Juliana Shonza ni hatari kuliko tunavyodhani

Juliana Shonza ni hatari kuliko tunavyodhani

Tusihadaike sana na kauli kuwa hana madhara. Dk Slaa mwenyewe alijua madhara yake ndio maana akawa anamzuia kuhudhuria mikutano ya uenezi mikoani. Hata alipohudhuria hakupewa nafasi ya kuzungumza. Katika siasa za kujihami kamwe huwezi kusema eti .nimezidiwa maarifa'. Hilo halipo. Kadhalika asingekuwa na madhara asingeondolewa bavicha.
 
Nani alikuwa anamjua Ally Bananga kabla ya kuhamia CHadema?

tuuchukulie kwa taadhari ushauri uliotolewa.
 
Juliana hana madhara kwa CDM...Uwezo wake ni mdogo sana, wanachokifanya CCM ni kujaribu kuwaamninisha Umma wa Watanzania kuwa wamefanikiwa kuwapata viongozi wa CDM wakati ukweli unajulikana kuwa MOLES wao wamerudi nyumbani baada ya kushindwa kazi...
Viashiria ni vingi sana kuwa huu ndo mwisho wa Juliana, sana sana watamkilimbita kwa kupokezana kama mpira wa kona, akija kushtuka tayari virusi vinene kama mbege vitakuwa vinapishana kwenye mwili wake..
 
Awe mwangalifu asije akapigwa mawe bure! Sasa hivi wananchi wengi hata vijijini hawataki kusikia kitu kinaitwa CCM.
 
Hajawahi kuwa na madhara na kamwe hatakuwa na madhara kwa CHADEMA. Kama angekuwa na madhara hata kumfukuza kwake ingekuwa taabu. Amefukuzwa kama majani yaliyokauka yanavyoondolewa kwenye uwanja uwe safi. Heche pekee amemudu kumtoa hata bila ya Baraza Kuu la chama wala viongozi wakuu wa chama, halafu huyo naye ndiye awe na madhara kwa chama? Ana siku chache sana mpaka atakapofutika kabisa kwenye siasa za Tanzania. Hata kusikika kwake kuwa yupo, imekuwa ni baada ya kufukuzwa. Hawasogelei hata kwa mbali akina Lamwai wala akina Kabourou, lakini wametoweka sembuse kinda huyu? Mbona mnataka kuwatisha watu wazima kwa kutumia kiwavi mkitaka kuwaaminisha watu kuwa ni koboko?

kuwepo na kutokuwepo kwake chadema naona sawa tu. huu mwezi ukiisha naye ataisha yaani ndo mwisho wa kumsikia. mia
 
Juliana shoza hana hatari yoyote mwanamke kaolewa hata eda hajakaa utasema mwanamke huyo???wako wapi kina tambwe hizza,akwilombe,kaborouru?????
 
Tatizo mkuu SHONZA anajulikana tu humu JF na kwenye baadhi ya watu walio wafuatiliji wazuri wa siasa....Inabidi kwanza kujitambulisha yeye ni nani katika kupambana kwake na CDM...

Pili mitaani unapoipondea CHADEMA na DR SLAA believe me wananchi hawakuelewi...Ana kazi kubwa sana ya kufanya hili....

Tatu watanzania wameshaichoka CCM..hata akifufuka NYERERE leo na kuanza kuipigia chepuo CCM itabidi afanye kazi ya ziada...
nyerere akifufuka akaipigia debe ccm akaruhusu watu wamuulize maswali kumi tu kuhusiana na uchafu wa ccm atakufa tena muda huo huo bila kujibu hata moja .big up
 
Wakuu nimekuwa nikifuatilia mtiririko wa matukio tangu kuibuliwa kwa hoja ya masalia hadi kufukuzwa na hatimaye kufikia hatua ya kuhamia chama tawala baadhi ya masalia akiwepo Juliana na Mwampamba. Kuibuka kwa ile hoja ni jambo ambalo japo lilijadiliwa sana, chanzo chake ni tata. Waliohamia CCM ni wawili; Juliana na Mtela lakini anayesikika zaidi ni huyu dada. Awali alisema yeye bado ni BAVICHA na hautambui utenguzi uliofanyika. Mara tukasikia yuko CCM na kapokelewa na Rais! Akiwa yeye na mwenzake. Mara anatoa kauli kuwa yeye ni mzawa wa Ubungo na yuko tayari kupambana na Mnyika.

Niseme tu kwamba kazi aliyotumwa sio kwamba ameikamilisha. Ndio kwanza inaanza. Huyu ni Delila. Ni mzuri wa sura na umbo lakini ana akili ya nyoka. CHADEMA itambue yafuatayo;
1. Safari ya Juliana kuzunguka Tanzania nzima kueneza sumu dhidi ya chadema ndio imeanza.
2. Juliana ni hatari kuliko Mwigulu na Nape.
3. Juliana ana hasira za kweli (japo ni kwa upuuzi wake) juu ya CHADEMA na viongozi wake.
4. Juliana atakachoomba toka CCM kwa ajili ya kuikandamiza cdm atapewa. Kumbuka huyu ni Delila.
5. Watu watavutika kumsikiliza huyu binti kwa kuwa ni mwanamke na ana mvuto. Atajenga huruma kwa wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
6. Kwa bahati mbaya kila atakachosema sasa na baadaye kitakuwa habari, hivyo athari yake si ndogo.

CHADEMA watambue sasa kuwa hawajaondoa tatizo bali wamezaa tatizo. Wamezaa si kwa kosa lao bali wakati mwingine inatokea tu. Wajipange katika kudhibiti athari zitakazotokana na kauli za huyu msichana. Historia isijeandikwa kupitia sumu ya huyu mtoto na kamwe asipuuzwe. Harakati zake kipindi cha masalia na PM7 dhidi ya CHADEMA zinajulikana, nazo zilikuwa za faragha na ziliathiri chama. Sasa hizi za hadharani nazo zikipuuzwa si balaa?

huyu mkuu usimpe kichwa hana lolote mimi binafsi namfananisha na TAMBWE HIZA, ni mlropokaji hana effect yoyote hakuna mtu anayemwongelea SHONZA zaidi ya yeye mwenyewe kujipostia habari na kujitafutia umaarufu. Mtu yeyote hatari huwa siyo mropokaji, Mtu yeyote Mropokaji watu wakishamzoea wanamuona shonza kama Tahira. Na Mtu yeyote anayemuona Juliana Shonza ni hatari , hata yeye ananipa wakati mgumu kuhusu uwezo wake wa kuangalia mambo na kufikiri yaani Naona kama uwezo wakwe wa kufikiria ni mdogo sana. Juliana Shonza she is just a lunartic ( some one who went grazy with every phase of the moon). Tuache kumjadili huyu lunartic hana effect yoyote kwenye chama .
 
Niliwahi kuandika kuwa baadhi ya makada wa cdm hususani masalia(pm7) wangehamia ccm nikiwataja mtela mwampamba ,juliana shonza na habibu mchange kuwa ni sehemu ya waliojipanga kama sio kupangwa kuhamia ccm baada ya mpango wa kuihujumu cdm wakiwa ndani kushindikana.muda haukupita kabla ya wawili kati ya watatu niliowataja kuhamia ccm na kama kawaida yao kutoa matusi kwa viongozi na chama kwa ujumla.kundi la masalia ni kubwa na haliundwi na hao wawili walioondoka.ni wengi na wengine kama mchange bado wapo ndani ya cdm.swali la kujiuliza hapa ni je,nani atawafata mwampamba na shonza ccm?
 
Umetumwa wewe unazunguka zunguka tu huna points izo propaganda zako za kutaka kumfanya ni mtu hatari wakati hana lolote kamwambie mumeo chumbani.
 
Wakuu nimekuwa nikifuatilia mtiririko wa matukio tangu kuibuliwa kwa hoja ya masalia hadi kufukuzwa na hatimaye kufikia hatua ya kuhamia chama tawala baadhi ya masalia akiwepo Juliana na Mwampamba. Kuibuka kwa ile hoja ni jambo ambalo japo lilijadiliwa sana, chanzo chake ni tata. Waliohamia CCM ni wawili; Juliana na Mtela lakini anayesikika zaidi ni huyu dada. Awali alisema yeye bado ni BAVICHA na hautambui utenguzi uliofanyika. Mara tukasikia yuko CCM na kapokelewa na Rais! Akiwa yeye na mwenzake. Mara anatoa kauli kuwa yeye ni mzawa wa Ubungo na yuko tayari kupambana na Mnyika.

Niseme tu kwamba kazi aliyotumwa sio kwamba ameikamilisha. Ndio kwanza inaanza. Huyu ni Delila. Ni mzuri wa sura na umbo lakini ana akili ya nyoka. CHADEMA itambue yafuatayo;
1. Safari ya Juliana kuzunguka Tanzania nzima kueneza sumu dhidi ya chadema ndio imeanza.
2. Juliana ni hatari kuliko Mwigulu na Nape.
3. Juliana ana hasira za kweli (japo ni kwa upuuzi wake) juu ya CHADEMA na viongozi wake.
4. Juliana atakachoomba toka CCM kwa ajili ya kuikandamiza cdm atapewa. Kumbuka huyu ni Delila.
5. Watu watavutika kumsikiliza huyu binti kwa kuwa ni mwanamke na ana mvuto. Atajenga huruma kwa wavivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau.
6. Kwa bahati mbaya kila atakachosema sasa na baadaye kitakuwa habari, hivyo athari yake si ndogo.

CHADEMA watambue sasa kuwa hawajaondoa tatizo bali wamezaa tatizo. Wamezaa si kwa kosa lao bali wakati mwingine inatokea tu. Wajipange katika kudhibiti athari zitakazotokana na kauli za huyu msichana. Historia isijeandikwa kupitia sumu ya huyu mtoto na kamwe asipuuzwe. Harakati zake kipindi cha masalia na PM7 dhidi ya CHADEMA zinajulikana, nazo zilikuwa za faragha na ziliathiri chama. Sasa hizi za hadharani nazo zikipuuzwa si balaa?

Hana mvuto wowote zaid ya kalolait anayotumia., hakuna atakaye sikiliza upuuzi wake hasa kwa chama anachotembelea!
 
Mkuu RF,tambua kwamba hata huko ccm kuna watu hawafurai ujio wake,wanaona kama vile watawekwa benchi na yeye kupewa kipaumbele.so atakuwa anapambana na internal na external forces.kwa mtazamo wangu huyu binti kajimaliza kisiasa.
 
ukijisikia kubofya batani basi ndio unabofya mpaka zinafutika kwa utumbo huu?....uwoga wako na saikolojia yako peleka huko watu hatuambiwi kitu kuhusu chadema acha aende zake sio mda atafuatwa na baba yake shibuda.........
 
Tusihadaike sana na kauli kuwa hana madhara. Dk Slaa mwenyewe alijua madhara yake ndio maana akawa anamzuia kuhudhuria mikutano ya uenezi mikoani. Hata alipohudhuria hakupewa nafasi ya kuzungumza. Katika siasa za kujihami kamwe huwezi kusema eti .nimezidiwa maarifa'. Hilo halipo. Kadhalika asingekuwa na madhara asingeondolewa bavicha.

Dr.slaa alikuwa anajua uwezo mdogo wa huyu binti hence alikuwa anaona kama atakiahaibisha chama wakisikia maneno ya huyu binti,ya uropokaji . wakati watu wanajua kwamba chadema kina watu makini wenye uwezo mkubwa wa kufikiria na kuchambua mambo. hence akaamua kumzuia abaki akifanya kazi za ofisini.
 
Nashangazwa na harakati na matusi yanayoendelezwa dhidi ya huyu mwana dada shupavu juliana shonza kisa kutoka chadema na kujiunga ccm. Alikiri mbele ya sekretariati ya ccm kuwa aliipenda chadema kwa dhati lakini amenyanyaswa na kufikiria mara mbili kuendelea kubaki chadema. Akasema yeye bado ni kijana na anaipenda nchi yake na anapenda siasa akafikiria njia nyinginr ya kuwasaidia watanzania kisiasa akaona ccm ndiyo chama kinachoweza kuishi na watu wa namna zote bila kujali tofauti. Sasa kumwita delila nyoka msaliti nadhani ni kufika mbali. Hata kama atazunguka nchi nzima si mpingane naye kwa hoja?? Sioni haja ya hofu. Nadhani katika makala yangu mjoa niliandika hapa kuhusu msimamo wa baadhi ya wasomi wanaomfahamu huyu msichana nao walishangaa chadema kukosa uvumilivu na kumfukuza mtu mwenye uwezo na ushawishi kama juliana. Nadhani wengi wanasema chadema imetupa almasi. Kweli ana iq ya hali ya juu nadhani ilibidi apewe muda wa kusikilizwa kuliko kufukuzwa. Kama chadema ilimfukuza imuache aangalie ustaarabu kwa wengine. Kama atapanda jukwaani kuisema chadema basi inabidi ajibiwe kwa hoja na si kutukanwa kama wengi wa wachangiaji wanavyofanya. Kwanza hiyo inaonesha kuwa bado chadema wanampenda lakini zaidi ni kama wanataka kumwaribia huko alikokwenda asifanikiwe. Labda hili ni onyo kwa chama kuwa na uvumilivu.
 
Huyo Juliana ndio nani? ndo kwanza namsikia tu! na kama simtambui basi hana lolote na CDM!aende wakazikwe tu! RPI CCM
 
Tatizo mkuu SHONZA anajulikana tu humu JF na kwenye baadhi ya watu walio wafuatiliji wazuri wa siasa....Inabidi kwanza kujitambulisha yeye ni nani katika kupambana kwake na CDM...

Pili mitaani unapoipondea CHADEMA na DR SLAA believe me wananchi hawakuelewi...Ana kazi kubwa sana ya kufanya hili....

Tatu watanzania wameshaichoka CCM..hata akifufuka NYERERE leo na kuanza kuipigia chepuo CCM itabidi afanye kazi ya ziada...
Mkuu amini usiamini Nyerere akifufuka sasa hivi moja kwa moja atajiunga CHADEMA, maana ndio wenye sera murua za kiukombozi, hawezi kujichanganya na mafisadi CCM!!!
 
Back
Top Bottom