John Magufuli: Ninautamani urais!

John Magufuli: Ninautamani urais!

Huyu atakuwa dhaifu kuliko JK! Mambo mengi ya kitaifa ananyamazia hatujui msimamo wake...kwanza toka lini injinia akawa raisi! Akajenge madaraja huko!
unamchukia bure tu, wewe umefanyia nini nchi yako, ukifika ofisi kutwa jamii forum, uzalishi wala nini
 
Mimi nakubaliana na wanaosema kuwa gamba ni gamba tu(Nyumba za serikali alizouza kwa hasara),lakini kuna magamba mengine ni dawa hata yakibanguliwa yanahifadhiwa kwa matumizi ya baadaye kwanini kwa sababu ni dawa.Tukumbuke Mh.Magufuri aliwahi kuwanyan'ganya viwanja magamba wenzie,aliwanyan'ganya magari ya umma yaliyoandikwa majina binafsi huku yakighalimiwa na serikali ktk uendeshaji wake,wenye kumbukumbu watakumbuka ilimbidi rais ampe ulinzi kwa ajili ya usalama wake, ktk hayo nampongeza,swali langu ni hili Je waliokumbwa na fagio lake watakubali awe na mamlaka kamili au watapenda awe chini ya ili aendelee kudhibitiwa? CC kama imetakasika basi itampitisha kugombea.
 
Hamuwezi kuwa marasi bana!....tunafahamu vema...mko very "mechanical"!!
Hiyo computer /simu unayotumia kujibu uzi huu ni product ya engineering,''no engineers no life''-PERIOD
ni watu wa vitendo sio wapiga domo huku mambo yakiharibika.
 
Waungwana naomba mulonge si kwa ushabiki wala unafiki, ila kwa hoja zilizoshiba na zenye mashiko. Kama uchaguzi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ungefanyika leo, ni nani ungempa kura yako aiongoze Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kati ya Dr. MAGUFULI na EDWARD LOWASA?
Kiongozi ambae ataweza kututoa kwenye hii bahari ya Ufukara, asimamie haki na kutetea maslahi ya wanyonge wa Tanzania na raslimali zao ambazo kwa mda mrefu sasa zinawanufaisha wachache hasa wa tabaka tawala?
Najua wengi ni wakereketwa wa vyama fulani fulani vya siasa hapa nchini, naomba tutoke huko kwa mda mfupi, tujengane kwa hoja zenye mashiko bila kujali chama cha siasa wanachotoka niliowataja. Mikataba isiyo na tija kwa Taifa, hofu ya kuwawajibisha mafisadi, wala rushwa na wimbi la uanzishaji wa mifumo ya utendaji kazi isio na tija kwa Taifa iwe dira yetu katika kuchambua uwezo wa wawahusika niliowataja hapo juu kwenye nafasi ya Uraisi wa nchi hii.
Mashiko ya hoja zenu, yatatujenga wengi na kutoa mwelekeo mpya wa harakati zinazoendelea hapa nchini na baadhi ya vigogo wenye nia ya kuwania nafasi 2015.
By LULAMSO
Hapo penye red,
lazima tujiulize ni vitu gani vinaleta hofu,kwa mtizamo wangu,namba moja naweka usafi wa mhusika.kama ni mtu aliyewahi kuhusika na scandal kadhaa,hii inaleta hofu kwani anaogopa kuumbuliwa na hata kuwajibishwa endapo msiri wake ataamua kutoa siri kama malipizo ya yale atakayotendewa wakati kiongozi akitekeleza majukumu yake.Hii inaweza kusababisha hata watu wasio na uwezo kupewa madaraka makubwa kama fadhila kwa msiri wa mhusika.
Pili ni kuhofia maisha yake endapo ataziba maslahi ya wenye uwezo,hii naipa asilimia ndogo kwani viongozi wakuu wa kitaifa hupewa ulinzi na serikali hata baada ya kustaafu majukumu yao.
Tatu kutojua mamlaka aliyonayo,hii husababisha kuwaogopa hata watu walioko chini yake kwa kudhania yeye ni yule wa zamani aliyewahi kuonewa na wahusika na hivyo akiwawajibisha atakipata cha mtema kuni,Hii nayo haina madhara sana maana siku moja anaweza kupata mtu wa kumfumbua macho
Hivyo naona kati ya hawa yeyote aliyewahi kuwa na scandal iwe ya kweli au ya kughushi hafai,kwani anayejua kama ni ya kweli au ya kughushi ni mhusika mwenyewe na si vinginevyo,kama ni ya kughushi ,ni afadhali haina madhara lakini kama ni ya kweli ni hatari kubwa maana atakuwa na wasiri wengi wanaotegemea kulipwa fadhila bila kujali uwezo wao wa kikazi.
 
Anakubalika sana huyu, sio watu watu wa ajabu ajabu hao wengine wenye mikashfa mpaka ya kupora wake za watu
labda ulikuwa hujazaliwa au hujatoka kijijini kwenu nyanchenche lakini huyu ndiye aliyeiba nyumba za serikali za oysterbay na kwingineko.
 
unamchukia bure tu, wewe umefanyia nini nchi yako, ukifika ofisi kutwa jamii forum, uzalishi wala nini

We ndio mbwiga kweli!
Wananchi wote ikiwemo wewe tunalipa kodi....!! ambazo mafisadi wanakula akiwemo Magufuli!
 
yaani umesema mwana hata mm ananikera kwa unafiki wake sijui anajipendekeza iili aonekane bora, kumbe si chochote
Huyu jamaa ni mnafiki sana kutwa ni kumsifia rais kuwa safari zake ndio zinaleta misaada Kumbe ni hasara kubwa
 
wakimpa huyu karata awakilishe, anaweza kushinda kwasababu watu wengi mtaani wanaongea mema juu yake. hata mimi naweza kumpa kura huyu, to be frank...
 
We ndio mbwiga kweli!
Wananchi wote ikiwemo wewe tunalipa kodi....!! ambazo mafisadi wanakula akiwemo Magufuli!

utakalia hivyo hivyo mpaka uwe babu huna hata kiti unasubiri serikali ikununulie na wewe kutwa kupiga soga,
 
nitampa saport magufuri akiomba urais , maana hakuna mwingine kama yeye
 
katika viongozi 10 wasafi na makufuri yumo, anastahili kugombera urais wa nchi hii
 
Magufuli is very strong and smart for tht post

Ndg ifweero kweli usemavyo huyu kiutendaji yupo strong na wapo wengi ndani ya chama ni watendaji imara na thabiti lkn hawafai kuwa viongozi. Kiongozi haogopi na hawi mnafiki. Naamini kama ataondoka CCM na kubadilika kifikra ataweza kuwa Kiongozi mzuri sana kutenda na kuongoza.
 
Du huyu bwana sina swali akitangaza nia basi upele utakuwa umepata mkunaji hakuna mpinzan wake kutoka mashariki wala magharibi ila sema shida ni kwamba sijui kama anaweza pitishwa jina ila kaka huje jembe ulaya!!!!!hata wanaombeza wanajua maneno yake urais hauna fan ati mpaka awe nan mara ooh mbona injia hizo ni hoja za kitoto
 
tena nilikua nimeahirisha mambo ya kupiga kura wakimteua huyo itabidi nikapange foleni.

Samahani huwezi ukawa na akili timamu ukaahirisha kupiga kura, mbaya unatuambia kama sifa vile, nimekushusha kweli kweli, Wasio piga kura ndo wanaochangia watu wabovu kupata madaraka, je na wewe ni ama mbovu au uko nao wezi wetu???
 
utakalia hivyo hivyo mpaka uwe babu huna hata kiti unasubiri serikali ikununulie na wewe kutwa kupiga soga,

Hehee hehee!! mliutaka uraisi hata rushwa mlitumia huku mkichekacheka!!....
Sasa nchi inawashinda mnasema serilkali haifanyi kila kitu mlaaniwe wana CCM WOTE! kwa kukimbia wajiibu wenu wa kuongoza nchi na kubaki na ngonjera za serikali haiwezi kufanya kila kitu!!...
 
"Mpitisheni Waziri Magufuli Urais 2015".....Huu ni ushauri waliotoa Wakazi wa Tegeta kwa CCM

attachment.php

KATIKA hali isiyo ya kawaida, baadhi ya wakazi wa Tegeta, Dar es Salaam, wamekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumpitisha Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli awe mgombea wa chama hicho kwenye nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu 2015, kutokana na uchapakazi wake kwenye sekta ya ujenzi wa barabara nchini.


Wakazi hao walitoa ushauri huo jana wakati Dkt. Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Said Meck Sadick wakikagua barabara ya Mwenge-Tegeta, ambayo ujenzi wake umekamilika.

Katika ukaguzi huo, wakazi hao baada ya kumwona Dkt. Magufuli, walianza kumshangilia na kusema anafaa kuwa Rais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu 2015.

"Mheshimiwa wewe unafaa kuwa Rais, hongera sana kwa kutupunguzia foleni kwani una chapakazi...hakuna mwingine zaidi yako lakini barabara hii haina taa hivyo tunaomba utuwekee," walisema.

Akizungumza na wananchi hao, Dkt. Magufuli alisema maendeleo hayana itikadi ya chama chochote cha siasa wala dini bali ni ya watu wote ambapo miradi yote ya ujenzi wa Barabara katika jiji hilo itagharimu sh. trilioni moja hadi kukamilika kwake.

Alisema kazi hiyo inafanywa na Rais Jakaya Kikwete kutoka na ushirikiano mzuri uliopo na mataifa mengine na barabara hiyo ataizindua mwenyewe kabla ya kuondoka madarakani ili asije Rais mwingine akasema yeye ndiye aliijenga.

"Baada ya miaka mitatu, jiji la Dar es Salaam halitakuwa na foleni tena kwani hivi sasa, barabara hii imekamilika kwa gharama ya sh. bilioni 89, katika bajeti ya mwaka huu, tumetenga sh. bilioni 2 ili kuiwekea taa ila daraja lina uwezo wa kuhimili tani 180 lakini mnapaswa kutambua kuwa, hakuna vitamu bila uchungu," alisema Dkt. Magufuli.
Aliongeza kuwa, mbali ya barabara hiyo upanuzi wa Ujenzi wa Barabara ya Mwenge hadi Morocco, nao uko mbioni kuanza na ile ya kutoka Bagamoyo hadi bandarini ipo katika hatua za mwisho kwa ajili ya kuanza kazi ili kupunguza msongamano.

"Tupo katika hatua za mwisho za kuanza ujenzi wa barabara za juu, kutakuwa na barabara za ghorofa tatu zinazopishana pale Ubungo na Tazara ambako ujenzi wake utaanza Oktoba mwaka huu, nyingine itakuwa Kamata, lengo ni kupunguza foleni," alisema.

Kwa upande wake, Bw. Sadick aliwaonya watu wanaohujumu miundombinu ya miradi ya Barabara baada ya kupewa taarifa kuwa sababu zinazosababisha Mkandarasi wa Barabara ya Mabasi yaendayo Kasi (DART), kushindwa kuikabidhi ni kutokana na watu kuiba taa.

Alisema hadi sasa, taarifa alizopewa taa saba na mabomba yake yameibwa ambapo mifuniko ya maji mchafu 12 na alama za barabara 25, nazo zimeibwa na watu wasio waaminifu.

"Ni marufuku kwa mtu yeyote kufanya biashara eneo la barabara ya mradi huo au kupumzika katika vituo vya mabasi haya...miradi hii inatumia fedha nyingi lakini watu wachache wanataka kuturudisha nyuma," alisema Bw. Sadick.

Naye Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada alisema Serikali ya nchi yake itaendelea kufadhili miradi mbalimbali ya barabara ili kupunguza tatizo la foleni nchini.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale, alisema baadhi ya miradi ya barabara inakwamishwa na watu ambao tayari wamelipwa fidia lakini wanadai fidia waliyolipwa ni ndogo.
Source:Mpekuzi
 

Attachments

  • photo-1.JPG
    photo-1.JPG
    19.6 KB · Views: 2,805
Habari mzuri ila toa mambo ya uraisi hapo magufuli hanaga tamaa na hayo mambo
 
Back
Top Bottom