Jongoo ana nini mpaka wanawake mumuogope?

Jongoo ana nini mpaka wanawake mumuogope?

View attachment 499058

Nadhani wanaoogopa majongoo siyo wanawake peke yako... hata baadhi ya wanaume pia wanagopa majongoo...
  • Majongoo hupendelea sana kujitokeza nyakati za mvua.
  • Hawana sumu ya kusema, itamdhulu binadamu lakini wana tezi ambazo zinauwezo wa kutengeneza maji maji, ambayo husababisha allergy kwa watu wengi. Hayo maji maji yanauwezo wa kunguza ngozi yako au kusababisha muwasho mkali sana na kuharibu ngozi. Wengine wanasema usimguse jongoo atakujambia.
  • Ukiachilia mbali maji maji wanayotoa pia wanangata, na maumivu yake ni makali kwa sababu yanaambatanishwa na sumu, lakini siyo sumu ya kukuua.
  • Kuna baadhi ya majongoo, kwenye kujihami hurusha au humwaga maji maji yenye harufu kali, mbali na yote itakuachia vitu kama malengelenge kwenye ngozi yako.
  • Wengi pia labda watakuwa wanaogopa ile miguu yake... majongoo wana miguu 40-400 mpaka 750

cc: mahondaw
Hivi jongoo hutumika kufanyia nin? Na wanafaida gan?kunasiku niliona MTU akisafirisha hayo makitu kwenye boksi bahati mbaya hakufika mbali alikamatwa na polisi huku akilala mika kuna MTU amemchomea akasikika mtua akisema hao jongoo wana faida sikuelewa wanafaida gan
Ila jongoo wanatisha jamani has a ukutane na Yale makubwa yanarangi nyeusi lazima mwili usisimke na sarakas zisizo na matarajio
 
Nadhani hili suala linachangiwa na mabadiliko ya mazingira. Kwa mfano nilikokulia mimi kumshika kinyonga, konokono, jongoo, panzi maduduwasha ni mambo ya kawaida kabsa wakati mwingine kuna watu humshika hadi nyoka. Ila najaribu kupata picha kwa MTU aliekulia DSM ambae anajua kupanda daladala na Schule, biashara n.k.
Shambani hapajui,
Kufuga hajui ni sawa kuwa na uoga wa namna hio
 
huwa wanatisha hivi hasa wawe wale wanene. kuna siku nilipita chini ya muembe akanidondokea mmoja begani uuuwi siwez kusahau, mpaka kesho sipiti wala kusimama chini ya muembe
Hahahah inaelekea hata ukitaka kula embe ukimkumbuka jongoo basi unaliacha
 
Jongoo ana chemical anayo itoa inaitwa hydrogen cynide.... Utafit wang utaanzia kam hii chemical ipo kweny manii. Hapa c kuna watu wanasem jongoo =dushe. Ndiomana nimejarib ingia ndan kidogo
Hiyo kemikali anaitoa anapohisi hatari au anaitoa muda wowote tu?
 
Jongoo ana sumu inayoitwa cyanide ni hatari kama ukiila(ingest)... Anatumia kemikali hio kujilinda na wanaomla (predators kama ndege na baadhi ya wanyama)
Jongoo wengi wana rangi za onyo (aposematic colouration) mara nyingi ni nyeusi na rangi zingine mng'ao kama nyekundu na njano(hapo kwenye picha tunaona ni nyeusi na miguu mekundu) .... Rangi hizo huonya adui wa jongoo kama ndege na wengineo (ni kama kusema nione na kaa mbali na mimi, mi sifai kuliwa nina sumu kali)... Jongoo wengi wakiguswa hujifanya umbo la mviringo (kujilinda) au kujitupa(kwa kuzunguka kwa kasi kama nyoka) hapo uiga nyoka (mimicry) yote ni kujilinda na anayeweza kua adui... Kuna mnyama mmoja anapenda sana kula jongoo... Tunamuita fungo (civet),huyu mwili wake unaweza kuchakata sumu ya jongoo isimdhuru.
NB:kama sio mtaalam wadudu epuka kugusa wadudu wenye rangi za mng'ao...hasa mchanganyiko wa nyeusi, nyeupe, nyekundu au njano Wengi wao wanasumu(chemicals za majimaji) inayoweza kutoa malengelenge au kuunguza ngozi. Japo kuna wadudu wanatumia hizo rangi kudanganya wana sumu (mimicry)
Ama kweli wewe ni Jungle master, Ahsante sana mkuu kwa elimu ya bure kabisa,
na usisite kuja kutuelezea mengi zaidi ili tuwafahamu vizuri.
Sasa swali la kujiuliza inamaana hawa wanawake wamepewa sense kubwa kabisa ya kuhisi hatari ndomana huwa wanawaogopa pasipo kutambua wanawaogopa kwasababu gani? Cc miss chagga Valentina mahondaw ukhuty Shunie
 
Kuna duduwasha flani hivi tulipokuwa watoto tulikuwa tunaambiwa eti linaingia kunyonya ubongo kupitia puani, yaani mpaka na uzee huu sitaki kabisa kuliona lile ingawa najua siyo kweli.
mwenye tabia hiyo tuliambiwaga ni Kenge, sijui kweli
 
Ama kweli wewe ni Jungle master, Ahsante sana mkuu kwa elimu ya bure kabisa,
na usisite kuja kutuelezea mengi zaidi ili tuwafahamu vizuri.
Sasa swali la kujiuliza inamaana hawa wanawake wamepewa sense kubwa kabisa ya kuhisi hatari ndomana huwa wanawaogopa pasipo kutambua wanawaogopa kwasababu gani? Cc miss chagga Valentina mahondaw ukhuty Shunie
kabisa Mungu katupendelea
 
Jongoo ana sumu inayoitwa cyanide ni hatari kama ukiila(ingest)... Anatumia kemikali hio kujilinda na wanaomla (predators kama ndege na baadhi ya wanyama)
Jongoo wengi wana rangi za onyo (aposematic colouration) mara nyingi ni nyeusi na rangi zingine mng'ao kama nyekundu na njano(hapo kwenye picha tunaona ni nyeusi na miguu mekundu) .... Rangi hizo huonya adui wa jongoo kama ndege na wengineo (ni kama kusema nione na kaa mbali na mimi, mi sifai kuliwa nina sumu kali)... Jongoo wengi wakiguswa hujifanya umbo la mviringo (kujilinda) au kujitupa(kwa kuzunguka kwa kasi kama nyoka) hapo uiga nyoka (mimicry) yote ni kujilinda na anayeweza kua adui... Kuna mnyama mmoja anapenda sana kula jongoo... Tunamuita fungo (civet),huyu mwili wake unaweza kuchakata sumu ya jongoo isimdhuru.
NB:kama sio mtaalam wadudu epuka kugusa wadudu wenye rangi za mng'ao...hasa mchanganyiko wa nyeusi, nyeupe, nyekundu au njano Wengi wao wanasumu(chemicals za majimaji) inayoweza kutoa malengelenge au kuunguza ngozi. Japo kuna wadudu wanatumia hizo rangi kudanganya wana sumu (mimicry)
na kunakipindi kipo chanel ya wanyama dstv wanasema nyani hutumia jongooo kama dawa ya kujizuia na wadudu wanao wadhuru.. na niliona nyani anamkamata jongoo anana muuma na meno halafu anajirushia damu ya jongooo yule muelezeaji akasema ile ni kinga dhidi ya wadudu
 
Juzi nilihama nyumba kisa nilikuta gamba la nyoka ndani....nyoka ni hatari jmn kuliko hata jongoo
Bora nyoka umuone na umuue, kuliko kumuona alafu apotelee chumbani heheheh
 
kabisa Mungu katupendelea
Jongoo ana umbo lenye vipingili (segments) kila segment ina pea mbili za miguu (Jongoo anaweza kuwa na miguu mia mpaka 700 lakini haiwezi fika 1000 kama jina la Kiingereza linavosuggest "millipedes" (kutoka latin milli=1000 pedes=legs) wanapendelea unyevunyevu, mara nyingi huonekana nyakati za mvua au maeneo yanaotunza unyevunyevu kwa muda mrefu... Wanakufa haraka kama ardhi inakua kavu... Kuna baadhi ya Jongoo hukwepa hali ya ukavu kwa kujifukia kwenye udongo wenye unyevunyevu au chini ya magamba ya miti na mawe... Jongoo wanakula majani, mbao au mimea ilioza kwenye ardhi.... Ni muhimu sana kwa kuchakata maozo ya mimea lakini pia wanaweza kuwa waaribifu kwa kula mizizi ya karanga na hata pamba kama wakizidi... Jongoo hutaga mayai kwa kuyafukia kwenye ardhi (yenye unyevunyevu)
 
Jongoo ana umbo lenye vipingili (segments) kila segment ina pea mbili za miguu (Jongoo anaweza kuwa na miguu mia mpaka 700 lakini haiwezi fika 1000 kama jina la Kiingereza linavosuggest "millipedes" (kutoka latin milli=1000 pedes=legs) wanapendelea unyevunyevu, mara nyingi huonekana nyakati za mvua au maeneo yanaotunza unyevunyevu kwa muda mrefu... Wanakufa haraka kama ardhi inakua kavu... Kuna baadhi ya Jongoo hukwepa hali ya ukavu kwa kujifukia kwenye udongo wenye unyevunyevu au chini ya magamba ya miti na mawe... Jongoo wanakula majani, mbao au mimea ilioza kwenye ardhi.... Ni muhimu sana kwa kuchakata maozo ya mimea lakini pia wanaweza kuwa waaribifu kwa kula mizizi ya karanga na hata pamba kama wakizidi... Jongoo hutaga mayai kwa kuyafukia kwenye ardhi (yenye unyevunyevu)
asante mkuu kwa somo
 
Back
Top Bottom