Ukikaa chini na utafakari kwa makini utaona kila kitu katika nchi yetu kimesambaratika.Sekta muhimu katika kujenga maendeleo rasilimali watu imetupwa mbali. Elimu, afya, uvuvi, kilimo, nyumba na makazi, umiliki wa mali na ardhi vyote vinawaneemesha wanaoitwa wawekezaji. Raia wa Tanzania ameonekana si chochote si lolote, wakazi wa vijijini hadhi zao zimebadilika, kimsingi wanaonekana ni wapuuzi ambao ubinadamu wao unafananishwa na wanyama. Wanaonekana si watu wanaostahili kuishi nyumba nzuri, kunywa maji safi wala kupata huduma nzuri za afya, wameonekana na watu wa daraja la mwisho hivyo kufanya asilimia kubwa ya watanzania wanaounda kundi hili kuonekana wanaishi kwa fadhila tu ya watu 'wawekezaji au watu wenye masilahi na wawekezaji.
Nikiangalia kushoto na kulia sioni mtu mwenye nia na lengo la dhati la kututoa katika hili. Ndani ya CCM simuoni, huko UKAWA nako ndo kabisa na wapi sijui, kwa akina Dovutwa wote waliobaki wasakatonge wenye kuamini katika "wawekezaji"..
Mtu pekee ninayemuona kuwa anaweza kuwa "Musa" wetu na kututoa hapa tulipo ni John Pombe Magufuli. Angalau katika viongozi wa nchi hii hatishwi na wawekezaji na mwenye uthubutu wa kuwakemea na hata kuwashughulikia wanapopindihs utaratibu, pia Magufuli ndiye kiongozi pekee aliyepo katika serikali yetu ambaye kwanza hutambua kazi yake kwa mujibu wa sheria na huamua kuitekeleza pasipo kupepesa macho. Ana uwezo wa kusema ukweli hata kumwambia Rais mbele ya hadhara. Alishfanya hivyo kwa rais aliyestaafu Benjamin Mkapa na alishawahi kumwambia Rais wetu Kikwete umuhimu wa kufuata utaratibu na sheria na kuacha kusikiliza watu wenye fitina, uongo, umbea na uzandiki.
Bila kujali itikadi, kwa kuifikiria zaidi Tanzania, Tanzania ipi katika hali mbaya kiuongozi, nchi imepoteza muelekeo, watanzania tumedharau na tumeacha kufuata utaratibu, tumejenga utamaduni wa njia za mkato na nani ana nani wa kumlinda. Kila mtu anavunja sheria, kuhujumu nchi na kumuonea anayeweza kumuonea kwa nafasi yake na kwa nguvu yake.
Uongozi wa Magufuli umeonesha hauna kujuana, kupendelana, kuoneana haya wala aibu, ni uongozi wenye kuchapa kazi kwa kufuata sheria na uongozi wenye kuonesha kila kitu kina maana na bora kwa watanzania, hata uvuvi wa samaki.
Umefika muda kwetu watanzania tuamue kuondoka katika hali hii, tutafuta kiongozi ambaye hata kwa macho hatuna mashaka nae, kiongozi ambaye mioyoni mwetu tutakuwa na imani naye na tutakuwa kwatu kuwa nyuma yake kumfuta hata kama njia takayotumia itakuwa na miiba ilhali itatuchoma kiasi lakini tutafika kule tunapotaka kwenda kuliko ilivyo hivi sasa ambapo tumekuwa tunazunguka mduara pasipo kwenda popote badala yake tunaishia kupata kizunguzungu tu