J'tatu hiyooo, Lema njeeee....

J'tatu hiyooo, Lema njeeee....

J.K.Rayhope

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2011
Posts
316
Reaction score
31
Wadau, zimebaki saa chache ambapo mbunge wa Arusha mjini Mh. Godbless Lema atoke kule lupango. Ikiwa Hakimu siku hiyo ameamka akiwa na "stress" akasema hakuna dhamana, kwamba arudi Kisongo au ipo.

Unadhani Lema atakubali kurudi lupango? Je unadhani Mh.Lema amebadilika? Unatazamia nini mapokezi yake?

Nawasilisha
 
Wana wa Arusha.Tunataka iwepo hamasa kubwa watu wamsindikize Lema mahakamani kuanzia gereza la kisongo hadi mahakamani.Kuwe na umati mkubwa kuzidi wa wiki iliyopita.Diwani wetu Nanyaro hamasisha watu ili umati huo iwe ni salaam kwa mkuu wa mkoa ambaye jana amewatukana wana chadema.
 
Natamani Lema akataye tena kupewa dhamana utakuwa ni ujasiri wa hali ya juu
 
Ni kosa kisheria kukataa dhamana na kama mahakama ikiamua inaweza kukuacha ndani kama adhabu kadri itakavyoona inafaa. wale wenzetu watatuambia ni mkono wa CCM
 
lazima nikahudhurie mahakaman nikajue kitakachoendelea
 
Mimi nimeshaBook chumba pale Kisongo kuanzia kesho jumapili nitakua huko ili jumatatu niamkie gerezani kumsindikiza kamanda wa machalii kuja mahakamani! na ole wake huyo hakimu alete Magamba style! Bora atafute sehemu ya kwenda kuishi nje ya jiji la Arusha.
 
Kama Lema hakukubaliana na mahakama kwamba hataki kupewa dhamana kwa muda gani hasitahi kutoka kwa hiari yake hadi pale mahakama itakavyoamua vinginevyo
 
Siku ya Jumatatu ndani ya jiji la Arusha ni siku ya mapunziko baada ya kamanda Lema kutoka!
 
Lema hajui sheria na anataka kucheza nazo na ndio maana CCM wanamchezea kama mpira wa danadana. Alipokataa dhamana alifikiri ni kitendo cha kijasiri na kuwakomoa polisi kumbe wapinzani wake wakatumia nafasi hiyo kumbana kwa sheria. hakuna mkono wa mtu kwani hakunyimwa dhamana siku ya kwanza mbona mbowe, Lisu na Slaa wamepewa wanawasiliana vema na wanasheria wao.
 
Siku ya Jumatatu ndani ya jiji la Arusha ni siku ya mapunziko baada ya kamanda Lema kutoka!

Nina mashaka kama atatoka kesho labda akubali dhamana akikataa ili kukazia uamuzi wake wa kukaa mahabusu hatutamuona hiyo kesho
 
Mimi nimeshaBook chumba pale Kisongo kuanzia kesho jumapili nitakua huko ili jumatatu niamkie gerezani kumsindikiza kamanda wa machalii kuja mahakamani! na ole wake huyo hakimu alete Magamba style! Bora atafute sehemu ya kwenda kuishi nje ya jiji la Arusha.

Labda aende somalia kwani sidhani kama kuna sehem watamwitaji hapa TZ
 
Wana Arusha wengi mjitokeze kumpokea Che Guevara wa Tanzania ningekuwa pande izo nisingemiss.
 
Lema hajui sheria na anataka kucheza nazo na ndio maana CCM wanamchezea kama mpira wa danadana. Alipokataa dhamana alifikiri ni kitendo cha kijasiri na kuwakomoa polisi kumbe wapinzani wake wakatumia nafasi hiyo kumbana kwa sheria. hakuna mkono wa mtu kwani hakunyimwa dhamana siku ya kwanza mbona mbowe, Lisu na Slaa wamepewa wanawasiliana vema na wanasheria wao.

Hata kama ila kajenga heshima kwa vijana wake wa AR na TZ kwa ujumla
 
Magamba wanatamani akubali dhamana ili wapate usingizi
 
Natamani Lema akataye tena kupewa dhamana utakuwa ni ujasiri wa hali ya juu

Atawahi? si alitaka kutoka Serikali ikamwambia subiri ujuwe ni nani zaidi wewe kinyangarakata au Serikali?
 
kama lema hakukubaliana na mahakama kwamba hataki kupewa dhamana kwa muda gani hasitahi kutoka kwa hiari yake hadi pale mahakama itakavyoamua vinginevyo

unalipwa sh.ngapi kwa kazi hii??
 
WAHITIMU WETU CHUO CHA KUIMARISHA ARI YA UPAMBANAJI KISONGO PRISON NDIO HAO MAKAMANDA WETU WANAINGIA URAIANI WIKI IJAYO KUENDELEZA HARAKATI ZA KUTETEA 'HAKI NA UTU' WA MTANZANIA KWA KUDAI KATIBA MPYA YA WANANCHI

Huyo hapo ni GREAT THINKER Mkigoma anapopanga hoja zake kwa uwezo wake wote wa juu zaidi bila kujiuliza kama juhudi za mabadiliko yaweza kutadhminiwa kwa kutaza TUKIO au MCHAKATO mzima?

Nadhani hakuna hata mtu mmoja mwenye akili timamu asiyejua kwamba sana sana CUF wao walichokua wakikipigania tayari walishayapata huko CCM kutokusikika tena kwenye JUKWAA LA KUPIGANIA MABADILIKO nchini. Kama ni KULA MABUA kwa pamoja na nguruwe pori tayari wenzetu wako mbali mno katika hilo la MAPIGANIO YA KUCHUMIA TUMBO.

Kama mwisho wa fikra reli Kigoma ndio itakua imekaa hivi, basi kweli CUF waendelee kuchukua nafasi yao stahili KULA MABUA kwa pamoja na nguruwe pori kama ambavyo ilivyowahi kutamkwa huko nyuma.

Wapambanaji vita mbele ya kidemokrasia na tuwe na hivi karibuni huenda tukawa na mikutano ya wilaya hadi wilaya mara baada ya Makamanda wetu (Dr Slaa, Mbowe, Lema na ...) watakapokua WAMEHITIMU KUPITISHWA KWENYE TANURI LA KUKOMAA ZAIDI KIUPAMBANAJI huko KISONGO PRISONS kupigania HAKI NA UTU wa Mtanzania kwa Nguvu zaidi, Kasi Zaidi na Ari zaidi.

Tunaendelea kuwalaki viongozi wetu hawa kwa heshma na taratibu zote stahiki kote nchini huku tukiwapelekea wananchi ujumbe moja tu: PIGANIA HADI KUFA MCHAKATO MZIMA WA KUPATIKANA KATIBA MPYA YA WANANCHI na mema mengi kufutia baada ya hapo.


Wakati tukielewa fika ya kwamba SUALA LA MABADILIKO KWA MAFAA YA UMMA NI 'MCHAKATO' na kwamba wala si TUKIO tu la siku moja, CHADEMA hatujasau dira ya ukombozi kwa wananchi wote badala ya kuchukua njia ya mkato tu ya baadhi ya viongozi hasa wa chama fulani kujiamulia tu kuendelea KUJICHUMIA TUMBO.

Moto mkubwa ndio kama hivo kila kona ya nchi mpaka kieleweke.


Juzi nimecheka mpaka mbavu zimeniuma kusikia kiongozi Dkt slaa ajificha kwenye masanduku ya spika, kweli chadema mwacheni mzee wa watu ajipumzikie mikiki mikiki ya siasa haiwezi, wakaitisha maandamano nchi nzima utadhani chama chenyewe kipo nchi nzima kumbe ni Arusha, polisi wakatia mkwala ole wake atakaye andamana, wakafyata mkia.

Ndipo ninapowakumbuka cuf wao huwa wanasema wanapenda maandamano yanayozuiwa na polisi na wanapo waona polisi mzuka unapanda, cuf chukueni nafasi yenu mtukomboe.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom