Juice na unga wa ngano kutoka viwanda vya Kenya vitaingia Tanzania bila vikwazo na sementi kutoka viwanda vya Tanzania vitaingia Kenya bila vikwazo

Viwanda vyetu hususani kama vya Azam vijiandae kwa maumivu kwani itakuwa ngumu kushindana na maviwanda ya Kenya. Pia na sisi tunaotaka kujenga tujumba twetu tujiandae maumivu kwani cementi ya kutoka viwanda vyetu ambayo ina ubora wa hali ya juu hususani ile ya Dangote, kiasi kikubwa kitakuwa kinaenda Kenya kwani huko itauzwa bei kubwa. Hii ndiyo win win situation? Tunapata juice kwa bei nafuu na kupata sementi kwa bei ya juu zaidi.

Pia majadiliano ya EPA yameanza ili bidhaa kutoka nchi za Europa nazo ziingie Tanzania bila vikwazo kushindana na bidhaa za viwanda vyetu. Hili ni jambo jema ili kuvifundisha adabu viwanda vyetu ambavyo kila kukicha vinatupandishia bei ya bidhaa zao. Mafuta ya kupikia, sukari na kadhalika bei zake hazikamatiki.


Azam na mo mbona wana viwanda kenya
 
Una endorse mkataba wa EPA na EU, sisi tunapeleka nini EU hadi uruhusu bidhaa zote za EU ziingie Tz duty free ? Huyu ndio Rais atakayeua kabisa manufacturing industry ambayo ndio kwanza ilikuwa jnaanza kukomaa baada ya kazi ya muda mrefu ya Mkapa, JK na JPM.
Aue tu. Miaka yangu hii 65 sina la kupoteza
 
Tutakuja kujua baadae kuwa hatuna rais, ila wacha tupige miruzi na vigelegele kwa Sasa!

What's going to happen is an influx of Kenyan made goods in Tz, our export will be totally reduced hence decline of our currency due to higher importation of goods than exportation.

Rais huyu anajaribu kuivua chupi nchi ili kila taifa lijipigie litakavyo, soon ujanja ujanja wa Kenya dhidi ya Tz utarudi kwa Kasi.
Umesemaje paragraph ya mwisho?
 
Viwanda vyetu hususani kama vya Azam vijiandae kwa maumivu kwani itakuwa ngumu kushindana na maviwanda ya Kenya. Pia na sisi tunaotaka kujenga tujumba twetu tujiandae maumivu kwani cementi ya kutoka viwanda vyetu ambayo ina ubora wa hali ya juu hususani ile ya Dangote, kiasi kikubwa kitakuwa kinaenda Kenya kwani huko itauzwa bei kubwa. Hii ndiyo win win situation? Tunapata juice kwa bei nafuu na kupata sementi kwa bei ya juu zaidi.

Pia majadiliano ya EPA yameanza ili bidhaa kutoka nchi za Europa nazo ziingie Tanzania bila vikwazo kushindana na bidhaa za viwanda vyetu. Hili ni jambo jema ili kuvifundisha adabu viwanda vyetu ambavyo kila kukicha vinatupandishia bei ya bidhaa zao. Mafuta ya kupikia, sukari na kadhalika bei zake hazikamatiki.


Kenya hakuna kiwanda cha ngano kikubwa kama AZAM. Na ubora wa bidhaa za AZAM ni wa kimataifa,kwa hiyo AZAM wamepata fursa ya kuuza bidhaa zao Kenya.
 
Tutakuja kujua baadae kuwa hatuna rais, ila wacha tupige miruzi na vigelegele kwa Sasa!

What's going to happen is an influx of Kenyan made goods in Tz, our export will be totally reduced hence decline of our currency due to higher importation of goods than exportation.

Rais huyu anajaribu kuivua chupi nchi ili kila taifa lijipigie litakavyo, soon ujanja ujanja wa Kenya dhidi ya Tz utarudi kwa Kasi.
hivi sasa wajameni tutakaa hivi mpaka lini?!? maana miaka nenda miaka rudi kauli ni ileile tunalinda viwanda vyetu wakati huohuo tunasaini mikataba ya kimataifa (kama huu wa Afrika Mashariki). tunaogopa kushindana!?! yaani hapa tulipofikia hatuna maarifa tene ya kuboresha bidhaa zetu za viwanda kuhimili vishindo vya ushindani?!? hivi makampuni yetu hayawezi kwenda kuuza bidhaa kenya?!?,Burundi, Congo DRC, Chad au Mali!?! hebu wajuzi sanakabisa wa uchumi wa viwanda mtufundishe hapa
 
Huyo ndio SSH, yeye mwenyewe anakuambia anatumia akili, sijui hizi ndio akili zenyewe?
We kenge tuliza mshono. Sisi wenye akili tunaona mambo makubwa anayofanya mama.

We kenge kwa akili yako ndogo huwezi kuona. Kila siku,kazi yako ni kumponda mama..why?
 
Kenya hakuna kiwanda cha ngano kikubwa kama AZAM. Na ubora wa bidhaa za AZAM ni wa kimataifa,kwa hiyo AZAM wamepata fursa ya kuuza bidhaa zao Kenya.
ni kweli sidhani kama AZAM anatetemeshwa na hilo, kuanzia afrika mashariki hii yote mpaka kusini mwa Afrika AZAM yupo hivyo sidhani kama ana hofu yoyote
 
Una endorse mkataba wa EPA na EU, sisi tunapeleka nini EU hadi uruhusu bidhaa zote za EU ziingie Tz duty free ? Huyu ndio Rais atakayeua kabisa manufacturing industry ambayo ndio kwanza ilikuwa jnaanza kukomaa baada ya kazi ya muda mrefu ya Mkapa, JK na JPM.
Nonsense!

You are just making noise.
 
Tutakuja kujua baadae kuwa hatuna rais, ila wacha tupige miruzi na vigelegele kwa Sasa!

What's going to happen is an influx of Kenyan made goods in Tz, our export will be totally reduced hence decline of our currency due to higher importation of goods than exportation.

Rais huyu anajaribu kuivua chupi nchi ili kila taifa lijipigie litakavyo, soon ujanja ujanja wa Kenya dhidi ya Tz utarudi kwa Kasi.
We mataga tulia. Acha kutupigia kelele.

Wakati dikteta wenu mwendazake alipokuwa anatuharibia nchi mbona mlikaa kimyaa? Tulieni mama ajenge nchi.
 
Soma historia kama wewe ni kijana. Viwanda vyote vilivyoko Kenya vilikuwa vyetu kwa pamoja na Uganda kupitia EAC ya zamani iliyoundwa baada tu ya nchi hizi kupata uhuru. Hata hiyo currency ya shillingi ilikuwa moja. Iddi Amini Dada alipoichukua Uganda na sisi kutopenda tukawa buisy kuzozana na huyo Amini. Kenya ikachukua advantage ya mzozano huo na kujimilikisha mali zote za EAC ikiwemo hivyo viwanda na kuvunja EAC. Baada ya kumaliza mzozano huo na Iddi Amini, Tanzania (chini ya JK Nyerere) na Uganda (chini ya Kabuta Mseveni) zilijikuta hazina viwanda, usafiri wa treni wala wa ndege na wala sarafu (currency). Zilirudi back to square one hadi sindano, viberiti, sabuni, dawa ya mswaki etc ilibidi ivinunue kutoka Kenya. Sasa tulikuwa tumeanza ku pick up, hili Kenya hawapendi wanataka tubaki vile vile.
Hiyo historia uliyotoa wapi jomba? Huyo aliyekusimulia alikulisha matango pori kabisa. Kwa mfano,Tanzania,Kenya na Uganda hazijawahi kutumia sarafu moja katika historia!
 
Mkuu kuishi madhariki ya mbali sio kujua kila kitu,
Juice za Azam zote ni chemicals syrups na zimeongezwa sukari,
Ceres na del monte ni natural juice , no preservatives na hazijaongezwa sukari , hawa jamaa kabla hawajaanza kutengeneza juice , waliwekeza kwanza kwenye kilimo cha matunda , ndo maana hata bei ya juice hizo hazifanani
Mbona sijasema najua kila kitu. Nilimaanisha kama wameweza kupata masoko huku watashindwaje kupata soko hapo jirani hadi tuwe na woga wote huo?
Kuhusu ingredients "zote" kuwa artificial kama lina ukweli maana wapo watu wengi wanaowauzia azam maembe na machungwa, sasa huwa wanayapeleka wapi? Kweli kuna juice zao ambazo ni ingredients zote ni artificial na wala hawajawahi ficha na mtu yeyote anaweza jua.
Then kuna ambazo wanatumua juice pulp au concentrate, hizi ni natural ingredients ambazo wanaimport. Concentrate ni juice ya kawaida ila imetolewa maji ili iwe rahisi kusafirishwa na kuhifadhi.
Halafu juu ya yote hayo tujue kila mzalishaji ana target market yake. Kuna watu wanotaka juice isiyo na sukari/preservatives iliyoongezwa na kuna wengine hawajali sana kuhusu hilo. Huyo anayetumia all natural ingredients wateja wake watanunua kwa bei ya juu kidogo kwa hiyo market yake sio sawa na anayetumia additives.
 
hivi sasa wajameni tutakaa hivi mpaka lini?!? maana miaka nenda miaka rudi kauli ni ileile tunalinda viwanda vyetu wakati huohuo tunasaini mikataba ya kimataifa (kama huu wa Afrika Mashariki). tunaogopa kushindana!?! yaani hapa tulipofikia hatuna maarifa tene ya kuboresha bidhaa zetu za viwanda kuhimili vishindo vya ushindani?!? hivi makampuni yetu hayawezi kwenda kuuza bidhaa kenya?!?,Burundi, Congo DRC, Chad au Mali!?! hebu wajuzi sanakabisa wa uchumi wa viwanda mtufundishe hapa
Yaani mimi ninachoshwa sana na hii mentality. Sijui watu wanaogopa nini kwa wakenya na wageni wengine. Mbona ni watu wa kawaida tu na tunashindana nao mara kibao tunawachakaza vibaya mno. Dunia ya sasa hivi sio ya kuogopana, vitu kama hivi ni fursa ya watu kujitanua.
 
Yaani tutafaidi uhondo huo! Na kuna Zesta Jam, Blue Band na Omo! Tutaachana na hiyo mi Redgold Jam na misabuni ya Doffi etc.

Kenya hakuna kiwanda cha ngano kikubwa kama AZAM. Na ubora wa bidhaa za AZAM ni wa kimataifa,kwa hiyo AZAM wamepata fursa ya kuuza bidhaa zao Kenya.
Makubaliano ni ngano ya Kenya kuuzwa Tanzania and not vice versa. Sisi tunaruhusiwa kuuza Kenya sementi na gesi tu, siyo ngano.
 
Hiyo historia uliyotoa wapi jomba? Huyo aliyekusimulia alikulisha matango pori kabisa. Kwa mfano,Tanzania,Kenya na Uganda hazijawahi kutumia sarafu moja katika historia!
Mimi nilikuwapo, si kwamba nimeisoma wapi. Tulikuwa na sarafu moja ya EA. Senti moja na senti 5 zilikuwa na tobo katikati la kuzibeba kama mshikaki. Ndiyo mambo yalikuwa hivyo mtukuu wangu. Senti moja unanunua kilo ya nyama ya ng'ombe ya kwenye ubao! Tumetoka mbali mtukuu wangu. Shillingi 5 unapata dume la makisai.
 
Hawawezi kufurukuta kwa AZAM. Bidhaa za AZAM zina viwango vya kimataifa halafu bei mteremko!
Mkuu tembea uone !
Azam ni chemicals , tupu , nenda kiwandani kwake pale mwandege , uone kama kuna mapera yanatumika inapotengenezwa guava juice , syrups , ingredients , preservatives na sukari .
 
Viwanda vyetu hususani kama vya Azam vijiandae kwa maumivu kwani itakuwa ngumu kushindana na maviwanda ya Kenya. Pia na sisi tunaotaka kujenga tujumba twetu tujiandae maumivu kwani cementi ya kutoka viwanda vyetu ambayo ina ubora wa hali ya juu hususani ile ya Dangote, kiasi kikubwa kitakuwa kinaenda Kenya kwani huko itauzwa bei kubwa. Hii ndiyo win win situation? Tunapata juice kwa bei nafuu na kupata sementi kwa bei ya juu zaidi.

Pia majadiliano ya EPA yameanza ili bidhaa kutoka nchi za Europa nazo ziingie Tanzania bila vikwazo kushindana na bidhaa za viwanda vyetu. Hili ni jambo jema ili kuvifundisha adabu viwanda vyetu ambavyo kila kukicha vinatupandishia bei ya bidhaa zao. Mafuta ya kupikia, sukari na kadhalika bei zake hazikamatiki.


Huu ndio uoga wa kijinga uliomcost Nyerere alidhani akizuia bidhaa za nje viwanda vyetu vitapata solo la ndani huku akisahau kwamba sio kila malighafi atanunua kutoka ndani ya nchi hivyo angehitaji kupata soko la nje ili kupata fedha za kigeni.

Pia alisahau kwamba soko la ndani halijitoshelezi sababu consumer power ilikuwa ndogo kama sasa ilivyo.

Angalia sasa watu waliishia kununua mahitaji ya muhimu hata soda ilionekana ni anasa na hata maji ya chips ikifika wakati wenye familia kubwa walirudi kwenye kuchemsha maji ya kunywa.

Hii yote Ina maanisha kwamba, tunahitaji kutafuta masoko zaidi. Jambo la muhimu ni kutengeneza bidhaa katika ubora wenye kushindana na bidhaa zao hatushindwi tatizo tumezoea kulipua ili tuuze ndani ya nchi yetu tu.

Let's go for international markets.
 
Mkuu tembea uone !
Azam ni chemicals , tupu , nenda kiwandani kwake pale mwandege , uone kama kuna mapera yanatumika inapotengenezwa guava juice , syrups , ingredients , preservatives na sukari .
Asome tu Ile packet ataelewa.
 
Back
Top Bottom