Jukwaa la Celebrity kwa sasa limevurugwa na watu hawa

Mwanzo jukwaa hili lilikuwa lina vitu vitamu vinavyohusu ma celebrity wetu na muziki wao kiujumla huku wanajamvi wakigusia pande zote kuhusu muziki wetu na lilinoga sana.

Ila majuzi hapa jamvini wamekuja chawa rundo humu ndani na kuharibu jukwaa kwa nyuzi za kichawa chawa ,ushabiki maandazi huku wakigeuza jukwaa kuwa Instagram ya umbea umbea. Na uteam bila wao kulipwa hata mia

Wakitoa nyuzi za kukatisha tamaa wasanii wengine wakienda mbali na kuingilia maisha yao binafsi na kuyakejeli. Yaani ukiingia jukwaa hili ni wao wanataka umtaje na kumsifia msanii mmoja tu yaani Diamond Platinumz.

Kwa mtindo huu tutasogeza mziki wetu mbele vipi? Maana hata Diamond mwenyewe anajitahid kuusogeza muziki mbele ila chawa wake ndo mnamuangusha.

Badilikeni tuongelee muziki wa wasanii na sio kupambanisha wasanii.
ila kuna watoto wapuuzi wamezid sana kusifia hadi zile copy and paste kwao wanaona sawa tu,hawajiulizi kwa nini nomination zimedrop sasa siku hizi?
 
ila kuna watoto wapuuzi wamezid sana kusifia hadi zile copy and paste kwao wanaona sawa tu,hawajiulizi kwa nini nomination zimedrop sasa siku hizi?
Na kama ukiongelea at east wanasema una chuki na wivu kumbuka dawa chungu ndo inayoponesha
 
Kunichukia Mimi haisaidii nafanya kazi halali hebu sasa tugeukie kwako usikute upo chuo na unashindia mihogo hahah
Wewe endelea kumiliki media hapa jf,sitaki kubishana na wewe.
Kama unataka hela weka namba apa nikuhonge,au Kama unaogopa kudhalilika nifate PM. Kuhusu swala la kula mihogo, me nakula mihogo Sana tu Ila iwe Ni ya kuchemsha,hivyo kama ulikuwa unataka kunipikia usijali pika tu, Ila kuwa makini usizidishe chumvi.
 
Wewe endelea kumiliki media hapa jf,sitaki kubishana na wewe.
Kama unataka hela weka namba apa nikuhonge,au Kama unaogopa kudhalilika nifate PM. Kuhusu swala la kula mihogo, me nakula mihogo Sana tu Ila iwe Ni ya kuchemsha,hivyo kama ulikuwa unataka kunipikia usijali pika tu, Ila kuwa makini usizidishe chumvi.
Dah Dada siku ukijua kuwa me ndo nawalisha utasema nini sasa..

Ujue mpka sasa sijajua why unanfatafata sana yaani umeshikilia kazi yangu sijui wapi nimesema namiliki media yaani sijui unatafuta mume wa kukuoa?

Tafuta mwingine Dada me nishaoa
 
Dah Dada siku ukijua kuwa me ndo nawalisha utasema nini sasa..

Ujue mpka sasa sijajua why unanfatafata sana yaani umeshikilia kazi yangu sijui wapi nimesema namiliki media yaani sijui unatafuta mume wa kukuoa?

Tafuta mwingine Dada me nishaoa
Sawa danga la jiji 🙌(vijana husema).
 
Vyovyote vile atavyosema haina shida

Yeye Diamond ni nani asiambiwe bhana
Joanah mbona diamond nilimkosoa tafuta Uzi unasema "diamond unakosea kwenye hili" sema tunatofautiana kwenye kujenga hoja ndio maana unahisi Kama labda diamond akoseagi.
 
Back
Top Bottom