Jongoo ana nini mpaka wanawake mumuogope?

Jongoo ana nini mpaka wanawake mumuogope?

Bora wao jongoo haonekani mara nyingi, wengine tunataman paka wapotee duniani maana tunaogopa kupita kiasi
37103e9554a1c086fa9e44016bd80240.jpg

Mwenzio paka ndio starehe yake...
 
jongoo akikupandia unawashwa kweli me siwapendi ila joka na panya nikikutana nao naweza zimia
 
huwa wanatisha hivi hasa wawe wale wanene. kuna siku nilipita chini ya muembe akanidondokea mmoja begani uuuwi siwez kusahau, mpaka kesho sipiti wala kusimama chini ya muembe
 
Jongoo ana chemical anayo itoa inaitwa hydrogen cynide.... Utafit wang utaanzia kam hii chemical ipo kweny manii. Hapa c kuna watu wanasem jongoo =dushe. Ndiomana nimejarib ingia ndan kidogo
 
View attachment 499058

Nadhani wanaoogopa majongoo siyo wanawake peke yako... hata baadhi ya wanaume pia wanagopa majongoo...
  • Majongoo hupendelea sana kujitokeza nyakati za mvua.
  • Hawana sumu ya kusema, itamdhulu binadamu lakini wana tezi ambazo zinauwezo wa kutengeneza maji maji, ambayo husababisha allergy kwa watu wengi. Hayo maji maji yanauwezo wa kunguza ngozi yako au kusababisha muwasho mkali sana na kuharibu ngozi. Wengine wanasema usimguse jongoo atakujambia.
  • Ukiachilia mbali maji maji wanayotoa pia wanangata, na maumivu yake ni makali kwa sababu yanaambatanishwa na sumu, lakini siyo sumu ya kukuua.
  • Kuna baadhi ya majongoo, kwenye kujihami hurusha au humwaga maji maji yenye harufu kali, mbali na yote itakuachia vitu kama malengelenge kwenye ngozi yako.
  • Wengi pia labda watakuwa wanaogopa ile miguu yake... majongoo wana miguu 40-400 mpaka 750

cc: mahondaw
Jongoo ana sumu inayoitwa cyanide ni hatari kama ukiila(ingest)... Anatumia kemikali hio kujilinda na wanaomla (predators kama ndege na baadhi ya wanyama)
Jongoo wengi wana rangi za onyo (aposematic colouration) mara nyingi ni nyeusi na rangi zingine mng'ao kama nyekundu na njano(hapo kwenye picha tunaona ni nyeusi na miguu mekundu) .... Rangi hizo huonya adui wa jongoo kama ndege na wengineo (ni kama kusema nione na kaa mbali na mimi, mi sifai kuliwa nina sumu kali)... Jongoo wengi wakiguswa hujifanya umbo la mviringo (kujilinda) au kujitupa(kwa kuzunguka kwa kasi kama nyoka) hapo uiga nyoka (mimicry) yote ni kujilinda na anayeweza kua adui... Kuna mnyama mmoja anapenda sana kula jongoo... Tunamuita fungo (civet),huyu mwili wake unaweza kuchakata sumu ya jongoo isimdhuru.
NB:kama sio mtaalam wadudu epuka kugusa wadudu wenye rangi za mng'ao...hasa mchanganyiko wa nyeusi, nyeupe, nyekundu au njano Wengi wao wanasumu(chemicals za majimaji) inayoweza kutoa malengelenge au kuunguza ngozi. Japo kuna wadudu wanatumia hizo rangi kudanganya wana sumu (mimicry)
 
Back
Top Bottom