PreGE2025 John Heche: John Mrema amekimbia na Akaunti za YouTube na X za Chama, tuligundua kila wiki analipwa Tsh. Milioni 3

PreGE2025 John Heche: John Mrema amekimbia na Akaunti za YouTube na X za Chama, tuligundua kila wiki analipwa Tsh. Milioni 3

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
440
Reaction score
3,211
1000343546.jpg
Tuna watu ambao wamenufaika na chama hiki wakakifanya kama mali binafsi. John Mrema alikuwa mkurugenzi wetu wa Habari na Uenezi na namtaja. YouTube channel ya chama inaitwa CHADEMA Digital inamilikiwa na nani?

Kwenye YouTube Channel, kila unapopata hits YouTube inakulipa pesa. Wakafungua YouTube acc ya chama, ina followers laki 4 kumbe ana imiliki yeye na kijana mmoja. Kila wiki wanalipwa zaidi ya Tsh. Milioni 3. Tumeyakuta hayo ofisini.

Unamiliki YouTube channel ya chama, unalipwa wewe, leo tumekata mirija ya ufisadi unaanza kupiga kelele huko? Na waende wanako enda. Hatuwezi kuwa na chama cha aina hii.

Wamechukua YouTube channel yetu wamekimbia nayo, wamechukua acc ya X wamekimbia nayo kwa kisingizio kwamba walitumia credentials zao kufungua acc hizo. Wameamua kuungana na dola, tutashughulika nao.

John Heche
Mei 16, 2025 kwenye Uzinduzi wa CHADEMA Family, Kata ya Bulyanhulu, Jimbo la Msalala, Chadema Familia ina wanachama hai 250.

Pia soma CHADEMA: Akaunti zetu za chama za YouTube na X (Twitter) zimedukuliwa

Majibu ya John Mrema - John Mrema: Madai ya kuwa nimekimbia na YouTube na X za CHADEMA si kweli, sikuwa hata na Password ya hiyo Mitandao
 
Mangi huyu ni hatari sana!

Mungu fundi kweli kweli, kaisaficha CHADEMA kabla haijashika dola. Vinginevyo, ingekuwa hatari sana chama hiki kushika dola kikiwa na aina hii ya watu. CCM wangekuwa cha mtoto.

Hakika Mungu ana makusudi na kila jambo.

Better a greedy hyena than a greedy politician.
 
Tuna watu ambao wamenufaika na chama hiki wakakifanya kama mali binafsi. John Mrema alikuwa mkurugenzi wetu wa Habari na Uenezi na namtaja. YouTube channel ya chama inaitwa CHADEMA Digital inamilikiwa na nani?

Kwenye YouTube Channel, kila unapopata hits YouTube inakulipa pesa. Wakafungua YouTube acc ya chama, ina followers laki 4 kumbe ana imiliki yeye na kijana mmoja. Kila wiki wanalipwa zaidi ya Tsh. Milioni 3. Tumeyakuta hayo ofisini.

Unamiliki YouTube channel ya chama, unalipwa wewe, leo tumekata mirija ya ufisadi unaanza kupiga kelele huko? Na waende wanako enda. Hatuwezi kuwa na chama cha aina hii.

Wamechukua YouTube channel yetu wamekimbia nayo, wamechukua acc ya X wamekimbia nayo kwa kisingizio kwamba walitumia credentials zao kufungua acc hizo. Wameamua kuungana na dola, tutashughulika nao.

John Heche
Mei 16, 2025 kwenye Uzinduzi wa CHADEMA Family

Pia soma CHADEMA: Akaunti zetu za chama za YouTube na X (Twitter) zimedukuliwa
Kulikuwa na mchwa wengi sana ndani ya chama
 
Kwamba Youtube Channel tu 3 M kwa kila wiki ?!!! na followers laki nne ?!!!!!

Basi wamuombe huyu bwana hata wampe pesa wamuajiri awe mfanyakazi wao ili aweze kuwaingizia kipato kwa vitu kama hivi...; Kwahio wao walikuwa hawafuatilii haya mambo yanavyokwenda ?

Tuachane na hawa tuelekeze resources chache kumpinga Samia
 
Back
Top Bottom