamfaa. Buriani Dada Shombo

Hii hoja ya uzawa haina uzito...red indians ni wazawa marekani lakini politically wako marginalised...wazaramo ni wazawa ukanda wa mashariki lakini politically wako marginalized....issue ni agenda gani unazo na mikakati ipi unaitumia..Shonza kwa "uzawa" wake Ubungo for that matter hana madhara yoyote kwa Mnyika na Chadema kwa ujumla.

Sent from my BlackBerry 9800 using JamiiForums
 
Nilitegemea kuwa ueleze kuwa hatokuwa na jipya badala yake unatuaminisha kuwa tumchunge ni hatari. Uatari wake ukiisha pindi alivyobainika kuwa ni msaliti. Dr slaa alisema hawez ongelea upuuz wa hili kundi.uzuri wake wa sura na utendaji kazi siuoni. Angekuwa mzuri siri zikavuja? Ni mganga njaa,ata ccm hawajampa kitu isipokuwa kumbukumbu ya kupga picha na rais basi
 
Tatizo mkuu SHONZA anajulikana tu humu JF na kwenye baadhi ya watu walio wafuatiliji wazuri wa siasa....Inabidi kwanza kujitambulisha yeye ni nani katika kupambana kwake na CDM...

Pili mitaani unapoipondea CHADEMA na DR SLAA believe me wananchi hawakuelewi...Ana kazi kubwa sana ya kufanya hili....

Tatu watanzania wameshaichoka CCM..hata akifufuka NYERERE leo na kuanza kuipigia chepuo CCM itabidi afanye kazi ya ziada...

Mwache akadhalilishwe kwa kuzomewa.
 
Back
Top Bottom