John Magufuli: Ninautamani urais!

John Magufuli: Ninautamani urais!

Mzee wa visasi asiyependa challenge si wapinzani wake woye ndani nanje ya chama wataishia jela
Watu wasiopenda kufuata sheria na utaratibu hao watakuwa hawana chao, visasi na kutopenda challenge si kweli, wasiopenda kusimamia haki ndio wanaona anawavurugia mambo yao kwa vile hamuonei mtu aibu.Angalau yeye mara mia kuliko wote waliobaki kutoka vyama vyoootea vya nchi hii, tusahai siasa, tuache uzandiki na majungu kama tunataka kutoka hapa tulipo, tumuombe Magufuli achukue nchi
 
"Mpitisheni Waziri Magufuli Urais 2015".....Huu ni ushauri waliotoa Wakazi wa Tegeta kwa CCM

attachment.php

KATIKA hali isiyo ya kawaida, baadhi ya wakazi wa Tegeta, Dar es Salaam, wamekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumpitisha Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli awe mgombea wa chama hicho kwenye nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu 2015, kutokana na uchapakazi wake kwenye sekta ya ujenzi wa barabara nchini.


Wakazi hao walitoa ushauri huo jana wakati Dkt. Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Said Meck Sadick wakikagua barabara ya Mwenge-Tegeta, ambayo ujenzi wake umekamilika.

Katika ukaguzi huo, wakazi hao baada ya kumwona Dkt. Magufuli, walianza kumshangilia na kusema anafaa kuwa Rais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu 2015.

"Mheshimiwa wewe unafaa kuwa Rais, hongera sana kwa kutupunguzia foleni kwani una chapakazi...hakuna mwingine zaidi yako lakini barabara hii haina taa hivyo tunaomba utuwekee," walisema.

Akizungumza na wananchi hao, Dkt. Magufuli alisema maendeleo hayana itikadi ya chama chochote cha siasa wala dini bali ni ya watu wote ambapo miradi yote ya ujenzi wa Barabara katika jiji hilo itagharimu sh. trilioni moja hadi kukamilika kwake.

Alisema kazi hiyo inafanywa na Rais Jakaya Kikwete kutoka na ushirikiano mzuri uliopo na mataifa mengine na barabara hiyo ataizindua mwenyewe kabla ya kuondoka madarakani ili asije Rais mwingine akasema yeye ndiye aliijenga.

"Baada ya miaka mitatu, jiji la Dar es Salaam halitakuwa na foleni tena kwani hivi sasa, barabara hii imekamilika kwa gharama ya sh. bilioni 89, katika bajeti ya mwaka huu, tumetenga sh. bilioni 2 ili kuiwekea taa ila daraja lina uwezo wa kuhimili tani 180 lakini mnapaswa kutambua kuwa, hakuna vitamu bila uchungu," alisema Dkt. Magufuli.
Aliongeza kuwa, mbali ya barabara hiyo upanuzi wa Ujenzi wa Barabara ya Mwenge hadi Morocco, nao uko mbioni kuanza na ile ya kutoka Bagamoyo hadi bandarini ipo katika hatua za mwisho kwa ajili ya kuanza kazi ili kupunguza msongamano.

"Tupo katika hatua za mwisho za kuanza ujenzi wa barabara za juu, kutakuwa na barabara za ghorofa tatu zinazopishana pale Ubungo na Tazara ambako ujenzi wake utaanza Oktoba mwaka huu, nyingine itakuwa Kamata, lengo ni kupunguza foleni," alisema.

Kwa upande wake, Bw. Sadick aliwaonya watu wanaohujumu miundombinu ya miradi ya Barabara baada ya kupewa taarifa kuwa sababu zinazosababisha Mkandarasi wa Barabara ya Mabasi yaendayo Kasi (DART), kushindwa kuikabidhi ni kutokana na watu kuiba taa.

Alisema hadi sasa, taarifa alizopewa taa saba na mabomba yake yameibwa ambapo mifuniko ya maji mchafu 12 na alama za barabara 25, nazo zimeibwa na watu wasio waaminifu.

"Ni marufuku kwa mtu yeyote kufanya biashara eneo la barabara ya mradi huo au kupumzika katika vituo vya mabasi haya...miradi hii inatumia fedha nyingi lakini watu wachache wanataka kuturudisha nyuma," alisema Bw. Sadick.

Naye Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada alisema Serikali ya nchi yake itaendelea kufadhili miradi mbalimbali ya barabara ili kupunguza tatizo la foleni nchini.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale, alisema baadhi ya miradi ya barabara inakwamishwa na watu ambao tayari wamelipwa fidia lakini wanadai fidia waliyolipwa ni ndogo.
Source:Mpekuzi

Magufuri yuko vizuri kiutendaji..ila ingependeza huyu jamaa angekuwa waziri mkuu..angetoa hamsha hamsha kwa mawaziri wake watu wangetoa kuwa mawaziri mizigo..
 
..kashfa yake ya kuuza nyumba za serikali kwa bei ya kutupa na kusababisha hasara ya mabilioni kama siyo trilioni ni ushahidi kwamba Dr.Magufuli hafai kwa nafasi ya uraisi.

..lingine ni tabia yake ni kiburi na ubabe katika utekelezaji wa majukumu yake. kuna wakati alivunja kituo cha mafuta kule Mwanza bila kuzingatia ushauri wa wataalamu. matokeo yake serikali ikaburuzwa mahakamani na ikaamuliwa kwamba mwenye kituo cha mafuta alipwe sh bilioni 14.

..vilevile Magufuli kwa kauli zake ktk mikutano mbalimbali inaelekea haamini ktk siasa za ushindani. yeye siku zote hutoa kauli za kukashifu wapinzani, na kudanganya wananchi waziwazi kuhusu mfumo wetu wa vyama vingi.

..mwisho, Dr.Magufuli hana busara na umakini unaotakiwa kuwa nao head of state. chukulia kitendo chake cha kwenda Kenya wakati wa uchaguzi na kumpigia kampeni Raila Odinga. Lile lilikuwa ni kosa kubwa sana la kidiplomasia kwa kuzingatia kwamba Dr.Magufuli ni waziri mwandamizi ktk serikali ya Tanzania. Kidiplomasia kitendo cha Magufuli kinaweza kabisa kuchukuliwa kama Tanzania kuingilia uchaguzi wa Kenya.

cc domokaya, Camalillo, Mojo, Mahebe, Mp Kalix2
 
Last edited by a moderator:
Bahati mbaya hatuna uraisi wa majimbo tungekushauri umpe huko kwenu. Unatikiriburaisi uwaziri? Wapo waliokuwa mawaziri wazuri kwa kazi na sura baada ya kupata uraisi wamechakaa na kuchoka mbaya
 
Bahati mbaya hatuna uraisi wa majimbo tungekushauri umpe huko kwenu. Unatikiriburaisi uwaziri? Wapo waliokuwa mawaziri wazuri kwa kazi na sura baada ya kupata uraisi wamechakaa na kuchoka mbaya
Mwenye kufikiri na kujibu hoja namna yako si aina ya watu nianofanyanao majadiliano, unao wa aina yako, nisamehe kama nitakuwa nimekuudhi kwa hoja niliyoileta
 
Mambo mengine ni ya kuongea barazani kwako sio huku kwenye fikra pevu. Ukija kijinga utapata majibu ya kijinga ili uudhike kama ulivyotuudhi. Ngoma draw.
 
Huyu aliehusika kuuza nyumba za serikali, Huyu alieratibu na kuwezesha kupaa kwa deni la Taifa kasha kuwagawia MAFISADI wenzie ulaji? hope your kidding ...
"Mpitisheni Waziri Magufuli Urais 2015".....Huu ni ushauri waliotoa Wakazi wa Tegeta kwa CCM

attachment.php

KATIKA hali isiyo ya kawaida, baadhi ya wakazi wa Tegeta, Dar es Salaam, wamekitaka Chama Cha Mapinduzi (CCM), kumpitisha Waziri wa Ujenzi, Dkt. John Magufuli awe mgombea wa chama hicho kwenye nafasi ya urais katika Uchaguzi Mkuu 2015, kutokana na uchapakazi wake kwenye sekta ya ujenzi wa barabara nchini.


Wakazi hao walitoa ushauri huo jana wakati Dkt. Magufuli akiwa na Mkuu wa Mkoa huo, Bw. Said Meck Sadick wakikagua barabara ya Mwenge-Tegeta, ambayo ujenzi wake umekamilika.

Katika ukaguzi huo, wakazi hao baada ya kumwona Dkt. Magufuli, walianza kumshangilia na kusema anafaa kuwa Rais kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu 2015.

"Mheshimiwa wewe unafaa kuwa Rais, hongera sana kwa kutupunguzia foleni kwani una chapakazi...hakuna mwingine zaidi yako lakini barabara hii haina taa hivyo tunaomba utuwekee," walisema.

Akizungumza na wananchi hao, Dkt. Magufuli alisema maendeleo hayana itikadi ya chama chochote cha siasa wala dini bali ni ya watu wote ambapo miradi yote ya ujenzi wa Barabara katika jiji hilo itagharimu sh. trilioni moja hadi kukamilika kwake.

Alisema kazi hiyo inafanywa na Rais Jakaya Kikwete kutoka na ushirikiano mzuri uliopo na mataifa mengine na barabara hiyo ataizindua mwenyewe kabla ya kuondoka madarakani ili asije Rais mwingine akasema yeye ndiye aliijenga.

"Baada ya miaka mitatu, jiji la Dar es Salaam halitakuwa na foleni tena kwani hivi sasa, barabara hii imekamilika kwa gharama ya sh. bilioni 89, katika bajeti ya mwaka huu, tumetenga sh. bilioni 2 ili kuiwekea taa ila daraja lina uwezo wa kuhimili tani 180 lakini mnapaswa kutambua kuwa, hakuna vitamu bila uchungu," alisema Dkt. Magufuli.
Aliongeza kuwa, mbali ya barabara hiyo upanuzi wa Ujenzi wa Barabara ya Mwenge hadi Morocco, nao uko mbioni kuanza na ile ya kutoka Bagamoyo hadi bandarini ipo katika hatua za mwisho kwa ajili ya kuanza kazi ili kupunguza msongamano.

"Tupo katika hatua za mwisho za kuanza ujenzi wa barabara za juu, kutakuwa na barabara za ghorofa tatu zinazopishana pale Ubungo na Tazara ambako ujenzi wake utaanza Oktoba mwaka huu, nyingine itakuwa Kamata, lengo ni kupunguza foleni," alisema.

Kwa upande wake, Bw. Sadick aliwaonya watu wanaohujumu miundombinu ya miradi ya Barabara baada ya kupewa taarifa kuwa sababu zinazosababisha Mkandarasi wa Barabara ya Mabasi yaendayo Kasi (DART), kushindwa kuikabidhi ni kutokana na watu kuiba taa.

Alisema hadi sasa, taarifa alizopewa taa saba na mabomba yake yameibwa ambapo mifuniko ya maji mchafu 12 na alama za barabara 25, nazo zimeibwa na watu wasio waaminifu.

"Ni marufuku kwa mtu yeyote kufanya biashara eneo la barabara ya mradi huo au kupumzika katika vituo vya mabasi haya...miradi hii inatumia fedha nyingi lakini watu wachache wanataka kuturudisha nyuma," alisema Bw. Sadick.

Naye Balozi wa Japan nchini, Masaki Okada alisema Serikali ya nchi yake itaendelea kufadhili miradi mbalimbali ya barabara ili kupunguza tatizo la foleni nchini.

Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale, alisema baadhi ya miradi ya barabara inakwamishwa na watu ambao tayari wamelipwa fidia lakini wanadai fidia waliyolipwa ni ndogo.
Source:Mpekuzi
 
Kwa tafiti zangu binafsi,nimegundua kuwa watanzania wameamka sasa kutoka usingizini kuwa,njama ya kutaka kuendelea kuongozwa na viongozi wafanyabiashara,wala rushwa na mafisadi.mwaka huu ni wa kiongozi makini mh.John Pombe Magufuli.wengine wakae benchi.waziri mkuu atakuwa mh.dr slaa,spika atakuwa lipumba.hayo ni mawazo yangu tu yaheshimiwe.
 
Afai na ubabe wake. akiwa rais haya ndo tutashuhudia
1. utawala wa mkapa utarud kwa mlango wa nyuma
2. mauaji ya wakulima na na wafugaji. wadukuma
wamezagaa kote nchini.msukuma awe raid nchi itakuwa jangwa kama mz na shy. nyumba za serkali ataziuza zilizobaki
 
Tehe tehe, John sawa lakini Wilibrodi na Haruna bado sijashawishika.
 
Afai na ubabe wake. akiwa rais haya ndo tutashuhudia
1. utawala wa mkapa utarud kwa mlango wa nyuma
2. mauaji ya wakulima na na wafugaji. wadukuma
wamezagaa kote nchini.msukuma awe raid nchi itakuwa jangwa kama mz na shy. nyumba za serkali ataziuza zilizobaki
Wwe na chuki binafsi tu na kumuonea gere John, hawa akina Wilibrodi na Haruna ndiyo feki kabisa.
 
Makufuli rais wa Tanzania,Lowassa rais wa Tanzania,Sitta rais wa Tanzania,Wassira rais wa Tanzania,Mwigulu rais wa Tanzania,January rais wa Tanzania,Tibaijuka rais wa Tanzania,Makinda rais wa Tanzania,Kigwangwala rais wa Tanzania,Shein rais wa Tanzania,Migiro rais wa Tanzania,Makongoro rais wa Tanzania.Aliye iloga CCM Alisha kufa siyo bure.
 
magufuli hafai kabisa bora hata mr.nice lakn si viroba, am sorry pumb.u daah! sorry again i meant pombe makufuli.
 
magufuli hafai kabisa bora hata mr.nice lakn si viroba, am sorry pumb.u daah! sorry again i meant pombe makufuli.
 
Kwenye kichwa cha habari "Magufuri" kwenye utumbo "Magufuli".

Hivi hizo shule huwa mnaenda kusomea ujinga?
 
Magufuli na mkapa waliuza nyumba za serikali hafai.
 
Afai na ubabe wake. akiwa rais haya ndo tutashuhudia
1. utawala wa mkapa utarud kwa mlango wa nyuma
2. mauaji ya wakulima na na wafugaji. wadukuma
wamezagaa kote nchini.msukuma awe raid nchi itakuwa jangwa kama mz na shy. nyumba za serkali ataziuza zilizobaki

Magufuli na Sumaye kama wanataka urais warejeshe kwanza nyumba za serikali walizogawiana na nyingine kuuziana kwa bei che.
 
Back
Top Bottom