Wanabodi.
Joto la Uchaguzi Mkuu linazidi kupamba moto baadhi ya makada wa Chadema wameanza kutangaza nia zao za kugombea nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho. Habari za ndani kabisa kutoka Makao Makuu ya Chadema pale Kinondoni Mtaa wa Ufipa kupitia kwa kada wa siku nyingi wa Chadema zinasema kuwa
Josephine Mshumbusi, amejiandaa kugombea ubunge Jimbo la Kawe kupitia Chadema mwaka 2015.
Jimbo la Kawe kwa sasa linaongozwa na Mbunge Halima Mdee, kupitia Chadema pia, inasemekana imetokea sintofahamu kati ya Halima Mdee na uongozi wa juu wa Chadema baada ya
Josephine, kutangaza nia yake ya kulitaka jimbo la Kawe imefikia mpaka Halima Mdee kususia mikutano na harakati za M4C.