Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 4,393
- 14,498
Makamu Mwenyekiti Tanganyika, John Heche kuzungumza na Watanzania kupitia Chadema Media TV YouTube, Jioni hii baada Polisi kuzuia Mkutano wake na Waandishi wa Habari uliokuwa ufanyike leo Juni 17, 2025 saa Tano Asubuhi
"Mwezi Juni 2025 Mahakama Kuu ya Tanzania ilitoa hukumu kwenye Shauri dogo la kesi ya msingi namba 8323-2025 ambapo ilieleza na kutoa amri tatu"
"Katika Kesi hiyo aliyokuwa Makamu mwenyekiti wa Chama chetu (CHADEMA) upande wa Zanzibar kwa miaka takribani miaka 15 ndugu Said Issa Mohammed pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Chama wa sasa ndugu Ahmed Rashid Hamis, Mama Maulida Komu amabao ni mmoja wa waasisi wa Chama kwa pamoja wameshtaki Chama wakilalamikia mgao wa rasilimali kuto wapendelea Zanzibar"
Mimi kwa niaba ya CHADEMA nasema hatuna imani na Jaji Mwanga kwa sababu hatuamini kama kuwanyima haki ya kusikilizwa bodi ya wadhamini wa Chama na Katibu Mkuu wa chama ni makosa ya kibinadamu badala yake tunaona alifanya akijua ili kutimiza lengo lake. Aidha Sababu ya pili inatokana na historia ya Jaji Mwanga, Mheshimiwa Jaji Mwanga ameteuliwa kutoka Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC) msimamo wa CHADEMA dhidi ya INEC pamoja na ZEC mara zote tunazikosoa kwa utendaji pamoja na muundo wake."
"Katika mazingira hayo kesi inayohusu CHADEMA anapangiwa Jaji anayetoka kwenye Taasisi ambayo tunailalamikia hatuoni kama tunatendewa haki na kweli hatujatendewa haki sisi tunamuona akiwa na mgongano wa kimaslahi (conflict of interest) na kwa sababu hizo tunaomba Jaji Mwanga ajitoe katika kusikiliza kesi yetu"
"Mwezi Juni 2025 Mahakama Kuu ya Tanzania ilitoa hukumu kwenye Shauri dogo la kesi ya msingi namba 8323-2025 ambapo ilieleza na kutoa amri tatu"
"Katika Kesi hiyo aliyokuwa Makamu mwenyekiti wa Chama chetu (CHADEMA) upande wa Zanzibar kwa miaka takribani miaka 15 ndugu Said Issa Mohammed pamoja na Wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Chama wa sasa ndugu Ahmed Rashid Hamis, Mama Maulida Komu amabao ni mmoja wa waasisi wa Chama kwa pamoja wameshtaki Chama wakilalamikia mgao wa rasilimali kuto wapendelea Zanzibar"
Mimi kwa niaba ya CHADEMA nasema hatuna imani na Jaji Mwanga kwa sababu hatuamini kama kuwanyima haki ya kusikilizwa bodi ya wadhamini wa Chama na Katibu Mkuu wa chama ni makosa ya kibinadamu badala yake tunaona alifanya akijua ili kutimiza lengo lake. Aidha Sababu ya pili inatokana na historia ya Jaji Mwanga, Mheshimiwa Jaji Mwanga ameteuliwa kutoka Tume ya Uchaguzi Zanzibar(ZEC) msimamo wa CHADEMA dhidi ya INEC pamoja na ZEC mara zote tunazikosoa kwa utendaji pamoja na muundo wake."
"Katika mazingira hayo kesi inayohusu CHADEMA anapangiwa Jaji anayetoka kwenye Taasisi ambayo tunailalamikia hatuoni kama tunatendewa haki na kweli hatujatendewa haki sisi tunamuona akiwa na mgongano wa kimaslahi (conflict of interest) na kwa sababu hizo tunaomba Jaji Mwanga ajitoe katika kusikiliza kesi yetu"
