Elinewinga
JF-Expert Member
- Aug 16, 2011
- 632
- 175
Wanaotaka kumlaumu nasari wanakosea na ni wageni kwenye siasa,je kama alipata nafasi ya kukutana na magufuli mnajuaje hakumweleza yanayoendelea kule Dar na moro?
Muwe mnamshauri huyo Ngosha akiwa kwenye ziara kama Rais aache mipasho ya vyama. Shida naiona imeanza kwa kuingiza UCCM.Kama ni hivyo hata Magufuli ni rais wa watanzania hata sisi ambao hatukumpa kura tumeshamkubali.. Magufuli kaenda Arusha kama kiongozi wa serikali na si mwanachama wa CCM...
Mlaumu Nassari kama CDM haiitambui serikali lakini as long as wanaitambua basi hana kosa lolote. Kuna mchangiaji hapo kasema na Meya wa Arusha na viongozi wengine wa CDM walioenda mbona hujawa'address ??
Manina leo upo upande wa nasari!!!Kosa la Nassary ni lipi? Mbowe ndio awe wa kwanza kuwaomba radhi kwa kuwaletea fisadi Lowasa!
Mzalendo Nassari usichoke ...
Umeona eeh? naniliona mwigulu akifurahia na profesa Jay wakiwa na nyuso za tabasamu kabisa labda kama kuna Jambo liko nyuma ya pazia kuhusu Joshua sioni sababu yakufikia watu kua na chuki kiasi hicho wakati hii nchi ya kwetu sote.Kwanza Marandu inabidi uombe radhi kwa kuongezea maneno ya uwongo.Magufuli hakusema ndani ni ccm,alisema ndani mpenda maendeleo. Lakini tuulizane hapa,Nassari alikuwa pekee mtu wa chadema pale kwenye mapokezi? Kwa nini asakamwe yeye tu.
Kulikuwa na Mh Meya wa jiji la Arusha,kulikuwa watu wengi tu wa chadema. Pili Mh Msigwa alimpokea waziri mkuu Mjaliwa lakini hayajasemwa. Tatu Mbunge Mh prof Jay juzi alikuwa na waziri wa mifugo jimboni kwake kutatua mgigoro wa wakulima wa miwa,mbona haulizwi chochote?
Mkuu unakosea unaonyesha unasiasa za chuki sana mpaka basi sasa Rais yuko eneo lake afanyaje?Msichoelewa Kila Jambo Lina wakati wake, Sioni Ubaya Kuungana na Rais Katika Ziara za Maendeleo. Au Kumsifia akifanya Mema. Alichokosea Nassari Ni Timing, Kila Kitu Kina wakati wake. Wakati Wabunge wengine wa Chadema wakihangaika Kuwawekea Dhamana Wenzako, wewe Unazungusha matako yako na Anayehusika Kuwahujumu, Na Palepale anakutumia kuwalamba Vijembe wenzako. Na Unachekelea sio Wazimu huo!
Someni Kabla Hamjajibu, Mimi Joshua simjui Kiundani wala Sina Chuki naye, Nimetathmini yaliyotokea na Haivumiliki. Kama anajitambua alitakiwa Amponde Magufuli, Huwezi Kukubali Kutumiwa kama, "Condom" Kuwatukana wenzako waliokufikisha ulipo. Na Pia kwa yaliyokuwa yakiendelea Huko Dar es salaam na Kilombero, Joshua Nassari hakupaswa kukutana na Magufuli. Ingekuwa Halima Mdee Ni dada yake Nassari angeenda Kukutana na aliyemweka Rumande kwa sababu za Kishenzi? Sasa hilo ndio naona lilikuwa Kosa Kubwa na Ujinga wa Nassari.
Umesema ni tetesi,wacha mimi nipite sina muda.Niliona tetesi Jana, za habari ya Magufuli akimsifia Joshua Nassari, Kuwa Ni Kijana safi, ambaye Usoni ni Chadema lakini Ndani ni CCM. Haya yalikuwa Ni matusi ya Magufuli kwa Chadema kumtumia Nassari. Ni aibu sana na ni Unafiki Kusema ati mtu safi anayefanya Mema na anayetenda haki Ndani Ni CCM. Ni CCM ipi? Iliyoiba Ushindi wa Urais Bara? Iliyofuta Ushindi wa Zanzibar? Inayohaha Kila Mahali Kuiba Nafasi za Umeya? Iliyowarudisha wezi wote wa Escrow kwenye madaraka? Iliyokalia Uchafu wa Muhimbili, badari, TRA etc? CCM ipi ambayo huyu anazungumzia?
Najua Siku za Nyuma, Mwenyekiti Mbowe alishahudhuria na Kumsifia Kikwete na Magufuli katika Ufuunguzi wa Barabara. Lakini hakufanya hivyo wakati Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa wamekamatwa na Kufuunguliwa Kesi za Kishenzi. Alichokosea Nassari ni Timing, Kuwepo kwake Ziara za Magufuli kama Kimalaya fulani, Kumemfanya Magufuli amtumie sawia kujihalalisha na Kutukana Vyama.
Joshua Nassari bwana mdogo, Nikuambie Kuwa alichokupa Magufuli sio Sifa Ni Matusi, Nimekuona Kwenye Gazeti Ukichekelea kama juha, kwa sababu hutumii akili. Wakati akina Halima Mdee, Wabunge na Madiwani wa Chadema wakiwa Rumande wewe unapeleka maninii kwenye Ziara za anayetuma unyama huu.
Na Kama Ulilazamika Kwenda, Ulitakiwa Palepale baada ya Kikao Ukanushe, "Sifa" Zile na Useme wewe Upo pale Kama mbunge wa UKAWA na Huoni sawa Kufananishwa na CCM.
Mwisho Nikuambie Nassari Mwanangu, Ulichofanya Ni sawa na Kuwapiga Mateke ya Puani na Masikio, watu mmoja mmoja wa Chadema waliopigwa na Polisi, waliowekwe jela, waliokesha waliotoa fedha, waliokupigania kuwa Mbunge. Ukitaka Kujua CCM hawana Maslahi Na wewe Mwangalie Ole Sendeka! And you are very light weight compered to many! Hata Nikikusikiliza Bungeni Joshua Wewe bado Kabisa Kukua, angalia Usijinyonge Kisiasa.
Na Kwa Ukawa Kama Josua Hatatubu, Mvumilieni amalize Muda wake, lakini akimaliza aende atakako. Msimpe tena Tiketi ya Kugombea Ubunge Arumeru. Ni bora jimbo lipotee Kuliko kuwa na Mbunge anayesaliti Wenzake waliompigania
Haonekani ibadani,hiyo ni hoja dhaifu sana, kazi ya mbunge siyo kuhudhuria ibadaNoted mimi natokea Meru ni muda tu haujafika he has to quit! No compromise na anayemzika mazima ni mkuu wa Wilaya huyu ametokea kuwa karibu sana na wana Meru kuliko hata mbunge na mkuu huyu wa wilaya ana tengeneza njia nyeupe kwa mgombea wa ccm atakayekuja. Nasari haonekani ibadani wala kwingineko. .....anyway mambo yake ni complicated sana. CDM bado tunaipenda SANA