Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Beki mkongwe mwenye jina kubwa katika soka la Afrika Mashariki, Joash Onyango, amezua gumzo mara baada ya kujiunga rasmi na kikosi cha Kenya Police FC akitokea timu ya Dodoma Jiji ya Tanzania. Onyango, ambaye amewahi kung’ara na miamba wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Simba SC na Singida Black Stars, anatajwa kuwa na umri wa miaka 26, ingawa mitandaoni mashabiki wanazidi kufanya utani wakidai ana umri wake ni miaka 62.
Onyango mwenye miaka 26 anasifika kwa kuwa mchezaji mwenye nguvu, uzoefu mkubwa wa kimataifa na nidhamu ya kipekee katika safu ya ulinzi. Katika misimu aliyocheza nchini Tanzania, alijijengea sifa ya kuwa beki asiyeogopa changamoto, akiwazuia washambuliaji hatari na mara nyingi akitoa uongozi ndani ya uwanja.
Ujio wake ndani ya Kenya Police FC unatarajiwa kuimarisha safu ya ulinzi ya kikosi hicho kinachopania kupigania nafasi za juu katika Ligi Kuu ya Kenya. Mashabiki wengi wa Polisi wamesema hatua hii ni “saini ya kipekee” itakayoleta uthabiti na uzoefu kwa vijana waliopo.
Onyango mwenye miaka 26 anasifika kwa kuwa mchezaji mwenye nguvu, uzoefu mkubwa wa kimataifa na nidhamu ya kipekee katika safu ya ulinzi. Katika misimu aliyocheza nchini Tanzania, alijijengea sifa ya kuwa beki asiyeogopa changamoto, akiwazuia washambuliaji hatari na mara nyingi akitoa uongozi ndani ya uwanja.
Ujio wake ndani ya Kenya Police FC unatarajiwa kuimarisha safu ya ulinzi ya kikosi hicho kinachopania kupigania nafasi za juu katika Ligi Kuu ya Kenya. Mashabiki wengi wa Polisi wamesema hatua hii ni “saini ya kipekee” itakayoleta uthabiti na uzoefu kwa vijana waliopo.