Jongoo ana sumu inayoitwa cyanide ni hatari kama ukiila(ingest)... Anatumia kemikali hio kujilinda na wanaomla (predators kama ndege na baadhi ya wanyama)
Jongoo wengi wana rangi za onyo (aposematic colouration) mara nyingi ni nyeusi na rangi zingine mng'ao kama nyekundu na njano(hapo kwenye picha tunaona ni nyeusi na miguu mekundu) .... Rangi hizo huonya adui wa jongoo kama ndege na wengineo (ni kama kusema nione na kaa mbali na mimi, mi sifai kuliwa nina sumu kali)... Jongoo wengi wakiguswa hujifanya umbo la mviringo (kujilinda) au kujitupa(kwa kuzunguka kwa kasi kama nyoka) hapo uiga nyoka (mimicry) yote ni kujilinda na anayeweza kua adui... Kuna mnyama mmoja anapenda sana kula jongoo... Tunamuita fungo (civet),huyu mwili wake unaweza kuchakata sumu ya jongoo isimdhuru.
NB:kama sio mtaalam wadudu epuka kugusa wadudu wenye rangi za mng'ao...hasa mchanganyiko wa nyeusi, nyeupe, nyekundu au njano Wengi wao wanasumu(chemicals za majimaji) inayoweza kutoa malengelenge au kuunguza ngozi. Japo kuna wadudu wanatumia hizo rangi kudanganya wana sumu (mimicry)