John Mnyika: Taifa linaongozwa na sadist..

John Mnyika: Taifa linaongozwa na sadist..

Hizo ni allegations tu, he who allege, must prove, kama anao ushaidi wa kuthibitisha aje mbele na afanye hivyo.
 
Ni maneno ya Mbunge wa Kibamba na kiongozi wa CHADEMA, John J. Mnyika.

Ametweet kwamba taifa linaongozwa na sadist. Sijui anamaanisha taifa gani ila huenda akawa anamaanisha Tanzania. Kwa maana hiyo, kiongozi wa taifa hili ni sadist!

Sadist ni neno la kiingereza linalomaanisha mtu ambaye furaha yake inapatikana pale anapowaumiza wengine. Ni kama katili fulani hivi anayeburudishwa na mateso ya watu wengine.

Si mara ya kwanza kwa Mnyika kutoa misemo ya alama kwa viongozi wa taifa hili. Itakumbukwa wakati wa Rais Kikwete alimuita Rais huyo Dhaifu bungeni na jina hilo likavuma mpaka sasa.

Hili sio tusi kweli?!

Mnyika amalizane na hiyo SACCOS yao kabla hajaanza kutoa ushauri kwa wengine.
 
Nauliza jamani niambieni, mtu anayetaka watu waishi kama mashetani ni nani?

Ni nani huyo anayetumia rambirambi za wahanga huku akiwananga?

Anayetaka wasiokuwa na pesa ya kivuko wapige mbizi, ana upendo sana ati ehee?

Hivi kweli anayejali atawaambia watumishi wake muhimu ati wakabangue korosho kwa meno?

Ni jeuri ya namna kumwambia msaidizi na mtendaji wako mkuu ati nitawapiga hata shangazi zako!! Kweli?

MUNGU ATUPONYE NA ROHO YA USADIST, NI ROHO YA KOROSHO NA HAIFAI KABISA.

MSEMA KWELI NI MPENZI WA MUNGU.
 
Back
Top Bottom