PreGE2025 John Heche akamatwa na Polisi Kariakoo

PreGE2025 John Heche akamatwa na Polisi Kariakoo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
Tunakemea sana hili mtu kujichukulia hatua za kufanya Mkutano pahala bila kuzingatia taratibu husika / au zinazotakiwa kufuata,
-Inshort amefanya tukio ili akamatwe!
#Shame!
Nadhani takwa la kisheria ni kutoa taarifa (notice) ya mkutano, sio kuomba kibali.
 
No reforms no election imeshaingia kwenye veins za wanamageuzi.

Kuwakamata viongozi sio mwisho wa dawa kuendelea kufanya kazi.

Hebu angalia hapo ukurasa wa rais ulivyofikia level ya kuficha maoni ya watu robo tatu ya maoni ni kukosoa uongozi uliopwaya , haiishi hapo page ya rais inablock wananchi wake wakitoa maoni.

Bahati nzuri X haitoi namna ya mtu kufuta maoni asiyopenda zaidi ya kuficha vinginevyo hii page ingefuta maoni mengi na kuacha ya kusifia ila bado wamefunikwa , nina imani Samia anasoma hiyo page japo haiendeshi yeye ila kuna ujumbe watu wanatuma .


View: https://x.com/SuluhuSamia/status/1914260652291416533?s=19
 
Nimeiangalia hiyo Video hakuna sababu zozote za kuuharibu mkutano wa CHADEMA na Wananchi.
 
Haiwezekani akamatwe bila sababu, lazima kuna jambo, aidha kuna uchochezi aliokuwa akipandikiza hapo kariakoo kwani haiwezekani raia mwema kukamatwa bila sababu!
Watazania tuache kuugeuza upuuzi kuwa sehemu ya maisha yetu,umaskini wetu ni sababu ya upuuzi wetu. Na mambo yetu ya kipuuzi
 
Haiwezekani akamatwe bila sababu, lazima kuna jambo, aidha kuna uchochezi aliokuwa akipandikiza hapo kariakoo kwani haiwezekani raia mwema kukamatwa bila sababu!

Anachokifanya huyu polisi kimo kwenye PGO?

Alichukuliwa hatua gani kwa kujihusisha na siasa za kuchagua upande?
 
Hawa Mapolisi wamekuwa full wanasiasa wa CCM. Basi wajiite Jumuiya ya Polisi force ya CCM ili tujue moja.
 
kumbe akili wanayo ila wanajizima WI-FI
Heche ndio kajizima kariakoo huwezi simamisha gari madereva wa gari nyuma yako watakuja juu waweza choma moto gari kuwachelewesha waendako

Polisi walikuwa sahihi

Dar unasimamisheje gari katikati ya barabara busy eti unahutubia

Pale alikuwa anawinda pesa za tonetone limebuma
 
Wanachama wa chadema ni majasiri sana mtandaoni ila kwa ground viongozi wanakamatwa kama kuku tena mbele yao na wanatulia kama wamemwagiwa maji
 
Back
Top Bottom