Taifa la Majungu, Wikendi Hii Mataifa kama BRAZIL, INDONESIA , MALAYASIA, CHINA, na kazalika wanachi wake huamkia viwanjani kufanya mazoezi ili J3 wawe fiti kwa ajili ya Kujenga mataifa yao, Ndo maana Nchi kama Brazili Imeipita hadi Uingereza kwa sasa,
Huku Tanzania iwe siku ya kazi, iwe Wikendi ni Majungu kutwa nzima, watu wako bise kuwatumikia Bwana zao wakati Bwana zao siku kama ya leo asubuhi humakia kwenye Viwanja vya GYMKHANA kupasha then Mchana hujimwaga Serena Hoteli kunywa Nvinyo, watumika wako bise kwenye Mitandao watu hawalali, huu ni muda wa Msosi lakini watu wako Mtandaoni kufanya majungu,
Hii nchi kuendelea ni vigumu sana, mimi sina chama lakini some time Serikali inalaumiwa bure, haiwezekani watu wanaamkia kwenye mitandao, wanashinda kwenye mitandao,
Tumeshindwa hata kutengeneza hata vijiti vya meno, techinolijia rahisu kabisa, tunaagiza had toilet Paper, Ni muda gani watu wanawaza kuendeleza Taifa? Watu wakitoka humu ni Kusoma magazeti ya Porojo za siasa, na Udaku
Taifa la Majungu, Tiafa la watumika, ni lini Utatumikiwa na wewe?