Jongoo ana nini mpaka wanawake mumuogope?

Jongoo ana nini mpaka wanawake mumuogope?

Kila nikipitisha jicho langu nakutanana na huu uzi

Hilo jongoo jamani linanitesaa nikilionaaaa mh
 
Jongoo ni mdudu mdogo sana ambaye anaogopwa na jopo kubwa kabisa la wanawake,
Hii inafika mbali zaidi mpaka unakuta wanawake wanatoka nduki huku wakisasambua nguo zao, wengine hujikuta wanaruka Kung-Fu Panda bila kutegemea huku wakituachia TV ya bureee eti kisa wamekaona kajijongoo kanapita karibu yao!

Kitu kilichonifanya mpaka nishangae unakuta wengi ukiwauliza wanadai eti huwa wanamuogopa jongoo sana tena kuliko nyoka,
Umeona balaa hilo? Yani eti nyoka mwenye sumu kwao ni bwege tu, lakini akiona jongoo atapiga yowe utadhani U.S.A ameona mabomu ya Korea Kaskazini.!

Sasa wanawake inabidi mje mtuambie kipi kinachofanya mpaka mumuogope kiasi hiko?

mtoto mdogo wa kiume wa umri wa miaka 8 anaweza kuwa shujaa zaidi ya mwanamke wa miaka 40 anayeogopa jongoo.watoto wenyewe hawaogopi jongoo lakini utashangaa limama lizima linaogopa huwa wanajifanyisha tu
 
Hao unaosema wewe anaitwa Jongoo Bahari, huwa wanapatikana baharini hasa maeneo ya mtwara na Zanzibar, Kiingereza anaitwa orthurians, kwa Tanzania bara ni Marufuku kuwavua hawa wanavuliwa kwa magendo na huwa wanasafirishwa kwenda China na Japan, wako tofauti na hawa wanaoogopwa na Wanawake
12345562_1537756376515336_2143176297438305009_n.jpg
unamaanisha kama huyu mkuu maana nilikuwa sijui kama kuna jongoo bahari
 
Jongoo ni mdudu mdogo sana ambaye anaogopwa na jopo kubwa kabisa la wanawake,
Hii inafika mbali zaidi mpaka unakuta wanawake wanatoka nduki huku wakisasambua nguo zao, wengine hujikuta wanaruka Kung-Fu Panda bila kutegemea huku wakituachia TV ya bureee eti kisa wamekaona kajijongoo kanapita karibu yao!

Kitu kilichonifanya mpaka nishangae unakuta wengi ukiwauliza wanadai eti huwa wanamuogopa jongoo sana tena kuliko nyoka,
Umeona balaa hilo? Yani eti nyoka mwenye sumu kwao ni bwege tu, lakini akiona jongoo atapiga yowe utadhani U.S.A ameona mabomu ya Korea Kaskazini.!

Sasa wanawake inabidi mje mtuambie kipi kinachofanya mpaka mumuogope kiasi hiko?
Mkuuu subiri nikafanye uhakiki wa hiki then nitarud
 

Attachments

  • 17862706_1905311366415618_147950993096450433_n.jpg
    17862706_1905311366415618_147950993096450433_n.jpg
    55 KB · Views: 67
  • 17425106_1891972114416210_5673007929924776290_n.jpg
    17425106_1891972114416210_5673007929924776290_n.jpg
    23.5 KB · Views: 65
mtoto mdogo wa kiume wa umri wa miaka 8 anaweza kuwa shujaa zaidi ya mwanamke wa miaka 40 anayeogopa jongoo.watoto wenyewe hawaogopi jongoo lakini utashangaa limama lizima linaogopa huwa wanajifanyisha tu
Wanatukata stimu kwa kuogopa vitu vya ajabu ajabu,
Kuna siku nilitaka kuchinja kuku, sasa nikamwambia dem anishikie nikachukue kisu, dah ile namkabidhi hivi yule kuku akarusha mbawa kidogo basi yule dem alimrusha huku akipiga mayowe, kile kitendo cha kumuachia kiliniudhi sana manake ilinipa kazi ya kuanza kumkimbiza yule kuku
 
Jongoo ni mdudu mdogo sana ambaye anaogopwa na jopo kubwa kabisa la wanawake,
Hii inafika mbali zaidi mpaka unakuta wanawake wanatoka nduki huku wakisasambua nguo zao, wengine hujikuta wanaruka Kung-Fu Panda bila kutegemea huku wakituachia TV ya bureee eti kisa wamekaona kajijongoo kanapita karibu yao!

Kitu kilichonifanya mpaka nishangae unakuta wengi ukiwauliza wanadai eti huwa wanamuogopa jongoo sana tena kuliko nyoka,
Umeona balaa hilo? Yani eti nyoka mwenye sumu kwao ni bwege tu, lakini akiona jongoo atapiga yowe utadhani U.S.A ameona mabomu ya Korea Kaskazini.!

Sasa wanawake inabidi mje mtuambie kipi kinachofanya mpaka mumuogope kiasi hiko?


Nahisi wanamfananisha na dushelele linalo litembea likiwa na miguu Zaidi ya 1000.
 
Kiukweli me siogopi jongoo,nyoka,chura,kinyonga nawashika kabisa labda kutoka na nature ya kibarua changu isipokuwa mende especial yule anaye paa maana anakaa kama anakukimbiza unaweza gongana na ukuta
 
sijajua labda enzi za utoto wamama walikuwa wanatumia njia hii ili waache kukojoa kitandani,mimi ni mwanaume lakini kunakipindi cha nyuma sikuwa rafiki na chura kabisa nikimuona lazima nimpekipigo lakini yote nikwa imani niliyojijengea baada ya mama kutumia mbinu hii kunitisha niache kukojoa kitandani enzi za darasa la pili hasa kipindi cha baridi.Alikuwa ananambia ukilala leo nakufungia chura kiunoni ukikojoa tu chura anauma dudu,japo ilikuwa utani tu hakuwahi kufanya hivyo ila ilifikia hatua nikawa na wahate sana chura
 
Back
Top Bottom